JE! UNAJISIKIA KUVUNJA MAHUSIANO YAKO?



Una mwaka mmoja kwenye mahusiano na umeanza kujisikia kuvunja mahusiano yako? Ule upendo wa mwanzo. Uliokuwa nao unaonekana kuyeyuka?,maneno na lugha tamu za mwanzo ndo zinakufanya uhisi kuvunja maana unahisi upendo hakuna ?
Daaaah! Mbaya sana kwa kasi uliyoanza nayo kwa sasa unahisi huwezi kuendelea tena? Au unahisi ulikurupuka? 

Maswali mengi unaweza kujiuliza na kujiuliza tena mara kadhaa na hata moyo wako kusongwa na hofu na ile hofu inakupelekea kujisikia hivyo unavyojisikia.
Kuna kipindi nilipitia katika wakati kama huu,na haikuwa rahisi kwangu kuamua kuendelea mbele na mahusiano niliyokuwa nayo maana nilikuwa napambana katika ufahamu wangu na kila kukicha naona warembo wengine tena ni wazuri kuliko niliyenaye hivyo nilipita.Lakini kwa sasa nimekuwa sawasawa katika mahusiano yangu na nayafurahia kwa sasa.

Mpenzi msomaji wa makala hii labda niseme tu ,"kadri gari linavyopanda mlima ndivyo hata mlio wa gari hubadilika na hubadilika kwa sababu safari inakaribia kuwa nyepesi si muda litafika kwenye njia nzuri na kurudi kwenye mlio wake wa kawaida",

NINI UFANYE UNAPOFIKIA HAPO?
Kuna mambo yanaweza kuchangia hali hii lakini unapofikia kwenye dilemma kama hii yaani uache au uendelee?,fanya hayo yafuatayo;

1:Heshimu maamuzi yako
Kwanini nasema kuheshimu maamuzi yako? Iko hivi watu wengi wamejikuta wakiyasaliti maamuzi yao na pia wakiacha sintofahamu katika jamii zao,kutoheshimu mawazo wako ni "sabotaging" yaani unajihuhujumu mwenyewe,hata mfanyabiashara ambaye anataka kufanikiwa ni lazima awe na uwezo wa kuheshimu maamuzi yake.

Sababu inayoweza kupelekea maamuzi yako kubadilika ni yale unayoyaona sasa aidha inatamani wengine au udhaifu wa mwenzio,au ushauri kwa watu wengine.Kama ulichukua tulivu kutaka kupata mwenza wako kwa ajili ya ndoa nina hakika yalikuwa maamuzi ya hakika,huwezi ukasikia upendo umekufunika nyakati zote,mahusiano ya kwenye tamthilia si yako,imekupasa uyaishi ya kwako,uyatengeneze yako ili ukajivunie.

2:Tumia mapungufu unayoyaona kama nafasi ya kuonyesha upendo wako.
Mtu mmoja alisema ,"you will never find a perfect woman or man" na mimi nasema if you want a perfect lover,be that lover".
Mpenzi wa kweli anatengenezwa na mwenzi wake,tell your lover what you him or her to be,otherwise you will be breaking every courtship you establish and finally you will to be problem to your life.

3:Mueleze kwanini ulimchagua yeye miongoni mwa wengi.
Achana na kufumbia macho vitu ambavyo hukumkuta anavyo na ghafla alipokuwa nawe akaanza kuwa navyo,yawezekana anafanya vile akidhani utavutiwa zaidi kumbe ndo anakupa maswali zaidi kuhusu yeye kama ni mtu sahihi kwako.
Jizoeze kumwambia kila wakati hii itakusaidia kukupa amani na faraja na hata yeye atasema laaah!kweli nina mwenza wa ukweli na sio kila jambo unakuwa unajifanya unalikubali kumbe hata sivyo.

4:Zungumza na mwenzi wako kwa hatua mliyofikia na mnapoelekea.
Kama kuna jambo la msingi katika mahusiano ni hili kwa sababu huwezesha kujua mmefanikiwa kiasi gani,hii ni tathmini,huwezi kufika mahali ukafurahia ikiwa hakuna muda wa kutathimini kwa kiasi mmeweza kufanikiwa hasa katika malengo ya pamoja na yale ya binafsi.
Hayo ni baadhi ya mambo ambayo ukiyafanya yanaweza yakakuokoa katika hali hiyo ni muhimu sana kuyafurahia mahusiano yako na palipo na furaha hapakukosa kuparuzwa kwanza.Usikubali mazingira ya nje yaharibu mahusiano yako maana ni eneo la kutengeneza sura ya maisha yako ya baadae.

  Laban Nzelela

   065654760