HAPA NDIPO MAHALI TAJIRI NA MASKINI HUKUTANA




Huwa kila siku nakutana na vijana wengi wanajiuliza maswali haya :
  •   Hivi mimi nitaweza kukutana na Mengi?
  •   Hivi mimi nitaweza kukutana na Manji?
  •   Hivi mimi nitaweza kukutana na Bhaharesa??


Ukweli ni kwamba kuna mwanya(gap) kubwa kati ya tajiri na maskini na hapo ndipo kunatokea ugumu wa maskini kukutana na tajiri na mwisho watu huishia kuwaona kwenye runinga na kamwe hawewezi kuonana na matajiri uso kwa uso na kujadili mambo .

Rafiki yangu Kashindi Edson mhitimu wa Chuo kikuu cha Dar es salaam kwa mwaka huu sehemu ya DUCE jana nilikuwa naongea nae akasema kuwa daima mstari unaomtenganisha Tajiri na maskini ni mwembamba  sana japo imekuwa vigumu kwa tajiri na maskini kukutana .Nilivyomuuliza ni wapi sasa maskini na tajiri watakutana na kwa namna ipi alishindwa kunijibu .

Badae nilipata majibu yangu binafsi na nikayaamini .Sehemu pekee ambapo tajiri na maskini wanapaswa kukutana ni kwenye "wazo".Kama una uwezo wa kuzalisha wazo lenye tija hakuna sehemu ambapo huwezo kufika .Wazo ni ufunguo utakaofungua milango mingi na kukutanisha na mtu yeyote unayemtaka.Kama huwezi kuzalisha wazo kila siku utakutana na watu wale wale na hutakutana na watu muhimu wanaoweza kukusaidia.


Kupitia wazo la Adam Ngamange na mtandao wake wa kijani kibichi ,Adam amekutana na watu mbalimbali ,mawaziri mbali mbali na imemfungulia fursa mbalimbali .Ni wazo pekee litakalokutoa mahali ulipo kwenda mahali pengine bila hivyo utabaki kuwa wewe na hakun mtu atakayekutoa.