MWENDELEZO WA SIMULIZI LAMECK AMOS HULILO



Nilianza kushawishika na kujisikia kugombea nafasi ya uongozi kuwawakilisha mwaka wa kwanza kama mbunge waoNilichukua fomu huku nikiwa na uoga na kitojiamini ila nilijitahidi kutokuonyesha kwa hali ya nje.Sikutoa taarifa kwa wazazi wangu kwamba nimeamua kugombea uongozi maana wangenizuia kwa sababu miaka hiyo migomo ilikuwa mingi na watu walifukuzwa chuo Baada ya mchakato mzima kufanyika sikupita kwenye mchujo.

Lakini pia wakati huo nilikuwa nimejiunga na kikundi fulani ndani ya Fellowship yetu ya dini kinaitwa IT Bench Huko tulifanya shughuli zote za IT na media Sana sana tulifanya shughuli za kurekodi video wakati wa mikutano ya injili Nikiwa humo mwaka wa pili mwanzoni niliteuliwa kuwa mwenyekiti wa IT Bench.
Niliiongoza kwa mafanikio makubwa sana ndani ya mwaka mmoja tu na tukapewa kuwa idara
Katika uongozi wangu tulifanikiwa kununua vifaa vingi ikiwa ni pamoja na kuongeza ujuzi na mipaka ya kazi hadi nje ya chuo Tulitengeneza na kuprint kadi za harusi.Kutengeneza DVD za Matukio mbali mbali Hapa ndipo nilipoanza kuingiwa na element na moyo wa kufanya biashara Kwa bidii Hapo kabla nikiwa mwaka wa kwanza nilifanya lakini haikuwa kama mwaka wa pili  Nakumbuka mwaka wa kwanza nilijiunga na wenzangu watatu tukajiita TRUST COMPANY.

Hapa tulifanya biashara ya kuuza DVD empty pamoja na CD empty ikiwa ni pamoja na kufanya vomputer maintainance and repair Wakati nikiwa mwaka wa pili kasi yangu ya kutaka kuajiliwa ilipungua. Matendo yangu yaliashiria kwamba nilipenda siasa.

Na nilifuatilia kwa karibu sana siasa za chuo na hata za kitaifa Wakati huu migomo ilikuwa Mingi na ilinigusa sana ila sikuwa msitari wa mbele sana Nakumbuka nilitokea kupenda sana mambo ya uongozi Katika maktaba yangu ndogo ya vitabu ambavyo sikuwahi hata kuvisoma maana sikuweza na sikuwa na kingereza kilichonyooka nilikuwa na kitabu cha John C. Maxwell chenye kichwa kisemacho "21 irrefutable laws of leadership ".

Kulingana na kiu yangu ya uongozi nilianza kukisoma bila kujali naelewa vizuri au la Hapo ndipo tabia ya kusoma vitabu ilipozaliwa kwangu Nilikisoma kila nilipopata muda hata kama dakika moja tu Nilikisoma nikiwa kwenye daladala hata ofisi za watu Nilikisoma darasani pia nikisuburi mwalimu aingie  Nilianza kununua vitabu vingine Na kuvisoma pia.

Baada ya muda tabia hiyo ikawa sehemu ya maisha yangu japo ilinichukua muda kusoma na kumaliza kitabu kimoja Nakumbuka siku moja nikiwa na test nilishindwa kujizuia nikajikuta nasoma kwanza kitabu cha Maxwell ili kiishe ndio nisomee mtihani.Nashukuru Mungu nilipata Uwezo wa kumudu yote  Mwaka huo ulitokea mgomo na viongozi wengi sana walifukuzwa na wengine kusimamishwa chuo Mimi pia nilihofu sana kufukuzwa maana kuna wakati nilikuwa na kundi la wanafunzi wenzangu pale utawala nikapanda juu ya kiti kuhamasisha na kuwatoa uoga maana tunadai haki zetu hii iliitwa kutoa modality.

Nashukuru Mungu Nilipona katika hili Darasani nilijitahidi kujenga mahusiano mazuri na kila mwalimu aliyenifundisha Nilifuta ubao kila mara na nikisaidia kufunga projector na kuitoa katika kila kipindi Na watu walinifahamu kwa hilo .Baadhi hawakuipenda sana tabia hiyo japo haikuwapunguzia chochote ..Na baadhi walidhani nafanya hivyo nikiandaa mazingira ya kushinda uongozi kwa kipindi ambacho kilikuwa mbele Lakini mimi sikujali.

Nilifanya kila kilicho chema machoni pangu hata kama watu hawakuniunga mkonoNilitamani sana wanafunzi tuwe na maisha yatakayotoa mchango kwa jamii hata tungali shule.Nikiwa mwaka wa pili yaliyokea mafuriko hapa Dsm na watu waliachwa bila makazi Niliguswa sana na jambo hilo nikaamua kutoa wazo na kuhamasisha wanafunzi wenzangu tuchange tulichonacho ili tuwasaidie.
Kweli tulikusanya michango japo kulikuwa na changamoto za mwitukio wa watu.
Hivyo tulipata kiasi cha fedha na kisha mimi na mbunge wangu kwa wakati ule Bahati Kamwela tulipeleka msaada wa vitu mbali mbali vilivyonunuliwa kwa kutumia fedha iliyokusanywa.Haya yote yalizidi kunifanya nipende mambo ya uongozi na yalinifundisha kuwa kiongozi maana yake nini hata kama hauna cheo Fulani.

Muda ulipofika nilichukua fomu ya kugombea ngazi ya ukatibu wa college (COICT)
Hapa nilipita mchujo na kugombea lakini kura hazikutosha Ila nilikuwa mbunge wa kuteuliwa ikiwa tiketi ya kuwa mjumbe wa kamati kuu ya college kama mwakilishi wa taaluma.

Nilifanya kazi kwa bidii kushughulikia matatizo ya wanafunzi wenzangu Pia niliteuliwa kuwa naibu waziri wa mawasiliano na Habari katika serikali ya wanafunzi .Wakati huo nilifanya bidii kunoa kingereza changu japo hakukuwa na wengi wa kuongea nao hivyo ilibidi niongee peke yangu au nilisikilize speech a kuzirudia.

Nilipakuwa video za watu wengi mashuhuri kutoka youtube na kuzidikiliza nikiwa na lengo la kujifunza .Kabla nilisumbuliwa sana na muonekano wangu Hususa ni mpangilio wa meno yangu ya mbele hayakuota kwa mpangilio mzuri Hili lilinisumbua siku nyingi na bado liliendelea.

Pia nilichukua hatua ya kujifunza zaidi kupitia historia za watu wengine kama Martin Luther King Jr., Malcom X, Cheguavara, Mwl. Nyerere, Patrick Lumumba, Mobutu, Nkwame na wengine wengi
Historia za watu hawa na yale waliyoyafanya yalinipa kujifunza na sababu zaidi ya kulitafuta kusudi la kuishi kwangu.

Walinipa sababu ya kutokata tamaa hata kama mazingira ni magumu na watu hawaniungi mkono
Lakini kila mara nilijitahidi kuishi kile nilichokismini Mara suala la kuajiliwa likafutika nikaanza kuwaza zaidi kumiliki kampuni na kusaidia watu kujitambua Sikutamani tena maisha ya kwenda ofisi moja hadi nyingine kuomba kazi Nakumbuka siku moja baba nilienda kumtembelea baba hapa Nairobi nchi jirani ya Kenya Kwa kipindi hicho na yeye alikuwa masomoni huko.

Alinitaka nimweleze ni nachoweza juu ya maisha ya mbele na mipango niliyonayo Tuliongea mengi na nikamwambia jinsi ninavyoguswa na maisha duni ya watu na ambavyo ningependa kuwasaidia wajikwamue kwa kadili nitakavyoweza. Na nikamwambia sina mpango wa kuajiliwa Ila niko radhi nianze na kitu chochote hata kama ni kidogo.

Alipenda mawazo yangu na moyo nilioonyesha wa kutaka kuwasaidia watu, lakini akanishauri na kunisihi niajiliwe walau kwa miaka mitano kisha ndio nianze shughuli zangu Nilikubali ushauri wake kwa wakati ule na kuahidi kuufanyia kazi ili hali ndani bado nilikuwa na maamuzi yale yale huku nikiwaza namna ya kumshawishi akubaliane na maamuzi yangu ili nimwondoe wasi wasi.

Nikiwa mwaka wa pili mwisho mimi pamoja na Rafiki zangu watatu waliokuwa wamehitimu masomo mwaka huo tulianzisha kampuni ya IT and Media lakini haikifanikiwa kukua na ilikufa pole pole na kusambaratika.

Nikiwa mwaka wa Tatu 2013 niliendelea kusoma vitabu na hapa nilikuwa nimejitoa IT Bench na kuwa mwanachama wa kawaida Niligombea uongozi tena nafasi ya Mwenyekiti wa college niliyokuwa nikisoma na nikapita bila kupingwa.Hii ilinifundisha kutokata tamaa na kutoyaangalia sana madhaifu uliyonayo lakini kuangalia na kutumia nguvu au uimara wako katika maeneo Fulani.

Nikiwa mwaka wa tatu zilitoka nafasi za kujiunga na kozi fupi ya uongozi iliyoitwa chini ya East African Uongozi school ambayo ikijumuisha wanafunzi wa vyuo mchanganyiko Afrika Mashariki.Nilituma maombi yangu na nikaitwa kwenye usaili Baada ya usaili mimi sikuchaguliwa kujiunga Niliumia sana kuikosa nafasi ile muhimu kwangu.

Baada ya kukosa na kuumia nikatulia na kukubali kwamba nimekosa ile nafasi  Maana hata baba nilishamwambia na faida zake pia .Baada ya kukubaliana kuwa nimekosa na kukiri wazi mbele yangu kwamba waliopata wameonekana kuwa na vigezo kuliko mimi Nikijiuliza tena sababu za mimi kutaka ile kozi kwa shauku kubwa ilikuwa ni nini?Je ni malipo ya dola za kimarekani 15 kwa siku?Au nilitaka sana kujifunza mambo ya uongozi ?Jibu langu likawa dola 15 ndio lakini zaidi sana kujifunza Basi nikampigia simu Mwalimu alinifanyia usaili nikamuomba nipate nafasi ya kusoma bila kulipwa chochote na nikamuahidi sitakuwa na Madai yoyote.Akaniambia haina tabu we siku ya kuanza njoo.

Nikafurahi sana Siku wanafungua mafunzo kwa sherehe sikuweza kuhudhuria nilikuwa safarini kwa mahafari ya baba yangu alikuwa anapata shahada yake ya kwanza Bahati nzuri siku hiyo usiku ndiyo nilifika dar kutoka Nairobi.Kesho yake asubuhi mapema kabla darasa lianze nilienda kwa mwalimu akaniambia watu wamejaa na yeye Hana mamlaka ya kuongeza huku akisahau kuwa aliniambia nije siku ya kuanza Nilijisikia kuishiwa nguvu maana nakosa kozi hivyo.

Lakini katika maneno yake aliniambia VC ndiye mwenye mamlaka Na huyu hakuwa mwingine alikuwa Prof. Rwekaza Mkandala ambaye bado ni VC hadi sasa Nikamfuata ofisini na kujitambulisha na kumweleza kila kitu na kwamba ninachohitaji ni kusoma tu na si vinginevyo.Naye pia akaniambia itakuwa ngumu maana kuna gharama ambazo wenzangu wanalipiwa sasa.

Nikamwambia nikizijua hizo kama zipo ndani ya Uwezo wangu nitalipa tu Akakaa kimya kwa muda kisha nikamuaga naondoka wakati nanyanyuka kwenye kiti niondoke maana imeshakuwa nongwa akaniambia we nenda coordinator akwambie hizo gharama kisha utaamua kujiunga au kuacha.Hilo jibu likanipa furaha maana nikajua nishajiunga japo mfukoni sikuwa na hata senti moja ya kulipa.

 Nikaenda nikamwambia coordinator VC amekubali nijiunge ila ameniambia nikuone unijulishe gharama ili nilipe.Coordinator akasema sawa haina tatizo nione wakati wa mapumziko baada ya kipindi Kweli baada ya hapo nilienda kumwona na akaniambia gharama zote ni dola za kimarekani 180 sawa na tsh. 290,700/= maana exchange rate kwa wakati huo ilikuwa sh 1615/=Nikaona ni nyingi kwangu maana sikuwa na kitu wakati huo na nilibaki chuo kushughulikia masuala ya wanafunzi wenzangu ila nikamwambia haina tatizo nitalipa kwa awamu.

Basi maisha yakaendelea wakati wa kozi nilitokea kupendwa na watu wote darasani hata walimu pia.Pia kama kawaida mimi ndiye niliyepewa jukumu la kufunga na kuondoa projector wakati wa session, hapo nikaanza kuona umuhimu wa kihelehele changu kuwafungia walimu projector na kufuta ubao Kule darasani bila kudai chochote wala bila kutumwa na mtu.

Nilijitahidi kutokuonyesha kwamba mimi silipwiNa nilifanya hivyo. Nilijitahidi kutoa maoni ya namna ambavyo tungeweza kujifunza zaidi na ilinipa fursa ya kushinda nafasi ya ukatibu mkuu katika uongozi wa wanafunzi huku nikipita kwa kura nyingi sana kuliko mpinzani wangu.

Nilifanikiwa kusoma na kumaliza kozi vizuri.changamoto nilizokutana nazo wakati wa kujiunga na masomo niliyojifunza pamoja na watu niliokutana nao, nikajikuta nimekuwa tofauti na mwenye mawazo chanya zaidi.Kwa kweli nikiwa uongozi school nilijifunza mengi.

Nilikuwa najua kutengeneza connectionLakini hapa nilijifunza zaidiBaada ya hapo nilipata fursa kuhudhuria debate ya wanafunzi wa vyuo vikuu wa yumuiya ya Afrika Mashariki  Ilifanyika pale JB Belmont Hotel Posta .Kiukweli nilikuwa nimeyumba kiuchumiIla nilikuwa na suti ambayo mzee alikuwa ameninunulia Kwa hiyo nikawa nahudhuria kila siku, hapo nipo smart sana but kwa mfuko sina kitu Ila uzuri tulipata lunch na nilikuwa na Pesa kidogo ya kunisaidia kurudi chuo kwa daladala
Nilijitahidi kujenga mahusiano na watu wapya.

Na nikapata marafiki wengi Huko kwa mara ya pili nilikutana na Raymond Maro ambaye alikuwa Balozi wa vijana anayewakilisha Tanzania kwa vijana katika jumuiya ya afrika mashariki Hivyo siku iliyofuatia nilipata fursa ya kuzungumzia tukio lile kwenye redio Huu ndio ulikuwa mwanzo wangu wa kuanza kuengage media.Sikuwa na ujasiri sana lakini kwa nje sikuonyesha hofu wala ugeni wowote

Interview ya kwanza tulifanya na East Africa Radio. Na hii ilichukua dakika kumi na tano hewani.Sio Siri hii kwangu ilikuwa ni hatua kubwa sana na nillizidi kuhamasika na kupenda masuala ya  diplomasia na siasa kwa ujumla.Tulivyotoka nje tulikutana na Constantine Mihambo wa capital radio naye akaomba tufanye naye interview Hii ya sasa ilikuwa recorded ambayo ingeruka kesho yake kwenye kipindi cha morning jam ambacho yeye ndiye mtangazaji Niliwataarifu watu wasikilize na nilipata positive feedback nyingi.

ITAENDELEA ……….