KUISHI NA WAFANYAKAZI WA NDANI By: kelvin Kitaso, 0713804078





Katika kipindi hiki kuna matukio mengi mabaya yametokea yakihusisha wafanya kazi wa ndani kama ndio chanzo cha hayo yote, katika jamii watu hawa wamekuwa wakidharahulika sana na wakati mwingine wamekuwa wakiitwa majina majina mabaya ya kudharauliwa. Hii imepelekea kazi hii kuonekana ni kazi ya kawaida sana na haina thamani na kuna mabosi wengine wamekuwa wakiwadharau sana na kuona ni watu wenye shida, dhiki na umaskini mwingi. Hali hii imeibua tabaka kubwa kati ya mabosi na wafanya kazi hawa na imezua migogoro ambayo wengine imeishia pabaya kwa kuacha alama mbaya.

Aidha kuna familia nyingine zimeishia pabaya sana pale ambapo mwanandoa mmoja wapo anapojihusisha moja kwa moja kimapenzi na mfanyakazi wa ndani na wengine wamezaa nao, na kuna wafanya kazi wa ndani wengine wamevunja ndoa za mabosi wao na wao kukaimu nafasi hizo. Surah ii imelenga kukueleza namna njema ambayo unaweza kukaa na wafanyakazi wa ndani.Wafanya kazi wa ndani ni watu muhimu sana kwa kuwa wanasaidia sana majukumu ya familia kutendeka kirahisi.
amna njema ya kuishi na mfanyakazi wa ndani:-

1    1.  Mfanye kuwa rafiki yako.
Jambo la msingi ambalo unaweza kulifanya kwa mjakazi wa ndani kwako ni kumfanya kuwa rafiki. Yohana 15:15, Yesu anasema “siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo Bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu”.

Njia pekee ambayo bosi anaweza kukamata ukaribu wa mfanyakazi wake ni kumfanya kuwa rafiki, Yesu anasema tumekuwa marafiki kwa kuwa tunashirikishwa ayatoayo kwa Baba yake. Urafiki unaimarika pale kunapotokea ushirikishaji. Ukitaka kuukamata kwa urahisi moyo wa mfanyakazi wako na akaanza kuishi kwa uaminifu kwako na akawa kama ndugu ni pale unaanza kuishi kwa kumshirikisha mambo mengi uliyonayo na unayoyapata.

Ukienda kuwanunulia wanao nguo au zawadi naye pia mchukulie, unapowatoa wanao kwenda kutembea nae pia mchukue, unapokula na wanao mezani nae pia kuleni nae, mfundishe mambo mengi kuhusu maisha.Watumishi wengi wanaangaika kufundisha watu nje ya nyumba zao lakini wale wa nyumbani hawajui hata kama ni waalimu wazuri.

  2. Faida za wazi zitakazotokea kama kutakuwa na urafiki:-
  •   Atakuwa wazi kukushirikisha mambo ambayo hata wazazi au marafiki zake hajawahi kuwaambia.
  •     Atakuwa akifanya kazi zote kwa moyo wa kupenda na uhiyari na wala si ilimradi.
  •      Atakuwa akijituma kufanya mambo ambayo si kazi zake ila tu ni kwa sababu ajua anamsaidia rafiki yake.
  •         Kuna ujuzi ambao unao utaanza kuambukizwa ndani yake.
  •   Maono, tabia, na shauku ulivyonavyo vitaanza kuambukizwa ndani yake na atajiona anawajibu wa moja kwa moja wa kukuunga mkono.
  •    Atawatumikia watoto wako kwenye ngazi ya uzazi na hata kama haupo watoto wako hawataona kupungukiwa. Ataishi na upendo wa hali ya juu sana kwa watoto wako)
  •   Atakujali na kujali mambo yako na atafanikiwa kujua nini unapenda na atakutendea hayo ili rafiki yake uzidi kufurahi.
  • Ataona anawajibu wa moja kwa moja wa kulinda na kutunza mali zako.


              Epuka kuishi naye kama mtumwa

Watu wengi wamedhania kuishi kwa namna hiyo na kuwafanya wafanyakazi wao kuwaogopa na kutetemeka wanapowaona huo ndo ufahari, wao hufurahi wakiona wamegonga mlango sebuleni kila mtu akakimbilia ndani, na mbaya zaidi kuna familia ambazo mfanyakazi wa ndani anakula jikoni anapopikia na haruhusiwi kula na watoto wa bosi wake, hali hii ni mbaya sana, ebu yatazame mambo yanayoweza kutokea hali kama hii inapotokea:-
  •    Anaishi kwa uoga, na hata akionyesha nidhamu inakuwa siyo halisi bali ni nidhamu ya uoga.
  •     Anaishi kwa wasiwasi kama mtu hasiye na makao na wakati wowote anaweza kuondoka.
  •        Hana raha na maisha anayoishi, anaishi kwa kuvumilia tu.
  •       Hana uhuru na kitu chochote kisicho miliki yake.
  •         Anafanya kazi zake kwa uogo ili asije kusemwa.
  •       Hana uchungu na miliki ya bosi wake kwa kuwa anaona kama haimuhusu.
  •        Anaweza kuishi nawe kama adui na akawatazama watoto wako kama watoto wa adui zake, na kwa kuwa hawezi kushindana nawe kuna uwezekano mmkubwa sana akajilipizia kisasi kwa watoto wako pale unapokuwa haupo.
  •      Ni nadra sana kutekeleza mambo katika viwango unavyovitaka kwa kuwa unavihitaji kwa kuwa haupo moyoni mwao.
 

3   3.   Wape uhuru.
Mabosi wengi wanaishi na wafanya kazi wa ndani ila wamewafanya kutokuwa huru kabisa kwao. Na hii imepelekea wafanya kazi hao kutokuwa huru hata kama mambo yanawasumbua.  Kila uhuru hakikisha uwe na mipaka ya kufanya na ya kutokufanya, uhuru hapa namaanisha katika mambo ambayo yanasababisha ustawi wa maisha yao katika upande wa kimwili na wa kiroho.

4.     Mjengee maisha bora ya baadae.
Hivi utajisikia raha gani utakapokuja kuona baada ya miaka 10 ya kukaa na huyo mfanyakazi unapata taarifa kuwa ni tajiri sehemu Fulani na anakutaja kwa namna ulivyomsaidia kufikia hapo.

Ni mabosi wachache sana ambao wafanyakazi wao wanawasifia kuwa wamesaidika kufikia maisha bora baada ya kuishi nao, ila mabosi wengi huwa wanaangalia maisha yao tu. Jitahidi uangalie na maisha ya mfanyakazi wako kuwa atakuja kuwa na maisha gani baada ya kuishi nawe, mwazie yaliyo mema na mtendee yaliyomema ilia je kuwa na maisha yaliyo mazuri baadae.

Si vyema unaishi na mfanyakazi miaka hata 3 halafu anatoka hajui huko anapoena anaenda kufanya kitu gani, mfundishe ujuzi mbalimbali, katika kiwango cha mshahara unaompa kiasi kingine kidogo unaweza ukawa unamuwekea akiba hata benki na wakati mwingine unaweza kumfungulia hata biashara ndogo ya usimamizi mdogo ili tu aje kuwa na maisha bora ya baadae.

5.     Kuwa mwalimu kwake.
Kuna mambo hayafahamu na ukweli ni kuwa amekulia kwenye mazingira tofauti na kuna tabia ambazo amekuwa nazo na kuna vitu ambavyo anaviamini na amekuwa akiviamini vitu hivyo, kama hautakuwa na moyo wa kialimu kwake kila siku utakwaza naye na wakati mwingine utajikuta unamlazimisha kufanya vitu ambavyo yeye haviamini ila atajikuta anafanya tu kwa kuwa wewe umesema.
Usipomfundisha akajua mitazamo na shabaha zako itakuwa ni rahisi na yeye kuendelea na utawala wa mfumo wa maisha yake na akajikuta anawaambukiza mpaka watoto wako tabia yake. Na ndio maana unaweza kukuta wanao walikuwa wanaenda vizuri sana ila tu alipokuja mfanyakazi tabia zao zimeanza kubadilika, hii ni kwa sababu watoto wanapenda kuiga sana na wakati mwingi wanaathririwa na wale waliokaribu nao.
Usidhanie kuwa yupo pale kwa ajili ya kukusaidia kazi tu, kumbuka na upande wa pili kwa ataishi na wanao kwa ukaribu na kwa muda wote ambao wewe haupo, kama hajui wewe ni nani, unaamini nini, na unashabaha gani lazima atajikuta anaingiza tabia yake kwa watoto wako. Wekeza muda wa kutosha katika kumuelimisha na kumvumilia katika hatua zote za kujifunza, ipo siku tu atakuja kufuzu vizuri.

6.     Kuwa mlezi kwake.
Jambo jingine unaloweza kulifanya kwake ni kuamua kuishi naye kama mzazi mlezi kwake, ukifanya hivyo utamfanya ajione kuwa yupo nyumbani na atawachukulia wanao kama wadogo zake.

7.     Onyesha upendo.
Kitu pia ambacho kitamfanya mfanyakazi wako kuishi vizuri nawe na watoto wako ni namna vile utakavoweza kumuonyesha upendo utakaomfanya ajisikie vizuri kwa ajili yako.

Mipaka ya mfanya kazi wa ndani
Maelezo yangu yatakuwa yamepungua sana kama sitojikita kueleza mipaka ya mfanya kazi wa ndani, familia nyingi zimeingia kwenye majanga makubwa kwa ajili ya kukosa mipaka ndani ya familia, ebu tutzame baadhi ya mipaka ya msingi sana kuwekewa vipaumbele katika ngazi ya familia:-

1.     Mipaka katika shughuli za chumbani kwa mke na mume.
Naelewa kuna wengine hawatanielewa zaidi, ila kuna kesi nyingi sana zimeibuka nyakati za leo, unakuta mume analalamika kuwa mke wake kalala na kijana wa kazi au mke kulalamika kuwa mme wake kalala na msichana wa kazi.
Ni busara sana pamoja na hali ya kuwa marafiki kukawa na mipaka ya kuingia na kufanya shughuli za chumbani, shughuli za chumba cha wazazi ziwahusu wazazi wenyewe na si kumuongeza mfanyakazi wa ndani aanze kujishughulisha nazo. Kuna athari kubwa pia kama shughuli za mke zikafanywa na msichana wa kazi, inaweza kuibua dharau na wakati mwingine binti akaanza kujiona yupo sawa tu na bosi wake.
Sarah alipomruhusu Ibrahim azae na Hajiri, Hajiri akaanza kumdharau Sarah na kumuona sawa tu na yeye. Kuna mambo ni lazima muweke mipaka na usipoweka mipaka anaweza akaanza kuzoea zoea kwa ajabu. Si kila kazi unapaswa kumuachia mfanyakazi wa ndani eti kwa sababu unamlipa mshahara, kuna vitu vingine unajiharibia mwenyewe. Kwa mfano mke unataka chakula cha mmeo kiandaliwe na mfanyakazi, akipakue, amtengee na amnawishe huku nawe umekaa tu unasubiri nawe unawishwe kwa kuwa wewe bosi umeajiri. Hii tabia inapoteza taswira ya mumeo kwake na wakati mwingine umuhimu wako kwake unapungua na anagundua kuwa umuhimu wako ni kwenye masuala ya unyumba na tabia ukiikomaza kuna wakati ataona hata unyumba anaweza kuupata kwa msichana wa kazi na hapo ndipo ndoa uingia matatizoni.

2.     Mipaka katika vitu vya kuangalia na kuvifanya.
Unaweza ukapata binti au mvulana ambaye anapenda kuangalia au kufanya vitu vinavyoharibu tabia njema, wewe kama mzazi na kiongozi muwekee mipaka ili ajue kuwa si kila kitu anapaswa kuangalia na kukifanya, hii itamponya yeye na watoto wako ambao wanashinda pamoja nae.

SIMULIZI ZA KUKUJENGA KUHUSU WAFANYA KAZI WA NDANI

Nilivyonusurika kufungwa jera kifungo cha maisha

Nilipomaliza kidato cha sita nilikuwa na rafiki zangu ambao nilikuwa nikikutana nao kila siku jioni kwa ajili ya ibada ya pamoja, wakati ule katika ushirika huu tulikuwa tukimuona Mungu sana. Nilipenda kuwa karibu na watoto na hata kucheza nao kila nilipokuwa Napata nafasi ya kufanya hivyo. Kuna mtoto ambaye alikuwa akiishi jirani kabisa na eneo ambalo tulikuwa tukifanyia ibada zetu, nilipokuwa nikimuona nilipenda kumbeba na kucheza nae. Siku moja nilikuja kupata taarifa za ajabu sana kuwa nilikuwa nimemchezea Yule mtoto mdogo sana wa kike kwa kuchezea sehemu zake za siri kwa vidole. Maana mtoto alishikwa na homa kali sana na walipompeleka hospitalini kumpima wakagundua ugonjwa huo unatokana na kuchezewa sehemu zake za uzazi kwa vidole.

Yule mama alimuamini sana msichana wake wa kazi za ndani na alipomuuliza alikataa kabisa na akasema hajui na wala hausiki kabisa na uharibifu huo, majibu yale yalimpelekea Yule mama aamini kuwa ni mimi ndiye niliyemfanyia mtoto Yule mchezo ule mchafu na aliposhauriana na marafiki zake wakahafikiana kuwa ni lazima waende kufungua kesi ili nikafie jera. Mama Yule aliingiwa na chuki kubwa mno ya kunichukia, ashukuriwe Mungu wa mbinguni akamsukuma Yule mama aje kuzungumza na mama mwenzake ambaye ndiye mwenye nyumba katika lile eneo ambalo tulikuwa tukifanyia ibada, ilikuwa ni taarifa ngumu kuaminika na hata Yule mpewa taarifa aliogopa naye akaanza kupoteza imani nami kabisa. Ila walichopatana ni kuwa maadamu tatizo doctor amerimudu kwa tiba ni bora wanihurumie tu kuliko kuniangamiza kwa kunipeleka jera, waliazimia kwa pamoja kuwa kwa hali ya wazazi wangu kunipeleka jera wangenipoteza na wangepoteza hatima ya familia yangu pia maana katika familia nilionekana ni kijana pekee ambaye nimeanza kuchomoza mwanga wa mafanikio.

Nilipozipata habari hizi lilikuwa jambo gumu kuliamini na lilinitetemesha sana moyo wangu, na kunifanya kupoteza ujasiri mbele ya mama Yule aliyeathiriwa mtoto wake.

Bwana anifadhili katika janga hili
Wakati Fulani asubuhi katika kipindi cha fuku fuku hili BWANA alishuka na akanitia moyo kuwa nisiogope maana yeye amekwisha yamaliza yote na wala hakuna baya lolote litakalo nipata. Nikapata amani kuwa limeisha ila nilikuwa nikitamani sana siku Mungu afunue yote wazi ili ijulikane kuwa si mimi niliyefanya yale.
Ulipita muda kidogo Yule msichana wa kazi alikuwa akipenda sana uasherati, na kuna mambo ambayo alikuwa akiangalia ambayo yalikuwa yakimuinulia hisia ila alikosa sehemu ya kwenda kutuliza hisia zake, ikamlazimu kufanya mchezo wa kumchezea mtoto Yule ili kujiridhisha kihisia na alipenda kumfanyia mara kwa mara. Isingekuwa rahisi kabisa kwa mzazi kujua jambo lile kwa kuwa akirudi kazini yeye alichokuwa anauliza ni mtoto ameoga au amekula.

Isingekuwa rahisi kumkagua mwanae kwa kuwa vitu alivyokuwa anavitaka alikuta vimefanyika vyote kwa ustadi mkubwa. Ila daktari pekee aliona bora amchunguze mwili mzima ndipo alipokuta tatizo hilo.

Nguvu za Mungu za funua tatizo
Siku moja walikuta binti ameanza kupagawa na mapepo na yalimzidi katika kiwango cha kugeuka na kuwa kama chizi, walimpeleka sehemu mbalimbali kwa maombi, na alipokuja kufunguliwa tu binti alianza kutamka siri za ajabu na akazungumza kwa wazi kuwa yeye ndiye aliyekuwa anamchezea mtoto Yule. Hapa kweli BWANA alinitetea na kuwadhihirishia kuwa sikutenda yale. Na alizungumza kuwa hata wakati wa mchana huwa analeta wanaume mule ndani ili kufanya uzinzi nao.
Katika simulizi hii waweza kujifunza kuwa kuna umuhimu wa wazazi kuwa karibu na watoto wao zaidi ya vile wafanyakazi wa ndani walivyo karibu nao.

Mfanyakazi wa ndani wakala wa shetani.
Rafiki usomaye kitabu hiki, sijakusudia kuandika kitabu hiki ili nikutishe au nikufanye uwaone wafanyakazi wa ndani ni watu wabaya.
Nikiwa kwenye huduma mkoa Fulani katika nchi yangu Tanzania, nilipata simulizi kutoka kwa mwenyeji wangu ilinibidi nitafakari kwa kina sana. Kama ibilisi anakutafuta na kutafuta uzao wako jua kuwa anaweza kutuma hata wakala wake aje kuajiriwa kwako kama mfanyakazi wa ndani, na akija aweza tumika kama wakala wa kuharibu ndoa, kuharibu watoto wako, kuharibu uchumi wako na kila chema.
Rafiki yangu akanieleza kwa kuna mama aliyeokoka alichukua mfanyakazi wa ndani na alipomchukua alikuwa akimsaidia kufanya kila kitu kwa ufanisi na uharaka wa hali ya juu sana. Binti Yule alipenda sana kufanya kazi na kila alilokuwa akilifanya lilikuwa likiisha kwa uharaka na ufanisi mzuri, na binti Yule alipenda sana ibada, na alikuwa anawasisitiza wanafamilia wale wawe wanaomba kila siku kabla hawajaenda kulala.

Jambo lile lilifanya wanafamilia wampende sana na waone kuwa Mungu amewapendelea na kuwapatia mtumishi wake mzuri aje kuwafanyia kazi za ndani, na walipokuwa kanisani Yule msichana alipendelea kuimba pamoja na waongoza sifa. Loooh! Kumbe binti Yule hakuwa na chembe chembe za Uungu ndani yake hata kidogo bali alitumwa na adui kuja kuiangamiza ile familia na kuipoteza kabisa katika mstari wa ki-Mungu, na kiukweli japo walifanya ibada na kila kitu kilionekana kinaenda vizuri ila hali ya ulimwengu wa Roho ilikuwa ikiwabadilikia na kuna mambo walikuwa wakianza kuyashindwa taratibu.

Siku rafiki yangu anatembelea familia ile, Mungu alianza kumsemesha kuwa mtoto Yule ni wakala wa shetani na hata vyakula vyake ni mauchafu tu japo kinauzuri na ustadi, na wakati mtumishi yupo sebuleni mama mwenyeji kwa upendo akamtuma binti akaandae chakula jikoni ambapo hata moto ulikuwa haujawashwa, alipoenda ndani ya muda mfupi sana akawa amekoleza na kupiga chakula kizuri na kukiweka mezani, Yule mtumishi Mungu akazidi kumsisitiza kuwa si chakula cha kawaida kile, ilibidi iitishwe ibada ya familia muda huo.

Ilipoitishwa ibada mtumishi akamwambia aombe, kwa kawaida hakukuwa na mtu anayeomba vizuri na kunena kwa lugha kama Yule binti katika ile familia, alipoambiwa aombe akawaambia wote wafumbe macho ili aombe. Wote wakafunika isipokuwa Yule rafiki yangu, Yule binti akamsihi afunike macho ili aombe ila mtumishi akakataa akamwambia aombe hivyo hivyo, kwa kujilazimisha akaanza kuomba ila alishindwa kutamka maneno akawa anazungumza zungumza tu yasiyoeleweka na mwishoni akaanza kumpigia kelele mtumishi kuwa anamtesa amuache, hapo ndipo mapepo yaliporipuka na kuanza kujieleza yametumwa kuangamiza familia na familia yenyewe haikuwa na habari na hilo, ilifurahi kupata rafiki.

Simulizi hii itakufundisha kuwa katika uchaguzi wa wafanya kazi wa ndani ni busara ukamwomba Mungu sana ili apate kukupatia kijakazi wa kusudi lake kwako. Na pia familia isiyo na nguvu za Mungu ni kambi ya shetani.

Msichana mchawi nyumbani kwa mama yangu.
Mama yangu ni mkarimu sana haswa katika kukirimu wageni, tangu nakuwa nilikuwa nikiona wageni mbalimbali wakiletwa nyumbani kwetu na mama huwapokea na humshawishi baba pia kuwapokea na kukaa nao kwa kitambo.

Siku moja nikiwa nyumbani kimapumziko nikitokea Dar es Salaam ambapo nimekuwa nikifanya kazi zangu, wakati Fulani mama alinishirikisha kuwa kuna msichana amempokea na anahitaji kazi na msichana huyu alikuwa hatokei mbali na nyumbani na pale alipokuwa akiishi walimuondoa kwa kuwa waliogopa kuwa alikuwa mchawi na walilalamika kuwa toka aanze kuwa katika familia hiyo mambo yao yamekuwa yakiharibika, kwa tiketi ya wokovu wake mama akampokea na akaongea nae na mwisho akamsihi ampokee Yesu Kristo na Yule binti alikubali kuipokea sara ya toba, nafikiri ukiri wake ulitokana na hitaji lake la kupata mahali pa kujihifadhi. Niliporudi jioni mama alinieleza kwa furaha kuwa binti Yule ameokoka sasa na anatarajia kumtuma aende Dar es Salaam akawe mfanyakazi wa ndani kwa Dada yangu (mtoto wa mama mkubwa).

Nilijikuta nakosa amani na suala lile na ikanilazimu kumuita Yule dada nje nikae nae kumuhoji, nilimuhoji sana na nikagundua kuwa alikuwa akitumika kichawi tangu akiwa mdogo kwa kufundishwa na bibi na baba yake. Mwisho nikamuomba nimuombee ila alikataa akasema akipombewa huwa anachoka sana na mwili unakosa nguvu, nguvu ya Mungu ilipozidi kutanda katika lile eneo nikamwambia anyooshe mkono wake unishike alikataa kabisa, ilinibidi kumuinua na kumpeleka ndani ambapo nilipofika tu na kumshika alijikuta ameanguka na pepo zikianza kupiga kelele. Nikukumbushe kuwa kama hakuna nguvu za Mungu utaajiri hata wachawi na utaona shida yake katika utendaji kazi wao na ni lazima wafanye uharibifu.