KUMBE TATIZO UNALOTAKA KULITATUA NALO LIMEJIPANGA



Hebu kama wewe ulisoma shule ya msingi enzi zile za Nyerere, Mwinyi au Mkapa tujikumbushe hadithi hii ambayo ina funzo kubwa  sina uhakika wa enzi za Kikwete na sasa Maghufuli kama hadithi hii inasomwa .Hadithi hii ni ile ya *Nani atamfunga Paka Kengele???* .Twende wote hapa chini na ujifunze kitu .

"Kulikuwa na duka Kubwa la Vyakula na Vinywaji katika mji. Panya Wengi waliishi katika  duka hilo la vyakula na vinywaji. Chakula kilikuwa ni kingi sana kwa ajili yao. Walikula kila kitu na kuharibu mifuko yote ya vyakula. Waliharibu pia mikate, biskuti na matunda ya duka.

Mwenye duka alishikwa na wasiwasi kweli. Hivyo, yeye alipata wazo "mimi lazima ninunue paka na atakaa humu ndani ya hili duka. Kufanya hivo naweza kuokoa mambo yangu."

Alimnunua Paka mmoja mzuri, mkubwa na kisha kumwacha pale. Paka alikuwa na wakati mzuri wa kuwinda panya na kuwaua. Panya hawakuweza kuzunguka kwa uhuru sasa. Waliogopa kwamba wakati wowote paka ange wakamata na kuwala.

Panya walitaka kufanya kitu fulani. Wakaitisha mkutano na wote wakasema "Ni lazima kujikwamua na paka. Je, kuna mtu ana maoni?"

Panya wote wameketi na kuogopa. panya mmoja mwelevu alisimama na akasema, "paka hutembea kwa upole. Hilo ni tatizo. Kama tunaweza kumfunga kengele kwenye shingo yake, basi mambo yatakuwa mazuri. Tunaweza kujua harakati zake  zote ".

"Ndiyo, hilo ni jibu sahihi," walisema panya wote. panya wa miaka mingi alisimama polepole na akauliza, "Ni Nani atakaye Mfunga paka kengele? " Baada ya muda mchache hakukuwa na yeyote wa kujibu swali hili.:"

Angalia wakati huyu Mwenye duka akiwa na mawazo ya kutatua tatizo ili aendelee na biashara yake kumbe adui yake mkubwa naye amejipanga asikamilishe azima yake .



 *FUNZO*

_Wakati unapoingiwa na wazo la kufanya jambo fulani mazingira yanayokuzunguka huja na vipangamizi vya kutofanikisha mambo yako .Mazingira hayo yanaweza kuwa ni watu wasiotaka uendelee na kukurudisha nyuma .

Wakati unatafuta kukamilisha ndoto zako na malengo yako wapo watu watakaa kikao kwa pamoja na kukufanya usifanikishe ndoto yako .Watatafuta mbinu za kukufunga kengele .Kengele ni maneno utakayoambiwa kuhusu kile unachowaza kukifanya  na ukiyasikiliza utavunjika moyo sana na hutasonga mbele.

Wakati naendelea kuandika ghafla hapa nakumbuka hadithi ya Yusufu kwa wale Wakristo akitajwa kuwa  moja ya watu na ndoto kubwa za kufanikiwa lakini ndugu zake nao wakaa kikao kama walivyokaa panya ili Wamwangamize Yusufu .Nadhani Unakumbuka ilifika hatua akauzwa na hapa ni baada ya pona pona ya Kuchinjwa na ndugu zake wa Damu.Usingekuwa moyo dhabiti wa Yusufu asingeweza kufanikisha ndoto zake /

Daima siyo kitu rahisi kufanikisha kile unachowaza .Unapaswa kujua hata mazingira yamejipanga vizuri kabisa kuhakikisha kwamba hufanikishi kile ambacho umekipanga .Hivyo ili kukifikia lengo inahitaji ujenge uwezo mkubwa wa kuzalisha njia mbadala wa kulikabili Tatizo au Changamoto unayopitia_