HII NDIO SABABU YA TWIGA KUWA NA SHINGO NDEFU ~Joas Yunus 0753836463




Habari  Ndugu Msomaji wa makala hii!

Twiga ndiye mnyama aliye na shingo ndefu sana na mwenye uwezo wa kulisha kwenye majani marefu sana kuliko  wanyama wengine .Hii inamanisha kuwa twiga ana uwezo wa kulisha majani ayatakayo yawe ya juu au chini na hii humfanya ajihakikishie chakula chake hasa kipindi kigumu cha ukosefu wa chakula.

Hata hivyo twiga inasemekana hapo awali hakuwa na shingo ndefu (As far as organic evolution is concerned) lakini kilichomfanya awe na shingo ndefu ni namna twiga alivyokuwa akipenda kulisha majani yaliyoko juu sana na kadri shingo lilivyozidi kutumika kurisha majani ya juu ndo lilivyoongezeka .

Biolojia inasema katika organic evolution uliyosoma kuwa kadri kitu kinavyozidi kutumika huwa kinaongezeka na kama kitu hakitumiki huwa kinapotea .(Law of use and disuse).

Hii inatufundisha kuwa tunaweza kuamua kuwa vyovyote tunavyotaka kuwa kama tukitumia vile tulivyonavyo(you can be whoever you wanna be).Shida inayosababisha usiwe vile unavyotaka ni uvivu na kukata tamaa mapema.

Twiga anatufundisha kuwa watu wanaofanikiwa ni wale wanaotumia walivyonavyo huku wakizishinda changamoto ambazo zinazuia kuwa vile wanavyotaka kuwa.

Ukweli ni kwamba kama hutumii ulivyo navyo vitapotea au  kuwa butu kama kisu kisichotumika .
  • Kama hutumii kipaji ,kitapotea
  • Kama hutumii akili ulizopewa na Mungu Maisha yako hayatabadilika
  • Kama hutumii fursa utakuwa maskini