SABABU 12 KWANINI HUNA FURAHA KATIKA MAISHA YAKO ~ Kashindi Edson






Tafiti zinaonesha kuwa, Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo raia wake hawana “Furaha” kwa kiasi cha hali ya juu. Mwanzoni sikuwa nikiamini hizi tafiti hasa baada ya kugundua zimefanywa na watu ambao siyo kutoka Tanzania.

Hata hivyo, kwa zaidi ya mwaka mmoja nimekwa nikifanya uchunguzi wa ukweli wa hizi taarifa. Ni kweli, “Watanzania wengi hawana furaha”. Unaweza ukapanda daladala kutoka Mbagala mpaka Makumbusho bila kumuona abiria hata mmoja akicheka. Hata ukiangalia nyuso zao hazina tabasamu. Pia unawaza ukaingia kwenye mgahawa ukakuta kuna watu 6, kati ya hao sita,  mmoja au wawili ndo wenye furaha, ndo wenye nyuso zilizo na tabasamu. Wengine wanne waliobaki hawako tayari hata kuongeleshwa(wamenuna). Nimewahi kuishi kwenye mtaa Fulani, si rahisi kuwakuta pamoja wakiongea vizuri na kufurahi pamoja, kila mtu ana mambo yake, muda wote wamekunjiana sura. Ingia hata kwenye Ofisi kubwa, Ofisi ambazo watu wana pokea mishahara mikubwa na vyeo vikubwa, utashaangaa watu wana misongo ya mawazo mpaka basi(Extreme Stress).

 Wengine hata kuongeleshana hawaongeleshani. Nenda barabarani, utakutana na watu wakiwa kwa makundi au mmojammoja, utashangaa watu ni wawili au watu wakionesha kwenda sehemu moja kwa pamoja lakini hata hawaongei, wala hawafurahii safari yao, wamekaziana sura kama wanaenda vitani. Hata mtu mmoja, yuko anatembea ukimuangalia kama kaibeba dunia kichwani kwake, ukimsalimia utafikiri alikuwa usingizini, sura kavu utafikiri siku ya tatu hajacheka.
Kulingana na tafiti na uchunguzi wa muda mrefu, kuna mamba na vyanzo ambavyo humpelekea mtu kukosa furaha katika maisha yake ya kila siku. Kama huna furaha, unawaona watu hawana furaha, sababu kuu 12 zifuatazo ndizo hupelekea binadamu kuishi bila furaha.

1.Kuogopa vitu ambavyo havijatokea.
Unaishi na mawazo ya kwamba jambo fulani halita fanikiwa, umejuaje?, Unawaza kwamba nikisalitiwa na mpenzi wangu sijui itakuwaje, je asipokusaliti?, unawaza kwamba itakuwaje nikifukuzwa kazi?, unajuaje kama utafukuzwa?, Tajiri anawaza vipi siku akifirisika, hata usingizi hapati, kwani maskini waa sio binadamu, Kila tukio katika maisha lina wakati wake na maumivu yake. Acha kuumia kwa tukio ambalo halijatokea. Unajinyima raha tu mwenye. Acha wasi wasi.

2.Kuhifadhi vinyongo moyoni. 
Kuishi huku ukimchukia mtu fulani ni sawa na kunywa sumu huku ukidhani atakufa mtu mwingine. Tuache vinyongo na watu kwani hatutakuwa na amani mioyoni mwetu, tutaishi bila furaha. Mtu akigombana na rafiki yake jana, leo kamchukia hata amabaye hakuwepo kwenye ugomvi wao. Hapo huwezi kuwa na furaha kwa sababu tayari huna wa kumfurahia.

3.Kutokujiamini
Jiamini unaweza kuwa Doctor, Unaweza ukawa kiongozi kama JK Nyerere, Pombe Maguful, Obama, Zitto Kabwe, unaweza ukawa Mfanya biashara mkubwa kama Eric Shigongo, Bahresa, Ruge Mtahaba, Unaweza ukawa Mchungaj au Shehe, unaweza ukawa Mwanamuziki kama Ben Pol, Rose Mhando, Farid Kubanda, Jay Z, Unaweza ukawa mwanamichezo kama Lionel Mess, Christiano Ronaldo, Fransis Cheka, Flola Mbasha, Unaweza ukawa Professor, Unaweza ukawa Mwandishi. “Maisha haya, unaweza ukawa yeyote yule unayetaka kuwa katika hii dunia”. Acha kukosa amani, amani acha kukosa furaha, jiamini, chukua majukumu, pambana.

4.Marafiki. Ukiwa karibu ya watu 5 wezi, wewe utakuwa mwizi wa 6, ukiwa karibu ya watu 5 matajiri we ni tajiri wa 6, ukiwa karibu ya watu 5 wapuuzi, we ni mpuuzi wa 6, ukiwa karibu ya watu 5 wanye furaha wewe utakuwa mtu wa 6 kuwa na furaha. “Ukiwa karibu ya watu 5 wasio na fuaha, 
jiandae kuwa mtu wa 6………………. Angalia watu unaokanao kwa muda mrefu kwa sababu wewe ni matokeo ya wale watu wanaokuzunguka. Jaribu kuwa karibu na watu walio na furaha, ufurahie maisha yako. Tafuta hata watu walio katika misingi ya dini. Muishi hata kwa kufarijiana.

5.Msongo wa mawazo. Kuna watu wanajifanya wanajua kuwaza sana. Yeye ana waza na kuwazua. Swala sio kuwaza, je unawaza nini? Walishakuwepo watu wanaowaza kukushinda hata wewe, Yesu, Mohhamed, Soctrates, Plato, Aristotle, Mahatma Gandhi, Confusius na wengine usio wajua. We leo unawaza nini?, Unawaza wazo moja, kabla hujalimaliza ushawaza lingine mwishowe unajikuta mawazo yanadandiana na kurundikana kichwani mpaka unapungua kilo. Tulia, pumua, fikiria kitu, kitendee kazi, kimalize. Sio unawaza bila kufikiria. Fikiria namna ya kuwaza tofatuiti na hapo ni “stress” na kujikosesha furaha bure.Ubomgo wa mwanadamu unawa uwezo wa kufanyia kazi wazo moja kwa wakati mmoja zaidi ya hapo unajidanganya. Hakuna sababu ya kurundika vingi kichwani
.
6.Mihemko hasi. Hii ni mihemo dhaifu kama vile, chuki, wivu, umbeya, roho mbaya, hasira. Ukiwa na mihemko hii dhaifu siku zote utakuwa tofauti na wale walio na mihemko imara kama vile upendo, uwazi, ushirikiano, umoja. Walio na mihemko dhaifu ndo hao ambao hawana furha hata kidogo. Dakika moja kakuchekea au kakusema vizuri, kesho kakununia na kukusema vibaya. “Mihemko hasi, ni adui wa furaha katika maisha ya mwanadamu”.

7.Mahusiano. Utakutana na tajiri au mtu tu mwenye pesa zake, elimu nzuri, kazi nzuri lakini cha kushangaza hana tabasamu wala bashasha maisha yake yote. Kumbe haelewani na mke/mme wake, boss wake haelewani nae, mahusiano na majirani sio mazuri, serikali nayo pia ina wasiwasi nae, kwa harakahaka huyu mtu hawezi kuwa na furaha. Tujitahidi kujenga mahusiano mazuri na jamii zetu ili tukae kwa amani na furaha.

8.Kutokujua furaha ni nini. Leo hii mtu ukimuuliza furaha ni nini, majibu atakayokupa lazima utacheka na pia “utafurahi sana”. Watu hawajui furaha nini, furaha sio amani ya nafsi, furaha sio kupata kile unachohitaji, furaha sio kupata mke/mme mzuri, furaha sio amani tu ya rohoni, hapana, “Furaha ni kukubali na kuridhika nafsini, rohoni, akillini na mwilini ”. Furaha nini swala la wewe kuamua kufurahi au kuto kufurahi. Kuna watu hawana pesa ila bado wana furaha, kuna yatima wenye furaha kuwashinda watu wenye baba na mama mpaka bibi na babu. Furaha ni kuridhika. Furaha ni kutosheka. Furaha haipo kwa Tajiri wala maskini, furaha anayo kila mtu, Furaha ni picha ya akilini, furaha ipo akilini mwetu na sio sehemu yoyote. Ukiamua kuwa na furaha au usiwe na furaha ni wewe tu. Furaha ni maamuzi. “Ukitaka kuwa na furaha kuwa, kama hutaki acha, chukia”

9.Fikra Potofu. Kuna watu wanaokunywa pombe, wanaotumia shisha, sigara, ngono, wakidhani wanapata furaha, kule ni kujiua sio kujifurahisha. Ni sawa ni kipofu anaevuka barabara. Kuna watu wanaodhani kuwa, kuwa na pesa ndo kuwa na furaha sio kweli, kuna watu wanaodhani kuwa maskini hana furaha sio kweli, furaha haina uhusiano wowote na pombe, pesa, sigara, nk. Mtu anakunywa pombe akishalewa anawatukana watu, hiyo ni furaha au karaha. Tuache dhana potofu za kwamba tukijihisi hatuna furaha, eti tukimbilie bar,

10.Kukata Tamaa. Kuna watu walisha poteza kila kitu kuhusu matumani ya kufanikiwa. Ukiwa huna matumaini ni sawa na maiti inayoishi kwenye mwili wa kuazima. Rudisha matumaini, amini kuwa kila kitu kinawezekana ukijituma, na kupamba na kujifunza. Hakuna njia ya makto katika mafanikio. Amka, endelea kupigania ndoto zako. “Mara tu uanapo kata tamaa, ndo hapo hapo unapopoteza kila kitu”. Ukikata tamaa tayari unaanza kuwazia waliofanikiwa katika jambo fulani na kujizika kwenye tabia haribifu kama vile wizi, uhuni, ujambazi, na mwishowe kukosa amani na furaha ya maisha yako.

11.Ubinafsi. Kuna watu kila jambo, kila shida, kila tatizo ni la kwao peke yao. Hatu swemi kwamba ukanadi shida na matatizo yako, ila jitahidi kutafuta ushauri, kuongea na wenzio hasa wale unaowaamini kuwa ni sahihi kwako. Acha kukumbatia shida zako. Tafuta tiba ya shida zako, “Kuficha shida na matatizo yako ni sawa na kujivalisha sanda wewe mwenye ukiwa bado hai”. Pia wanasema kuwa, “Mficha maradhi kifo humuumbua”. Kuna watu wanashida nyingi zinazotatulika lakini wamezikumbatia. Kwa upande mwingine kila kinacho kukuta wewe hata wenzio kilisha wakuta. Kama kufiwa watu walishafiwa sana, kama kuugua watu walishaugua, kama kutukanwa au kudharauliwa watu walishadhadharauliwa sana. Jua hicho kinachokukuta wewe muda huu pia na wenzio kilisha wakuta tangu zama hizo. Kuwa na amani

12.Kuishi kwa yaliyopita. “Sahau yaliyopita, samehe yaliyopita, chukua hatua, shika majukumu songa mbele”. Kujuta hakusaidii, acha kuishi na matukio mabaya ya nyuma kichwani mwako. Kama kama kuna kitu ulisha kosea, hata kama ni kwa uzembe wako mwenyewe jisamehe songa mbele, ukisha jisamehe wewe wasamee na walio kukosea ili ufungue mifereji ya amani na furaha katika maisha.
Mbali na hayo, Kutokujua sababu ya maisha, kukosa imani ya rohoni, tama za kupitiliza, kushinwa mambo mengi maishani, magonjwa, uvivu & uzembe, kutokujifunza pia vinaweza kukufanya ukaishi bila “furaha”.
“Furaha ni Afya Ya Mwili, Akili, Nafsi & Mwili. Sababu kuu ya kuishi hapa duniani ni “kufurahi””

                          Linda Furaha Yako, Furahia Maisha Yako