YAFAHAMU MAENEO YA KUFANYA UWEKEZAJI ~ Joas Yunus



Katika vitu ambavyo humtofautisha tajiri na maskini ni namna wanavyofanya uwekezaji .Mfano Maskini hununua ardhi na kuiacha miaka kumi bila kuiendeleza huku tajiri akinunua ardhi hufanya mwendelezo wa ardhi hiyo kwa kujenga kiwanda,kulima n.k.

Watu wengi wanapenda kuwekeza lakini hawana ujuzi wa wapi wanapaswa kuwekeza na mwisho wa siku maisha yameendelea kuwa kama yalivyo kwa muda mrefu .

Sababu kubwa ya watu kuwekeza na kubaki kuwa kama walivyo ni kuwa hawakufuata kanuni za uwekezaji .Yafuatayo ni maeneo muhimu ya kufanya uwekezaji wenye tija kwa faida ya vizazi vyako .

        1. *Uwekezaji katika Maarifa* :

Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa Maarifa~Biblia

 Eneo hili la maarifa ndio  msingi mkubwa wa mwekezaji awaye yeyote .Ni kama vile mjenzi wa nyumba asivyoweza kujenga nyumba yeyote bila msingi .Ni muhimu sana kuyatafauta maarifa kwa gharama yoyote maana maarifa ndiyo funguo ya vitu vyote hapa Duniani .Bila maarifa utanunua eneo kubwa na hutaweza kuliendeleza ,bila maarifa hutapata mawazo ya nini ufanye kama biashara yako haiendi .Bila maarifa utabaki ukiamini kuwa kuna watu wana bahati na wewe huna bahati

Tajiri huchukua miaka mingi sana akitafuta maarifa ya kile anachodhani anaweza kufanya wakati maskini hana muda wa kutafuta maarifa na ndiyo maana mambo yake hayaendi .Unapaswa kusoma vitabu sana ,unapaswa kuhudhuria semina mbalimbali ,unapaswa kusikiliza vit vya kukuongezea maarifa .

Shida na hii kwamba usipoyatafuta maarifa kuna vitu vingi hutaweza kuvifanya .Kwa mfano una wazo la kuanzisha biashara ya mtandaoni (online business) wakati huo hutafuti maarifa ya kuijua vizuri biashara hiyo ujue huwezi kufika unakotaka kufika .

2.*Uwekezaji katika Muda*: Vijana wengi sasa wanatamani maisha yaende haraka haraka sana .Wanatamani mafanikio haraka sana huku wakisahau kuwa hata kuzaliwa kwa binadamu ni mchakato wa muda mrefu .

Ukitaka kuwa na mafanikio makubwa lazima UJUE kuwa kuna vitu haviwezi kuleta matokeo haraka kama unavyoweza kufikiri ,vinahitaji subira ili vianze kutoa matokeo .Ndiyo maana imekuchukua miaka 17 Na zaidi mpaka unaitwa mtu mwenye shahada ya kwanza .

Ni muhimu sana kujua kuwa muda ni mali na hivyo kadri unavyowekeza kwenye muda ndivyo unavyopata matokeo makubwa .

3. *Uwekezaji katika watu*: Hii ni sehemu ya uwekezaji ambayo watu wengi wamejisahau na mwisho wa siku wameshindwa kufanikiwa .
Watu pekee ndio wanaoweza kukufanya ufanikiwe kwa haraka zaidi .Tengeneza mtandao wa watu wenye tija na fikra chanya ambao kila iitwapo leo watakufanya kuiona ndoto yako kuwa  inawezekana .

Kuwekeza katika watu pengine utatumia muda na vitu vingine lakini wewe usijali ,jua kuwa huo ni uwekezaji unaodumu miaka na miaka .Tumia muda kuwasaidia watu na kutengeneza mtandao wa watu .

Matajiri wengi Duniani walijua nguvu iliyoko kwenye mtandao wa watu(Power of Network) na kupitia mtandao walipata mafanikio waliyoyataka .