Tarehe moja mwezi wa tano 2016, nilienda kijijini Bariadi.Tukiwa
kule kijijini mvua kubwa ilinyesha.Kumbe kile kijiji kipo katikati ya mito miwili
ambayo yote ilijaa siku hiyo.Hatukuwa na namna isipokuwa kulala kule
kule.Tulienda kulala kwa mzee mmoja ambaye alikuwa amejenga nyumba nzuri sana
kijijini pale.
Jioni kwenye saa
moja hivi alitutembeza kwenye eneo lake. Aisee! nilishangaa sana .Mzee alisema “Nilipoona nipo peke yangu huku porini
niliamua kuanzisha center (kijiwe).Nikanunua mashine ya kusaga unga, nikajenga na maduka
,na nikajenga godown la kuhifadhia
nafaka, na nikajenga na frame za maduka” Mzee alisema.
Mzee huyo ana ukubwa
wa eneo lipatalo mamia kadhaa ya ekari, ni kubwa sana.Watu walioona amawekeza
hivyo vitu na wengine wakaja wakaanza kununua maeneo yake na kujenga. Sasa hivi
ni kamekuwa kamji kakubwa watu ni wengi sana.Serikali imeshapeleka umeme katika
kijiji hicho na maeneo yake yote ameshayaandalia ramani za mipango miji huku
ametenga eneo kubwa la kuanzisha CHUO.Zaidi ya yote mzee huyu anafuga ng‘ombe
kwahiyo maziwa kwake si kitu.Kabla ya umeme alikuwa anatumia umeme wa
jua(solar).Kwa sasa mzee huyo amestaafu alikuwa MRATIBU WA ELIMU katika kata yake.
Kwanini nimewashirikisha
jambo hili la mzee?. Ni kwa sababu mimi nilijifunza jambo kubwa sana kwake.
Kwamba fursa zipo kila mahali mjini na vijijini.Kwa sasa mzee anasubiri tu watu
waje kununua viwanja maana tayari ameshavipima na kwa jinsi mahali pale palivyo
mzee wa watu atavuna pesa nyingi sana.Nilipojaribu kumdodosa aliwezaje kumiliki
eneo kubwa namna ile? Alisema yeye alikuwa ananunua kidogo kidogo na hatimaye
akawa na eneo kubwa vile. Kufikiri kwake huyo mzee huenda kuliwa tofauti sana
na watu wengi. Chukulia kwa mfano, mimi au wewe tungekuwa huyo mzee, Je, tusingekimbilia kujenga mjini na kupaacha kule
kijijini?.Kila mtu ajiulize hili swali kama ungekuwa wewe mzee yule ungejenga.
Tunapojifunza
kufanikiwa sio tu kutafuta fursa bali pia kubadili mfumo wetu wa kufikiri
kuhusu mjini na kijijini.Wengi wa wale wanaoitwa wasomi, akili zao haziwazi
fursa zilizopo kijijini bali zimejikita kuwaza fursa za mjini ambazo wakati
mwingine ni ghali kuzipata.Ukimwambia leo mtu akaishi Nguruka kule kigoma sijui
kama atakubali atajitetea sana, mara nyingi ataanza kusema si unajua kazi zangu ni za mjini?.
Siku moja
nilikuwa nasafiri kutoka Dar kwenda Lindi njiani niliona maeneo makubwa sana
lakini hayana watu.Nilipofika nikauliza wenyeji mbona njiani nimeona maeneo
makubwa hayana watu?Wakasema yaani huku watu ni wachache sana na kuna maeneo
mengine hayana wamiliki.Nilishangaa saana nikasema kweli Tanzania tuna
umasikini wa kulogwa .Mifumo tuliyonayo ya kufikiri imetuathiri kwa kiwango
kikubwa sana kiasi kwamba kila tunachikiwaza tunafikiria mjini ambako kuna
msongamano mkubwa.Mjini sio kubaya ni kuzuri sana ukiweka mambo yako sawa.
Lakini tumejisahau kufikiria fursa nyingi zilizopo vijijini.
Kwa mfano mimi nimefika
hapa Bariadi mjini sijuani na mtu hata mmoja. Nimekaa nikaona mambo hayaendi
lakini kwa kuwa nilikuwa nafahamu siri ya kuangalia fursa mjini na vijijini.Nilianza
ziara za vijiji kutafuta maeneo ya kulima bustani.Mahusiano mazuri na
wanakijiji yamenifanya nipate ekari 3 za kulima bustani bure.Nimeshalima ekari
moja matikiti maji, nyingine nimepanda papai na nyingine najiandaa kupanda
vitunguu.Yote hayo nimeyapata bure cha kushangaza kuna wafanyakazi wenzangu ofisini
wanajiita wasomi wao habari za vijijini haziwahusu.Sikilizia sasa mziki wake na
hivi Maghufuli kabana matumizi, kila siku ni kulalamika.
Ndugu,Umejipangaje
kufanikiwa ukiwa mjini na umejipangaje kufanikiwa ukiwa kijijini?Je, siku
ukilazimika kuishi kijijini ndo itakuwa mwisho wako wa mafanikio?.Watu wengi
nimewaona mara wakihamishwa vituo vyao vya kazi wakapelekwa kijijini ndani
ndani kabisa, maisha yao huwa taabu sana kwa sababu hawajajipanga kuona fursa
wakiwa kijijini.
Mungu anasema
hivi , na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya BWANA,
Mungu wako. Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.Kumbukumbu la torati
28:2-3. Ushauri wangu ni kwamba, hata kama unataka kuanzisha mradi wowote
fikiria pande zote uone wapi pana fursa pana na endelevu ikuwa ni mjini au
kijijini.Tusilemewe mawazo yetu upande mmoja tu.Ushauri wangu wa pili, jiandae
kuishi kila mahali iwe ni mjini au kijiji.Ushauri wangu wa tatu, tunapenda san
kuilaumu serikali eti kwa sababu huduma zote inazipeleka Dar.
Wakati
tunailaumu serikali tumesahau kwamba hata sisi huduma miradi mingi tunaiweka
eneo moja kwa nini tusisambaze miradi yetu?Humu kuna wageni wengi wengine
hawanifahamu kwa majina naitwa Mabula Jilala.
~Mabula Jilala