SIMULIZI YA MAFANIKIO YA LAMECK AMOS KIJANA MDOGO MMILIKI WA KAMPUNI KUBWA


Nashukuru kwa kupata nafasi hii ya kushirikishana nanyi kwa sehemu historia ya maisha yangu   mpaka nilipofika sasa.Nimshukuru kipekee admin na rafiki yangu pia Yunus Joas kwa kuandaa jukwaa hili adhimu ili tuweze kupeana hamasa na kupiga hatua katika Nyanja mbali mbali chanya za kimaendeleo.
Pia nikushukuru wewe kijana uliyeacha shughuli zako ili uweze kufuatana nami katika simulizi hii itakayopelekea kujifunza kwetu sote na kusaidiana pia kiushauri kwa namna moja ama nyingine.Ninafanya kazi na Mpango Mkakati Technologies kama CEO.

Lakini pia ni mhamasishaji wa mambo chanya katika jamii.Pia katika suala zima la kuhamasisha  mimi huendesha more campaign kila mwaka ambayo ipo chini ya mpangomkakati kwa sasa.Kampeni hii ilianzishwa na mimi mwenyewe mwaka 2014 ikiwa na jina la 2014more na kauli mbiu isemayo ishi zaidi ya 2013 katika 2014.Ikiwa na dhumuni kuu moja kuwahamasisha watu kutafuta kupiga hatua zaidi mbele na kukataa kutorudi nyuma au chini ya pale walipokuwa.Lakini madhumuni madogomadogo ya kampeni hii yalikuwa matatu:
  •  Suluhisho la ajira kwa vijana kupitia vijana wao wenyewe (Youth Centred solution to unemployment)
  • Matumizi mazuri ya mitandao ya kijamii na miundombinu ya internet
  • Nafasi ya kijana katika maendeleo ya nchi yake

 Basi nisiende sana huko maana badaye nitawaelezea vizuri na namna tunavyoifanya kampeniIla kwa ufupi kampeni inaendelea mwaka huu ni 2016more "live beyond 2015 in 2016"Yenye kauli mbiu isemayo "INAWEZEKANA".


Nirudi kwa upande wangu binafsi na maisha yangu tangu nazaliwa mpaka nilipo sasaMimi ni mzaliwa wa pili kati ya watoto watano katika familia ya Bw. na Bi. Amos T. Hulilo Baba yangu ni MchungajiMnano tarehe 28. 09. 1988 nilizaliwa.Nimekulia kijiji cha Kamanga wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza mahali ambapo niliishi miaka kumi ya kwanza ya maisha yangu kabla ya familia yetu yote kuhamia mjini kwa majukum ya kikazi ya mzee wangu.
Nakumbuka nikiwa nilisifika kwa kumbukumbu ya kuwakalili wageni waliokuwa wakija nyumbani.Lakini pia nilitamani sana kuwa kondakta wa malori makubwa na kila mara nilipanga mawe na kujenga mfano wa gari na kuingia ndani yake na kuliendesha.

Lakini mara kadhaa pia nilisikika nikisema kwamba nataka kuwa mchungaji baada ya kupata hamasa kutoka kwa mchungaji mmoja aliyetokea wilaya ya Sengerema kuja kijijini kwetu aliyekuwa akiendesha Pikipiki. Nikikumbuka hadithi hizi hunifanya nipate nguvu ya kwenda mbele bila kukata tamaa.

Siku moja alikuja jamaa mmoja anayefanya biashara ya kusukuma torori akiwa na viatu vizuri nikamuuliza umepata wapi akaniambia nimesukuma torori nikanunua, nikawaza kama torori ndio njia hata mi naweza nikatoroka nyumbani kwenda gengeni nikasukume torori nipate Pesa za kununua tafu buti lakini sikufanikiwa kufika nilizuiliwa njiani na ndipo mzee wangu alininunulia viatu hivyo.

Mzee wangu alianza kunionesha umuhimu wa elimu tangu mapema.Alikuwa akitoka kwenye biashara zake za samaki mchana alituketisha mimi na kaka yangu na kuanza kutufundisha namna ya kuandika namba kwenye kibao maalumu alichokinunua pamoja na chaki. Tulifirahia sana kujifunza.

Mwaka 1994 kwa mara ya kwanza nilipelekwa shule ya awali pamoja na kaka yangu hapo kijijini. Nakumbuka tulikalia mawe na tuliandika chini. Enzi zile za kuzungusha mkono juu ya kichwa na uguse sikio ndio uandikishwe darasa la kwanza .Mimi nilihudhuria siku chache kisha nikaacha na kukaa nyumbani.Kaka yangu aliendelea na mwaka uliofuata alijiunga na darasa la kwanza.
Mimi nikiwa nyumbani na harakati zangu za kutimiza ndoto ya kuwa kondakta au Mchungaji.

Maisha yalikuwa mazuri maana nilicheza na watoto wenzangu nikitikisa miti kama gari huku nikichuma Pesa zisizoisha juu ya miti yaani matawi ya miti .Siku moja asubuhi saa mida ya saa tatu katika harakati za kuendelea kucheza na jamaa zangu wavulana na wasichana. Niliruka toka juu ya jiwe kubwa hadi chini kwenye shamba la mahindi.

Nilivyotua chini pembeni yangu niliona nyoka mkubwa sana aliyejikunja nane, sifahamu kama alikuwa amelala au ametega mtego na mimi yawezekana nilikuwa nimepatikana.Haraka haraka nikaingiwa na ukimya na ujasiri wa kutopiga kelele wa kulia wa kukimbia isipokuwa kutembea taratibu kwa kunyata ili mshikaji asishtuke kwamba mi nipo ili anifanyie yake.Huwa nikiifikiria hii sehemu nawiwa kusema sikustahili ila niliachwa kwa sababu Fulani .
Nikafanya kazi ya kusomba mawe jamaa wakampiga na baadaye wakampiga na jembe kama leki lakini Lenye meno marefu na bado akawa na nguvu za kuvutia upande wakeLakini mwishoni tulimwua yule nyoka.

Mnamo mwaka 1996 kwa hiari yangu na kupenda kwangu mwenyewe na kwa maamuzi ambayo mpaka Leo nashangaa niliamua kurudi shule.Kaka yangu aliagizwa udongo mfinyanzi ili atengeneze Sanaa ya shule kwa somo la stadi za kazi nafikiri, mimi pia nikaenda naye kutafuta udongo mfinyanzi na nikatangaza kwenda shule siku iliyofuatia.Asubuhi kulivyokucha kaka yangu alivyoamka na kujiandaa na mimi nilifanya hivyo.

Alipoanza kuondoka nilimfuata nyuma tukaongozana.Nilipofika maeneo ya shule ya awali ambapo zamani ilikuwa stoo ya pamba niliamua kutupa udongo mfinyanzi na kuelekea darasani huku nikimuacha kaka yangu akiendelea kwenda shule ya msingi maana ilikuwa mbele kidogo zaidi ya shule yetu ya vidudu.

Niliingia darasani, Mwalimu alivyouliza wanafunzi wapya na mimi nikaenda kujiandikisha upya, huyu Mwalimu alikuwa mzee sana alifahamika kwa jina la Malele.Mwanzo wa shule haukuwa mwepesi, nilianza hatua ile ile ya kuandika chini na nikiwa sijui kitu.Nakumbuka siku moja nikiwa sijui nifanye nini maana siwezi dada mmoja anaitwa Ester alinitia moyo kwa kuniambia maneno haya, " usihofu utajua tu", haya maneno huwa nayakumbuka hadi Leo na picha ya yale maongezi ipo kichwani mwangu mpaka kesho kutwa.

Yawezekana sikuyaelewa yale maneno lakini naamini yamechangia sana mimi kuwa jinsi nilivyo Leo maana yalinipa moyo wa kutokata tamaa na kuniongezea nguvu ya kwenda mbele zaidi .Usiache kumtia moyo mtu kwa kumwambia maneno mazuri, maneno yana nguvu sana.

Kweli nikaendelea kwa bidii. Kuna wakati nilikosa hesabu zote niliporudi nyumbani nikamsimulia mama, kisha akanifundisha namna ya kujumlisha na kutoa kwa kuhesabu vidole vya mikono tangu siku hiyo kufeli hesabu kwangu ilikuwa historia, hii nayo sitaisahau ASANTE SANA MAMA.Usiishie kuwaandikisha watoto wako shule tu waweza kuwa Mwalimu wao pia.



Mwisho wa mwaka yaliyo mwa majina ya wanafunzi wanaojiunga na darasa la kwanza Shule ya Msingi Kamanga, na mimi nilifurahi kusikia jina langu likitajwa katika nafasi ya 37.Mwaka 1997 nilianza darasa la kwanza chini ya Mwalimu yule yule huku nikiwa sijui kusoma na kuandika nisichoweza kukisoma ila mkali wa kuhesabu namba na kujumlisha na kutoa.Nikiwa darasa la kwanza nikifanya juhudi nijue kusoma na nikafanikiwa.

Nilitumia kitabu cha hadithi ya chombo kilichovunjika kama kitabu changu cha kujifunzia kila nilipopata muda wakati wa mapumziko shule chini ya mti wa mzambarau na niliweza kusoma hata vitabu vingine pia na stori ya dagaa bila kukwama nadhani mnaikumbuka.Nilifanya vizuri darasa la kwanza na kushika nafasi ya sita.Mwaka 1998 Januari nilihamishiwa shule ya Msingi Kirumba jijini Mwanza.

Nilipofika tu mitihani yangu ya kufunga mhula wa kwanza nilikuwa mtu wa 128.Baba hakufurahishwa na hali hiyo ingawaje nilikuwa nimepata alama za juu tu.Mhula uliofuata nilianza utoro na kuchelewa shule nikiwa kundi moja na kaka yangu pamoja na rafiki yangu Paschal.Siku moja nilikimbizwa sana na nikaamua kujipeleka kwa Mwalimu kwa hiari na nikachapwa viboko visivyozidi vitatu ambavyo hata sikusikia maumivu yake sana kiasi cha kulia na tangu siku hiyo nikasema utoro basi Niliendelea vizuri na darasa la Tatu hali yangu yakitaaluma ilianza kubadikikaNikashika nafasi ya nne.

Darasa la nne tukafungana wawili nafasi ya Tatu mhula wa kwanza na mtihani wa taifa nikang'ara kwa kushika nafasi ya kwanza shuleni kwetu.Darasa la tano nikawa wa tatu la sita nikawa wa pili na darasa la saba nikawa namba moja na kushika nafasi ya nne mtihani wa mock wilaya ya mwanza, hii ilikuwa 2003.Nakumbuka darasa la nne na kuendelea ndipo nilipojifunza kuomba Mungu kwa kuelekezwa na mama yanguIkiwa ni pamoja na kufunga kwa mahitaji yangu ya kimasomo.

Hivyo siwezi kusema neno au mimi ni wa tofauti sana lakini Mungu alihusika na bado anahusika kwa kiwango kikubwa na maisha yangu.Baada ya kumaliza darasa la saba sikujiunga na preform one.Nikiwa na rafiki yangu Mandela tuliamua kuanzisha biashara ya genge.Kweli tulipata kisehemu nyumbani kwao tukajenga kipanda na tukawa tunaleta vitu kutoka soko la Kirumba na kuuzaBaada ya kufanya biashara hivyo kwa muda niliondoka kwenda Musoma kwa Mjomba wangu ambapo nilipata fursa ya kusoma preform one mpaka matokeo yangu yalipotoka na nikachaguliwa kujiunga shule ya ufundi Mazengo Iliyopo Dodoma ambayo kwa sasa ndiyo chuo cha mtakatifu Yohana (St. John university).

Hapa nilikuwa miongoni mwa formone wadogo kuliko wote Na siku ya kwanza kuachwa shule mzee alivyonipeleka nililia machoziLakini niliamua kukomaa na sikusumbuliwa na wadogo tulilindwa sanaMaana form two walikuwa wasumbufu sana Basi hapa ufahamu wangu uliongezeka na nikakutana na mazingira mapya na watu wapya na ambayo yalinipa fursa ya kuishi kwenye mfumo mpya wa maisha ambao ulikuwa na Uhuru zaidi wa kujitegemea na kuamua japokuwa nilikuwa nimebanwa na sheria za shuleNilijisikia vizuri na fahari sana kuwa mmoja wapo wa wanafunzi wa shule hii japo chakula hakikuwa kizuri sana.Nilipomaliza form two tuliambiwa tuchague shule zingine maana Mazengo itakuwa chuo kikuu.

Mimi nilijaza Moshi Technical na nilipelekwa huko Nikasoma form three na form fourKisha nikafaulu kwa daraja la kwanza point 11 na nikachaguliwa kujiunga na shule ya sekondari Ilboru combination ya PCMWakati nikiwa form two baba alinitia moyo niwe daktari wa binadamu lakini nilikataa.

Nikiwa form 3 nikiacha somo la Baolojia na kusoma jiografia Huku nikiendelea kushikilia wazo la kuwa mhandisi wa talakilishi na kuwa mchumi ukiwa mpango kando wanguNilipomaliza kidato cha nne na baada ya kuwa na matokeo mazuri nilirudi kutamani sana kuwa Dk. Kwa sababu fulani fulani ambazo badaye niligundua si za msingi.

Niliwaza sana mpaka nikaugua mwishowe nikamwambia baba.Alichofanya alinishauri na kisha akanipeleka kwa daktari baada ya hapo nikawa vizuri na maisha yakaendelea Maisha Ilboru yalikuwa mazuriNilisoma kwa bidii sana .Huku nikiahirisha kwenda nyumbani na kubaki Arusha ili Pesa yangu ya nauli ninunu vitabu na kusoma masomo ya ziada maana vitabu vilikuwa ghari kidogo tofauti ni vya o level .

Niliendelea kutamani na kumwomba Mungu anipe nafasi ya kujiunga chuo kikuu cha Dsm kwa masomo ya uhandisi wa talakilishi Hapa kidogo nilianza kuhisi mwanga kwa mbali wa badiliko la maisha yangu Juu ya nilivyowaza na nilivyoyaona maisha yangu .Sikuwahi kujiunga na club yoyote lakini kwa mara ya kwanza nilijiunga na English Club Mi sikujua kitu kingine zaidi ya kusoma tu na kusali pamoja na michezoNilipoanza kwenda debate club ndipo Nilipoona kitu cha ziada kwa wenzangu.Waowalikuwa na uwezo wa kujenga hoja kwa lugha ya kingereza tena kwa kujiamini hata kwenye uwepo watoto wa kike na mimi sikuweza japo nilijaribu mara kadhaa huku nikipiga mweleka kwa vigugumizi vingi na kujiumauma Nilijiona duni sana.Nulijiona mimi si bora sana.
Pia nikakumbuka jinsi nilivyo na meno ambayo hayajapangika vizuri ikanisumbua sanaNilipomaliza kidato cha sita ndugu zangu walinitaka nibaki Arusha wanitafutie shule ya kufundisha kwa muda  Ila nilikuwa na mpango wa kwenda kuanzisha tuition centre.

Kwa hiyo Nilirudi nyumbani mwezi wa Tatu 2010.Nikiwa na rafiki yangu Hamis ambaye ni daktari kwa sasa tulitafuta centre tukaanza Hatukuwa na wanafunzi wengi sanaLakini baada ya siku chache niliitwa na mwalimu wangu aliyenifundisha masomo ya ziada nikiwa kidato cha tano alinisihi na kunibembeleza niende nikafundishe advanced physics na mamlaka yote yatakuwa juu yangu na hata fedha nitakazotoza zitakuwa zangu.

Kwa mara ya kwanza milikabidhiwa darasa Lenye wanafunzi zaidi ya hamsini na nikaanza kufundisha huku nikijipatia Pesa nyingi kwa wakati huo.Nilifanya kazi hiyo mpaka matokeo yangu yalipotoka Wanafunzi walinikubali sana Na hata matokeo hayakuniangusha pia Matokeo yangu yalipotoka nilifaulu kwa daraja la kwanza tena point 5 Nikaomba kujiunga Chuo kikuu cha Dar es salaam kwa masomo ya shahada ya kwanza ya uhandisi wa Tarakirishi na Teknolojia ya Habari (BSc. in Computer Engineering and IT).Nikijisikia furaha sana kutimiza sehemu ya malengo yangu ya kusomea kitu nikichokitaka.

Nilimshukuru Mungu sana kwa hatua hiyo Binafsi changamoto ambayo ilinisumbua kwa muda mrefu ni kitojiamini na kujiona mnyonge japo kikawaida usingeweza kunigundu  Basi mnamo mwezi oktoba 8. 2010 nilijiunga rasimi na chuo kikuu cha Dar es salaam Hapa malengo yangu yalikuwa kusoma kwa bidii na kufaulu kwa alama za juu kama kawaida nikiwa na ndoto za kufanya kazi na makampuni makubwa kama Tigo, Vodacom, TTCL au kubaki kuwa mkufunzi wa chuo Hiyo ndiyo picha niliyoingia nayo chuo kikuu.


Na kila usiku mmoja niliyoenda kulala nililala kwa amani nikiitazamia haja hiyo ya moyo wangu, lakini vile vile niliamka asubuhi kwa shauku kubwa nikijituma kulifikia hiloNikiendesha mjadala mkubwa sana nikiwa semester ya kwanzaNa semester ya pili Na nikifaulu kwa GPA nzuri sana Niliwiwa na kujiskia kweli nastahili kuwa Mwalimu Na wengi waliniambia hivy Na kunisifia kuwa ningefaa kuwa mhadhiri wa chuo kikuu.


Kipindi hicho chote nilikuwa na mitazamo ile ile niliyotoka nayo huku chini Natumai tupo pamoja, naomba kuishia hapo na kesho nitaendelea maana sehemu inayofuatia ndiyo chanzo cha mimi kuamua kuwa mjasiriamali na mhamasishaji pia.

 Asanteni kwa kunisikiliza

ITAENDELEA ………