NI KWANINI BAADHI YA FURSA HAZIDUMU??YAANI HAZIWI ZA MUDA MREFU??


Mfano;kuna kipindi inaibuka vijana wengi sana  walisomea hotel management.yaani kila kona wanasoma hiyo course.ikafika mahali ikaisha.Ikatokea wengi sana wakasomea public relations.nayo ikapita.Ikatokea hapa juzi wakaibuka matabibu wengi sana wa tiba mbadala.kila kituo cha tv ukifungua ni tiba mbadala.nayo imepoa.Ikaja ufugaji wa kware.wengi sana walifuga.sasa imepoa.Kwenye biashara nako hivyo hivyo.utakuta huyu kafungua saloon.basi mtaa mzima ni saloon.

Nimetoa mifano michache.Je??unafikiri nini sababu ya fursa kuibuka na kupotea??

 1. Kutokumtegemea Mungu na kufikiria peke yako unaweza.

2. Kutokuwa na imani kuwa utaishi.yaani kuna mpaka watumishi ukienda msibani utasikia wakisema ,sisi ni marehemu watarajiwa.sasa marehemu mtarajiwa anaweza kuwa na miradi endelevu??wenzetu wana mipango binafsi hadi ya miaka tisini na tano.wewe mpango wako mrefu umeweka miaka mingapi???kama sio miwili

3.Uvivu wa kufikiri.yaani mtu anaanzisha mradi au biashara.hakai kusoma,au kupeleleza au kutafuta taarifa nyingi kuhusu anachokifanya.anafungua biashara,anafanya usafi anakaa nje ya duka au ofisini bila hata kufanya vhochote kuongeza ujuzi.kwa hiyo miaka nenda rudi unakuwa huna jipya.mwishowe biashara inakufa.

4. Kutokuheshimu mitaji.Mtu unachuka mkopo kuanzisha biashara .na hutengi faida na mtaji.kwa hiyo unakula zote😃😃mwisho wa siku unabaki unarejesha tu huongezi bidhaa
5 Kukosa maarifa.(sio kukosa elimu) Elimu unayo lakini huna maarifa ya unachokifanya.kwa hiyo unakuwa unafanya alimradi.

6.Unakuwa huna mipango inayosubiri hela.kwa hiyo ukipata pesa ghafla,unafungua biashara au mradi ghafla unauendesha ghafla ,nao unakufa ghafla.huna mipango endelevu

7.Kuiga kitu cha mtu ambacho hujui alivyoanza na njia anayoipita.

8.Kupata taarifa potofu.Kuna watu huwa hawasemi kweli kuhusu miradi au biashara zao.mtu anakudanganya alianza na mtaji wa laki tano kumbe milioni tano.wewe unaingia kichwa kichwa.Au mtu anastawi magari manyumba anakuambia ni kazi hihii ya kufuga kuku.kumbe ana yake.

9.Hatuna maono kutoka ndani yetu.hatujui tunachotaka.tunabaki kusema nataka niwe kama diamond.

10.mfumo wa elimu ya nchi yetu.fikiria tanzania nzima shule za serikali na binafsi wanasoma vitu vinavyo fanana kwa asilimia kubwa.kwa hiyo kuna kuwa hakuna upenyo wa kuwaza tofauti.na mwanafunzi ukiwa sio msomaji binafsi umekwenda na maji.

11.kutokuwa na mpango wa kupata kipato endelevu.yaani kutaka hela kuendana na matumizi yaliyopo.Mtu unataka uajiriwe ili upate hela ya kuoa.Hakuna mpango wa kuwa na fedha ya kutosha.Kwa hiyo unaibukia tu fursa yoyote.(hand to mouth income))

12.Kuwazoea wateja na kukosa nidhamu ya kazi yako
Wengi wameibukia hizi fursa na hata wengine kuchukua mikopo matokeo yake wamejikuta wanazalisha kitu kilekile na kutegemea wateja wale wale.mwisho wa siku wakajikuta hawawezi kuendelea.Ninashauri tufanye yafuatayo ili tudumu ktk ujasiriamali au ktk biashara kwa muda mrefu na kutawala soko.

1.Kabla ya kufanya chochote,pata muda wa kumuuliza Mungu.zaburi;32:8

2.Pata muda wa kutosha kujisoma,kujichunguza na kujijua.jua uwezo wako na nguvu yako ilipo.fahamu UPEKEE wako.jitofautishe,tafuta habari,safiri n.k

3.Toka nje ya wewe.kile unachokiona ndani yako ,kitoe nje halafu kisimamie.huo ndio upekee wake.tuonyeshe uwezo wako .Fanya kama vile uko peke yako duniani.na kumbuka huna kopy,hakuna anaefanana na wewe.kwa hiyo hata siku moja usitafute kufanya kitu kinachofanana na wengine.

4.ISHI ukijua kuwa dunia inahitaji ulicho nacho ambacho hatukijui bado.Hakuna mtu aliyeujua umeme mpaka yule aliyeuvumbua alipouvumbua.angekaa kimya ingekuwa hasara kubwa.Na mwingine akaja akagundua umeme wa upepo bila kujali wa maji upo.Na mwingine kagundua umeme wa betri bila kujali.Sasa wewe mbona hutaki kutoa hicho kipaji chako????badala yake unataka kufanya ambavyo tayari vimefanyika.TUPE NEW BRAND,KUFANYIA EDITING VYA WENGINE IMETOSHA.

5.Weka mipango yenye muda maalumu.fursa za msimu pia ufanye,lakini usizitegemee.weka mipango ya kukaa sokoni pengine miaka hata 50 .Na kama hukusomea na unakipenda na unakiweza,ok.tafuta taarifa sahihi then go for it!!!kweli kabisa ukibobea ni raha hata ugonjwa fulani unaweza kuuchambua adi msikilizaji atasema una phd ya udaktari

Hivi unajua kuna watu hata bidhaa zikipanda bei huwa hawajui.??yaani hawafeeel the pinch.kwa nini???kwa sababu wana kipato cha kudumu na cha kutosha.Lakini ngoja soda ipande bei.wanalalamika mpa ulimi unatoka.anatamani apimiwe hapo ya mia.🙈

Tunataka vitu vya tofauti.Tanzania inakutegemea wewe kijana uje na mawazo ya tofauti ili tusonge mbele.Mungu alikusudia tuwe tofauti ndio maana katuba tofauti jamani.cha ajabu badala ya kuvaa kama wewe,kuongea kama wewe,kubuni kitu chako,kufanya biashara ya kwako,umebakia kuiga tu.kila mtu anataka kuvaa kama p square.

Kila mtu anataka kusuka kama rihhana.
Obama ameibuka na yes we can.
Basi kila mtu utamsikia yes we can.
Ukimuuliza we can nini,anangaa mimacho.

 BE YOU.REMAIN YOU!!!Hebu usiku wa leo jichunguze upya maana kuna vitu Mungu amekuwekea bado hujavitoa ulimwenguni.Anza sasa kutuambia wewe ni nani na una nini.