KANUNI ZITAKAZOKUFANYA UFURAHIE MAHUSIANO YAKO



Waswahili walisema kinga ni bora kuliko tiba tena wakaongeza kusema usipoziba ufa utajenga ukuta wakiwa na maana endapo jambo la kwanza likitiliwa mkazo basi la pili halitatokea na kama la pili litatokea basi gharama yake ni kubwa na inauma kuilipa.

Kwa dunia yetu tuliyonayo kwa sasa mambo mengi yamerahisishwa,nakumbuka enzi ninakua kumpata msichana ili ni ngumu ilikuwa inabidi ujipange tena na kupiga misele karibu na kwao hata mara tatu kwa siku huku ukiwa na pamba za kuazima.Nakumbuka jeans yangu ya mikasi maana ilikuwa inanisindikiza na tena nilipoambiwa nisubiri palepale kwa siku zote mwanaume nilikuwa sibanduki mpaka mtoto amekuja,kwangu mimi naiona ilikuwa gharama sana tofauti na sasa ukitaka mrembo ni haraka tu unampata,ukiwa na smartphone ndo kabisa umemaliza maana hakuna haja ya misele.

Mnapokuwa mmekubaliana kuwa kwenye mahusiano yenye lengo la kuwaunganisha kama wanandoa hapo baadae ni sawasawa na mwanafunzi anayesubiri mtihani sasa basi ili afaulu kunategemea sana nini anafanya kwa ajili ya mtihani ulio mbele yako vivyo hivyo katika mahusiano mnavyoishi leo ndivyo mbele mtakavyokuwa,msitegemee furaha katika ndoa ikiwa leo mnagombana tena mara kwa mara.

Nia kuishi kwa furaha katika mahusiano yako leo kwa ndoa yenye furaha,zifuatazo ni kanuni chache zinazoweza kukufanya ufurahie mahusiano yako;

1Usihangaike kufuatilia nyendo zake.
Kwanini usihangaike? Ni kwa sababu hakuna mwanaume au mwanamke anayeweza kubadilika kwa kufuatiliwa kwa lugha pendwa usimchunguze.Utakuta mwingine anamfuatilia mpaka kwenye mitandao ya kijamii ili aone anakuwa hewani masaa mangapi.Kwa mtindo huu huwezi kumwamini na kama utamwamini basi ni kwa kuchelewa na ushaumiza akili kumbuka kumfuatilia hakumfanyi kuwa mwaminifu.

2: Nidhamu ya mawasiliano.
Kuna wengine wakishaingia kwenye mahusiano basi ni kila sekunde,kila dakika wako wanawasiliana tu,japo si mbaya ikifanywa kwa nidhamu ila zingine zinazidi.Yawezekana mwenza wako yuko kazini na kazi zinahitaji utulivu sasa mara griiii griiii kwa wengine sijui ila kwangu naona ni kero.ikifika hatua ya kuulizwa ulikuwa unaongea nani? Hebu niulize ulitaka ukipiga ukute niko huru tu au simu nilinunua kuwasiliana na wewe tu?! Daah! Tulia mpe nafasi ya kufanya mambo ya maisha huku mkifanya mawasiliano yenye tija.Uzuri wa mahusiano ni kusikia kile ambacho hakijasikiwa sio kila wakati ni hichohicho tu.

3: Usithubutu kumtaja taja ex wako.
Kwa moyo wangu kiukweli nikisikia mchumba wangu anamtaja ex wake mara kwa mara siwezi kufurahia tena nitajiona kiraka yaani nimepachikwa tu,mimi sijapendwa ila anajifariji tu kwa machungu ya ex wake.loooh!mwenzangu kaa kimya maana huwezi jenga nyumba mpya kwa msingi wa zamani au ghorofa kwa msingi wa tope.

4:Msile kabla ya kunawa.
Kwa ustaraabu wa kawaida anayestahili kula chakula kinapokuwa kimetengwa ni yule aliyenawa,kama umeshahudhuria misiba wanaopewa chakula ni wale walionawa;Ni kosa kutenga chakula kabla ya maji ya kunawa na endapo utafanya hivyo basi huduma yako haitafurahiwa.Kula kabla ya kunawa ni kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa.
Rafiki yangu mmoja alinambia baada ya kudumu kwenye mahusiano kwa miaka kama miwili wakajikuta wamekutana kimwili,tangu siku hiyo akawa hana furaha na mchumba wake,nikamuuliza kwanini? Akanambia ni kwa sababu nimemtenda Mungu dhambi hivyo sifurahii tena kuwa na yeye lakini pili ananitia wasiwasi kwani kila akiniona anataka tufanye sasa mimi nikiwa mbali na yeye nani anamtimizia? Mwishowe hawa watu waliachana kabisa.

Kwa hizo chache furahia mahusiano yako,zingatia ili upunguze uwezekano wa kuumizwa.

Laban Nzelela

0656574760