*WAZAZI WAHESHIMIWE LAKINI SI KATIKA HILI* ~ Laban Nzelela


Siku moja nikiwa kwenye pitapita zangu ,nikaingia stationary moja na kumkuta mama mmoja ambaye ndiye mmiliki wa ile stationary akiwa na mfanyakazi wake.
Kwa kuwa nimezoeana sana na yule mfanyakazi wa stationary nikamtania kidogo kwa kumwambia,"kwanini hutaki nikuoe", ghafla yule mama akasema,*mmmmh vijana kama mnaoa oeni tu ila kwa kijana atakayeoa kwangu lazima ajishike*, nikamuuliza kwanini anasema hivyo?ndipo akanambia ushuhuda wakati anamuoza binti yake,na ilikua hivi;

Mama:Hivi mwanangu umempendea nini binti yangu? Maana kwa dini yetu tunaangalia vigezo kadhaa kama vile;uzuri,tabia na mali?
Kijana:  mwanao sijampendea kwa sababu ya elimu yake bali kwa tabia yake na uzuri pia.
Mama:   basi kama ni hivyo mke umepata lakini sikupi elimu yake wala elimu yake,fahamu kabisa mshahara wake na kazi yake havikuhusu kabisa. Kama masharti huyawezi basi muache mwanangu.

Duuuuh!!!!!! Maneno yalinichosha sana nikakumbuka imeandika mtu atawaacha wazazi wake na ataambana na mumewe au mkewe, nikajiuliza mengi sana je!!hii ndoa itakuwaje huko ndani maana yawezekana binti atakuwa na mafundisho ambayo ni matango pori,na ndoa itakuwa kama matangori.

Ikiwa mke au mume atakuwa hana maamuzi binafsi juu ya ndoa yake au uchumba basi mtu huyo atawaliwa na wazazi na madhara yatakayo tokea ni;

1:Atawaza kujenga au kuboresha kwao na kusahau kwamba anapaswa kujenga kwake yaani kwa mke au mume wake maana hao wameambatana .KUAMBATANA  ni kuunganisha,kuleta na kukusanya pamoja maono na mipango yenu kwa ajili ya ustawi wenu ,hivyo ikitokea unawaza sana kuhusu kwenu basi ilipaswa ubaki kwenu.

2:Hatokua na siri yoyote kwa wazazi,kila kitu anachopitia katika ndoa au uchumba vyote atakuwa anamimina kwa mzazi wake.Ndugu usiombe upate mtu wa namna hiyo .

3: Hatokuwa na maamuzi binafsi mpaka wazazi wamesema ndio.
Ni aibu kubwa sana kwa binti akiambiwa na mchumba wake mipango ya maisha au na mumewe hajibu mpaka ameuliza mzazi wake,halafu la mzazi na linashupaliwa kuliko.Hivi kwani huwezi kujiongeza ?najua ni mzazi wako lakini yeye alishamaliza yake hivyo fanya yako kwa utaratibu unaokubalika.

Numalizie na hadithi kukikuwa na mama mmoja ambaye akikuwa anafanya kazi BOT na ikatokea akamuoza binti yake lakini yule mama alikuwa ni wa kufuatilia kila siku,utasikia mwanangu umekula nini,unashiba kweli,kama yanakushinda njoo nyumbani haukufukuzwa na mengineyo mengi.

Je !mzazi apaswa kufanya hivi? Je siku wakifa itakuwaje sasa?

     Laban Nzelela
       0656574760