HUYU NDIYE MTOTO MMILIKI WA KAMPUNI MWENYE MIAKA 13.



Ni jambo linaloweza kushangaza hapa kwetu Tanzania lakini haya ndiyo maisha ambayo wenzetu wamefikia .Huku kwetu mtu akianzisha kampuni watu wanashangaa hata kama ana miaka 60 lakini huko kwa wenzetu watoto wadogo wanaanzisha makampuni na ni jambo la kawaida na hapa ndipo nakubaliana na msemo wa Bishop John Shusho kuwa Dunia inakimbia lakini watanzania tunatambaa.

Juzi Rafiki yangu Lazaro Samweli alituma picha ya mtoto ambaye alisema anamiliki kampuni akiwa na umri mdogo sana .Nilivyoona hivyo ilinilazimu kufuatilia historia ya huyo mtoto maana napenda kufuatilia vitu na kupata taarifa za uhakika .Leo nakujulisha  na wewe uweze kumfahamu msichana huyu mdogo ambaye alizaliwa kama wewe lakini yeye akiwa ni mtu wa kudhubutu kuliko wewe .Mtu  mmoja akasema umri ni namba tu na haufanyi chochote kwenye maisha kumbe hakuna muda wa kusubiri ndivyo alivyogundua msichana huyu anayefahamika kwa jina la "ASIA NEWSON"

Asia Newson ni msichana  mwenye umri wa miaka 13 kule marekani ambaye alianzisha Kampuni yake iitwayo Super Business Girl (http://www.superbusinessgirl.com) akiwa ana miaka mitano (5).Kampuni yake inahusika na utengenezaji wa mishumaa  na huwa unawafundisha watoto namna ya kuwa wajasiriamali maana ndoto yake ni kuona watoto wanakuwa wajasiriamali .

Alianza kujifunza kutengeneza mishumaa kutoka kwa baba yake na baadae akaanzisha kampuni kutokana na ujuzi aliopata kutoka kwa baba yake .Uwezo wake wa kujieleza unadhihirisha kuwa ni mtoto aliyeandaliwa na yeye akakubali kuandaliwa .

Asia amefanikiwa kushinda tuzo nyingi na kushiriki mashindano mengi duniani ikiwemo shindano la American Got Talent .Asia ana malengo ya kusoma sheria katika chuo kikuu cha Havard na mwisho anataka kuja Rais wa Marekani ili kutimiza ndoto yake .

Asia atoe funzo kwetu kuwaandaa watoto wetu kuwa waajiri hasa katika miaka hii ambayo ajira imekuwa changamoto .Ndiyo inawezekana kuwa na watoto kama Asia Newson kama familia zitawajengea uwezo watoto wao na kuwaonesha uwezekano wa kufanikiwa kama watatumia uwezo wa ndani walio nao .

Kwangu mimi Asia amenipa nguvu mpya ya kukaza uzi na kuamini kuwa hakuna lisilowezekana kama mtu akiamua .Kumbe unaweza kuwa yeyote na ukapata chochote unachokipata kama utaamua .

Wazazi ni changamoto kwenu kujiuliza nini utamrithisha mtoto wako ambacho kitamsaidia maisha yake yote .


Joas 0656110906

*Kumbuka kujisajiri kwenye semina ya mtandaoni  kwa ada ya sh 5,000/= tu.Tuma kwa Tigopesa 0656110906 na 0753836463*