Maana
ya uwekezaji :
Uwekezaji ni kitendo cha
kuingiza fedha kwenye mradi fulani kwa ajili ya kujipatia faida ama ya muda
mfupi au muda mrefu
Hakuna mwekezaji
anayewekeza kwa ajili ya kupata hasara kama yupo itabidi tumpeleke Milembe
akipimwe akili
KWANINI UWEKEZE ????
· Ajira yako si salama ,unaweza kuipoteza muda wowote na maisha yakawa magumu sana.Kama ukiachishwa kazi leo
na hujawekeza kuna uwezekano ukawa na msongo mkubwa wa mawazo na mara nyingi
watu hufa mapema
·
Faida ya vizazi vyako
Unaweza usifaidi sana
uwekezaji wako kwa sasa lakini kizazi chako kikaishi maisha ya furaha kwa
sababu uliwekeza vizuri
Miaka ya hivi karibuni
kumekuwepo na kasi na ongezeko la watu wengi wanaotaka kuwekeza .Hata hivyo
watu wengi hupenda kuwekeza katika vitu ambavyo pay back period yake ni ndogo
yaani wanapenda kuwekeza na kupata faida haraka sana .Watu wamewekeza kwenye maduka
,supermarkets n,k ambavyo wana uhakika wa kupata hela kwa muda mrefu
Hata hivyo uwekezaji wenye
faida kubwa ni uwekezaji wa muda mrefu .katika uwekezaji huu mtu huweza
kusubiri kwa zaidi ya miaka mitano ili kuona matunda .Hata hivyo watu wengi kwa
sababu ya kutokuwa wavumilivu wanashindwa kufanya uwekezaji huu .
BAADHI
YA UWEKEZAJI WA MUDA MREFU NI KAMA UFUATAO :
- UWEKEZAJI KATIKA MUNGU
Kuwekeza katika Mungu
ndicho kitu cha msingi kabisa katika uwekezaji wa aina yoyote .Pasipo Mungu
hatuwezi chochote na tukiwa na Mungu tunayaweza mambo yote katika yeye atutiaye
Nguvu hivyo tunapaswa kuwekeza muda na pesa zetu kwa Mungu sambamba na vipawa
na karama tulizopewa .
- UWEKEZAJI KATIKA MAARIFA
Najua unaweza usinielewe
lakini ukweli ni kwamba huu ndio uwekezaji ambao utakulipa sana kama utaamua
kuwekeza kwayo.Wekeza sana katika maarifa kwa gharama yoyote maana bila maarifa
hata hiyo miradi unayowekeza itakushinda kuendesha maana utakuwa na maarifa
duni .
- UWEKEZAJI KATIKA WATU
Watu wengi hawajui kuwa
watu ni mali na watu ni fedha pia .Sikia bila watu hakuna fedha na fedha
huletwa na watu .Sasa kama fedha ziko kwa watu ,kwanini usiwekeze kwa watu .
Siri hii wanaijua watu
wachache sana wenye maarifa na wale wanaoijua ndio wanaofaidi matunda .
Uwekezaji kwa watu
unahitaji kujitoa sana kwa ajili ya wengine lakini in long run watu hao hao
watakulipa maradufu kama utajua namna ya kuwatumia na kubuni huduma zako ambazo
kama umewekeza kwao lazima wafuate huduma yako kokote ulipo .
- UWEKEZAJI KATIKA ARDHI NA MASHAMBA
Huu pia ni uwekezaji wa
muda mrefu ambao hulipa sana japo kwa muda mrefu .Yapo mashamba mikoani
yanapatikana kwa bei rahisi ni vizuri kuyakimbilia na kuanza kuwekeza katika
ardhi .Faida ya uwekezaji katika ardhi ni kuwa unaweza kuanza mradi kama kilimo
na ufugaji au kilimo cha miti na ukajipatia pesa .Shida watu hawataki kutoka
mjini kwenda mikoa ya nje ambayo ardhi hupatikana kwa bei rahisi na huko
unaweza kufanya mambo mengi kwa kutumia kiasi kidogo tofauti na mji wa dar es
salaam ambapo kwa sasa ardhi imekuwa gharama sana .
_Rafiki yangu Michael UHAHULA yeye baada ya kumaliza Chuo kikuu cha Dar
es saalam alipata wazo la kuwekeza kwao Njombe baada ya kuona kuna mashamba
mengi ambayo hayana kitu na yana rutuba nzuri _
_Wakati
huo akiwa amemaliza mwaka 2014 ,Michael hakuwa na fedha kama inavyokuwa pale
mtu anavyokuwa amaemaliza chuo lakini kwa kuwa alikuwa na wazo alihaha kutafuta
mtaji huku akiwa anawashirikisha watu wazo lake lakini wengi walimbeza_
_Michael
hatimaye alikutana na wazungu na mara baada ya kuwasimulia ardhi iliyoko mkoani
Njombe kuwa haina watu na ni nzuri kwa mambo mbalimbali ,wazungu hao
walimsaidia kiasi kikubwa cha fedha ambacho Michael alisajiri asasi yake
iitwayo Mafanikio Foundation na sasa akiwa ameajiri vijana 200 wanaofanya kazi
za mashamba_
_Asasi
hii ya ndugu Michael inajihusisha na kumuuzia shamba mtu yeyote ,na kumtafutia
hati miliki pamoja na kumpandia mtu huyo mnunuzi wa shamba miti ya mbao na
nguzo kwa bei ndogo sana na shamba hilo linasimamiwa mpaka uvunaji_
Hii
ni fursa kwako kama ulikuwa hujaisikia na tayari Michael anapata kiasi kikubwa
cha fedha kupitia wazo lake la uwekezaji kwenye Mashamba