Moja ya vitu ambavyo watu wanapata shida ni Kubadilika.Kwa
Mfano jana Kijana Jithamini niliwaambia kuwa Sasa tunapaswa kuhama kutoka
watsap kwenda Telegram Lakini utashangaa Hawahami . unaweza kujiunga nasi
kupitia link hii( http://ow.ly/W02z302FGkv) ambapo Inabeba watu 5000. Hii ni kuweza kuwafikia watu wengi ili
waweza kupata maarifa.
Mtu Mmoja alisema kama
Huwezi kubadilika hakuna kitu kitakachobadilika na Daima mabadiliko
hayakwepeki.Ili ufanikiwe lazima
ukubali kubadilika kutoka kwenye mtazamo hasi kwenda mtazamo chanya.
Wakati mwingine inakuwa
ngumu kubadilika Hata kama Unapenda kubadilika. Mabadiliko hayaji ghafla Ni
mchakato. Anza Kubadilisha Kile ambacho ni rahisi kubadilika huku ukifanya
jitihada za Kubadili mambo mengine.
Kimsingi usipokubali
kubadilika hakuna kitu kitakachobadilika Lakini mara tu utakapoamua kubadilika
kila kitu kwenye maisha yako kitabadilika(if You change everything around You Will Change but if You dont nothing Will change ).
Kubadilika Huwa ni
gharama na ndio maana wengi wameshindwa kubadilika .Nakumbuka haikuwa rahisi
kwangu kubadilika na kuanza Kusoma vitabu na kuachana na baadhi ya vitu
vilivyokuwa havina maana kwangu. Lakini ilifika Mahali nikasema Nahitaji kubadilika.
Ndugu, mabadiliko Ni yako binafsi. Usisubiri Yule abadilike
ndo wewe ubadilike. Kama Unatumia muda ovyo amua kubadilika, fanya mazoezi ya
kubadilika. Kama una marafiki wasiokupeleka kokote, amua kubadilika.
JYB- 0753836463