JIFUNZE SIRI HIZI ZA WATU WALIOFANIKIWA ~Joas Yunus




Ili ufanikiwe hupaswi kufanya kila kitu .Unapaswa kuwa makini kujua kipi unapaswa kufanya na kipi hupaswi kufanya .Jumatano hii tulivu nataka nikuuleze mambo ambayo watu waliofanikiwa huwa hawayafanyi .

1.  Hawaishi kwa yaliyopita .
Watu waliofanikiwa huwa wanaishi kwa methali uliyofuundishwa na mwalimu wako kuwa yaliyopita si ndwele tugange yaliyopo na yajayo .
Kamwe usifikirie mambo yaliyopita ,iwe ni biashara iliyoharibiwa ,iwe ni kazi au mahusiano huwa yanaumiza na kushusha morali  ya kusonga mbele .Shida ni kwamba ukifikiria sana yaliyopita huwezi kufanyia kazi ndoto yako .Ni vizuri sana kujua maisha ni leo lakini hasa  kesho na si jana .Kwanini unakumbuka ulivyoshindwa jana ??? kwanini unakumbuka mahusiano yaliyoovunjika???

Unapaswa kujua kuwa lililoshindikana jana leo linaweza kufanyika kwa uzuri na uwaredi mkubwa sana .Mwimbaji mmoja wa Nyimbo za injili katika Albamu yake moja anasema "Jana imepita ,leo ni siku mpya tengeneza njia yako ili Bwana atende ".

2.Hawafanyi kisichoendana na ndoto zao
Watu waliofanikiwa huwa kabla ya kufanya huwa wanajiuliza maswali kama haya : kwanini nifanye hiki au kile?? je kinafaa??  je ni sahihi kwa mazingira haya ???

Rafiki kama unataka kufanikiwa hupaswi kufanya kila kinachokuwa mbele yako.Ni muhimu kujua kitakusaidia nini pindi ukikifanya na utakosa nini usipofanya .

3.Hawaamini kuwa unaweza kumfurahisha kila mtu
Huwezi kumfurahisha kila mtu kwa kile unachofanya .Watu waliofanikiwa wanalijua hili .Ni muhimu sana kujua kuwa hapa dunia watu wote hawawezi kukufurahia na hivyo usifanye vitu kwa kuwafurahisha watu .Fanya lile liloko moyoni mwako na ndani ya uwezo wako kama kweli unataka kufanikiwa .

4.Hawaamini kuwa kuna mtu hakosei
Watu waliofanikiwa huamini kuwa ili ufanikiwe lazima ukosee na makosa ni sehemu ya kujifunza .Hakuna mtu ambaye amekamilika .Hujifunza kutokana na makosa yao ya kila siku na kupitia makosa hufanya makubwa.Ili ufanikiwe usiogope kukokosea maana kukosea ni sehemu ya maisha.

5.Hawaachi kujiuliza kwanini wako hapo walipo
Watu waliofanikiwa mara zote hupenda kujiuliza ni kwanini wapo hapo walipo na hii ndo tofauti kubwa kati ya watu waliofanikiwa na wale ambao hawajafanikiwa.Watu waliofanikiwa hujiona kuwa wao siyo tu waliosababisha kufika pale walipo katika mafanikio hata kama wametumia nguvu zao wenyewe kufanikiwa .Lakini pale waliposhindwa kitu waliamini wao ndio sababu ya kushindwa kwao bila kumlaumu mtu mwingine .

6.Hawaachi Kuona Picha kubwa ya maisha yao
Watu waliofanikiwa huamini kuwa picha kubwa ndiyo pekee inayowawezesha kufanya mambo makubwa na kufanikiwa .Kila siku wanawaza mambo makubwa.Hawaangalii walipo sasa na wana nini lakini huangalia mambo ya mbele sana .

Ni muhimu sana ukitaka kufanikiwa usiangalie pale ulipo leo lakini uweke picha kubwa kichwani mwako kuwa unaweza kuwa mtu mwenye mafanikio makubwa.Kwanini unaangalia umaskini wa familia yako??? kwanini unaangalia mazingira??? .

7. Hawaachi Kuvumilia shida ya muda kwa faida ya miaka mingi .
Watu waliofanikiwa huwa huwa hawakwepi maumivu ya muda .Wao ni wavumilivu  sana tofauti na maskini ambaye hutaka kufanikiwa haraka au kufurahia raha ya muda mfupi .

Ndugu kama una nia ya dhati ya kufanikiwa ni muhimu sana ukawa mvumilivu katika mambo unayoyafanya .Acha kutafuta raha ya muda mfupi huku ukijiua mwenyewe .

0753836463
Kwa maarifa zaidi tembelea blog hizi