Thamani yako(your values)+Uwezo
wako(your core strength)+Kiu yako(Your Passion)+ huduma yako(your service )=Kusudi
lako=Maisha yenye maana
1.
THAMANI YAKO INAVYOKUFANYA UISHI MAISHA YENYE MAANA
Tunapozaliwa tunakuwa na thamani sawa
.Kadri tunavyokua thamani yetu hupanda au kushuka .
Maisha yetu ni kama bidhaa ambayo huweza
kupandishwa thamani au kushushwa.
Binadamu ndo kiumbe pekee chenye uwezo
wa kujiongezea thamani au kujishusha thamani .
Ili maisha yako yawe ya thamani unapaswa
kujiona wewe kama bidhaa iliyoko sokoni tayari kwa kuuzwa.Bidhaa hufutwa vumbi
,huwekwa vizuri kwenye mifuko mizuri n.k ili uvutie wateja na iweze kununulika
kwa haraka sana .
Jiulize mahali ulipo thamani yako ikoje
,je kwenye familia yako usipokuwepo wanajisikiaje au ndo ile wanasema bora
kaondoka .
Mshahara unaolipwa pengine ni kwa sababu
hujajua thamani yako au umeridhika kwa sababu ukiondoka kampuni itafurahi
kuondoka kwako maana hakuna jipya unaloongeza .
Je mtaani kwako/shuleni kwako/chuoni
kwako watu wasipokuona wanajisikiaje ???
Thamani yako hupimwa katika baadhi ya
maeneo yafuatayo :
· Unavaa mavazi ya
aina gani??
· Unaongea vitu
gani ??
· Unaishi na watu
gani ??
· Una mawazo ya
aina gani?
· Una wasiliana
namna gani??
· Nidhamu binafsi
· Uwezo wa
kujisimamia mwenyewe
· Ufanyaji kazi
kwa bidii
Kama ilivyo thamani ya bidhaa kuongezeka
hata wewe unaweza kujiongezea thamani kwa kufanya yafuatayo kinyume chake
utakuwa ukishusha thamani yako kila sekunde .
· Ongeza
thamani kwa Kumuomba Mungu akupe Hekima kutoka kwake
· Ongeza
thamani yako kwa kusoma vitabu vizuri na kupata maarifa
· Ongeza
thamani yako kwa kukaa na watu wenye thamani kubwa juu yako na wanaojitambua
· Ongeza
thamani kwa kuangalia TV zinazongeza thamani katika maisha yako .Piga chini TV
na vipindi vibovu maana siyo lazima uone kila kinachopita machoni pako
· Jifunze
namna ya kuwasiliana
· Jifunze
kujisimamia n.k
FAIDA
YA KUWA NA THAMANI ENEO ULIPO
· Utapendwa na watu wengi utachukiwa na wachache maana
kuna watu kazi yao ni kuwachukia wengine
· Utakuwa jasiri kuwashauri na kuwafundisha wengine
· Hutanyanyaswa kazini kwako na sehemu yoyote
· Utaheshimika na watu haijalishi una kipato gani au
ukoje
· Uzao wako utaheshimika
HASARA
YA KUTOKUWA NA THAMANI ENEO ULIPO
· Utadharaulika
· Utaanza kujichukia mwenyewe
· Utaanza kunungunika na Kumkosea Mungu