Kwa dereva anayezingatia na
kuheshimu taaluma yake,vilevile ambaye hataki kutoutendea haki haki muda
alioupoteza alipokuwa kwenye mafunzo yake ya udereva ni lazima afunge mkanda wa
usalama anapoingia ndani ya gari kwa ajili ya safari.
Nenda kwenye interview yoyote ya
makampuni ya usafirisha wa abiria au mizigo nenda na vyeti vyako pamoja na leseni yako ya
daraja la ngapi huko,lakini ukithubutu kuwasha gari na kutia gia kabla
hujafunga mkanda itakuwa imekula kwako,si kama hujui kuendesha gari hapana
unajua ila kosa lako hufuati kanuni.
Unaweza ukawa dereva mzuri lakini
usijue kulitumia vyema gari,hebu fikiria maisha ni yako lakini umewekea traffic
police wa kukusaidia kutumia gari lako kwa kufuata kanuni hali kadhalika utumie
barabara vizuri.
Unapoingia kwenye mahusiano ya
uchumba kanuni ya mkanda wa usalama ni muhimu,ili usilipe faini mbeleni kubali
kufunga mkanda,kwani utakapofunga mkanda hautakuwa na uhuru wa kufanya kila
kitu kama ilivyo dereva akifunga mkanda si rahisi kuinama na kuokota kitu chini
ya uvungu wa kiti.
Vijana wengi tunaingia kwenye
mahusiano na kuipuuzia kanuni hii matokeo yake tunapigwa mkono na askari,ndinga
tunapaki pembeni then tunalipa faini.
Nani anastahili hukumu kati ya
dereva na askari anayesimamia kanuni?,ukijiona umeonewa utakuwa mtu wa
kunung'unika tu ili hali wew ndo umevunja kanuni.
Nina maana gani hapa? Kwa taarifa
yako hakuna wachumba ambao hubaki na furaha mpaka ndoa isipokuwa wale ambao
hawakukutana kimwili,yaani hawakusahau kufunga mkanda wa usalama,kwani wale
wote ambao hufunga mkanda hata gari ikiyumba hawezi toka kwenye kiti na kwenye
uchumba ni hivyo hivyo si wakati wa kujiachia kwani endapo utajiachia utakwisha
tu.
Mahusiano ni kama probabation
period yaani wakati wa mtu kuthibitishwa kwamba ndiye au siye,waulize
wafanyakazi kama mimi katika kipindi unakuwa mchapa kazi ili mradi uthibitishwe
kuwa mwajiriwa,sasa mwenzangu na mie ile kuambiwa nitakuoa au tutaoana tayari
mnakuwa wanandoa kabla hata ya harusi.
Halafu unategemea kufika mwisho
kirahisi heeeeee!church boy wako radhi kula na kufuta ili usimsumbue mbeleni
kwani hatakuwa na furaha sana kwa sababu ya kuangukaz,church girl usilalamike
kisa jamaa kapita halafu hana habari na wewe ,si yeye ni nyinyi mlijiachia
mkatumia barabara vibaya kanuni ya cause and effect ikapitia hapo na faini yenu
yaweza kuwa kutofika mwisho.
Akija anayelia kwa sababu ya
mahusiano just muulize ulifunga mkanda wa usalama? Na kama ndio itakuwa kazi
rahisi kumshauri kwani utadeal na tatizo la kupotezewa muda na wala si lile la
kujuana kimwili.
Hakuna msafiri aliyeamua kushuka kwenye
gari na kutembea eti kwa sababu bus linachelewa,na kila mwenye maono husubiri
na kama hakuna subira hana anachoona mbele.Mkimuona mnatengenezeana mazingira
ya kukutana kimwili ni dhahiri hamna mnachosubiri simple and clear no future
ahead.
Team leader
FTF