Ili ufanikiwe hupaswi kufanya kila kitu
.Unapaswa kuwa makini kujua kipi unapaswa kufanya na kipi hupaswi kufanya
.Jumatano hii tulivu nataka nikuuleze mambo ambayo watu waliofanikiwa huwa hawayafanyi
.
1.
Hawaishi
kwa yaliyopita .
Watu waliofanikiwa huwa wanaishi kwa
methali uliyofuundishwa na mwalimu wako kuwa yaliyopita si ndwele tugange
yaliyopo na yajayo .
Kamwe usifikirie mambo yaliyopita ,iwe
ni biashara iliyoharibiwa ,iwe ni kazi au mahusiano huwa yanaumiza na kushusha
morali ya kusonga mbele .Shida ni kwamba
ukifikiria sana yaliyopita huwezi kufanyia kazi ndoto yako .Ni vizuri sana
kujua maisha ni leo lakini hasa kesho na
si jana .Kwanini unakumbuka ulivyoshindwa jana ??? kwanini unakumbuka mahusiano
yaliyoovunjika???
Unapaswa kujua kuwa lililoshindikana
jana leo linaweza kufanyika kwa uzuri na uwaredi mkubwa sana .Mwimbaji mmoja wa
Nyimbo za injili katika Albamu yake moja anasema "Jana imepita ,leo ni
siku mpya tengeneza njia yako ili Bwana atende ".
2.Hawafanyi kisichoendana na ndoto zao
Watu waliofanikiwa huwa kabla ya kufanya
huwa wanajiuliza maswali kama haya : kwanini nifanye hiki au kile?? je
kinafaa?? je ni sahihi kwa mazingira
haya ???
Rafiki kama unataka kufanikiwa hupaswi
kufanya kila kinachokuwa mbele yako.Ni muhimu kujua kitakusaidia nini pindi
ukikifanya na utakosa nini usipofanya .
3.Hawaamini kuwa unaweza kumfurahisha
kila mtu
Huwezi kumfurahisha kila mtu kwa kile
unachofanya .Watu waliofanikiwa wanalijua hili .Ni muhimu sana kujua kuwa hapa
dunia watu wote hawawezi kukufurahia na hivyo usifanye vitu kwa kuwafurahisha
watu .Fanya lile liloko moyoni mwako na ndani ya uwezo wako kama kweli unataka
kufanikiwa .
4.Hawaamini kuwa kuna mtu hakosei
Watu waliofanikiwa huamini kuwa ili
ufanikiwe lazima ukosee na makosa ni sehemu ya kujifunza .Hakuna mtu ambaye
amekamilika .Hujifunza kutokana na makosa yao ya kila siku na kupitia makosa
hufanya makubwa.Ili ufanikiwe usiogope kukokosea maana kukosea ni sehemu ya
maisha.
5.Hawaachi kujiuliza kwanini wako hapo
walipo
Watu waliofanikiwa mara zote hupenda
kujiuliza ni kwanini wapo hapo walipo na hii ndo tofauti kubwa kati ya watu
waliofanikiwa na wale ambao hawajafanikiwa.Watu waliofanikiwa hujiona kuwa wao
siyo tu waliosababisha kufika pale walipo katika mafanikio hata kama wametumia
nguvu zao wenyewe kufanikiwa .Lakini pale waliposhindwa kitu waliamini wao ndio
sababu ya kushindwa kwao bila kumlaumu mtu mwingine .
6.Hawaachi Kuona Picha kubwa ya maisha
yao
Watu waliofanikiwa huamini kuwa picha
kubwa ndiyo pekee inayowawezesha kufanya mambo makubwa na kufanikiwa .Kila siku
wanawaza mambo makubwa.Hawaangalii walipo sasa na wana nini lakini huangalia
mambo ya mbele sana .
Ni muhimu sana ukitaka kufanikiwa
usiangalie pale ulipo leo lakini uweke picha kubwa kichwani mwako kuwa unaweza
kuwa mtu mwenye mafanikio makubwa.Kwanini unaangalia umaskini wa familia
yako??? kwanini unaangalia mazingira??? .
7. Hawaachi Kuvumilia shida ya muda kwa
faida ya miaka mingi .
Watu waliofanikiwa huwa huwa hawakwepi
maumivu ya muda .Wao ni wavumilivu sana
tofauti na maskini ambaye hutaka kufanikiwa haraka au kufurahia raha ya muda
mfupi .
Ndugu kama una nia ya dhati ya
kufanikiwa ni muhimu sana ukawa mvumilivu katika mambo unayoyafanya .Acha kutafuta
raha ya muda mfupi huku ukijiua mwenyewe .
0753836463
Kwa maarifa zaidi tembelea blog hizi