Wakati tukikuta mambo yetu hayaendi huwa
tunadhani kuna mchawi anaiingilia mambo yetu kumbe mchawi wa mambo yetu ni sisi
wenyewe na si vinginevyo .
Zifuatazo ni sababu kumi zinazokufanya
usisonge mbele :
1.Huna ndoto : Kama hujui unataka nini
katika maisha yako wewe utakuwa ni mtu wa kusubiri Jua lichomoze na kuchwa
.Hutakuwa na msukumo wa ndani wa kuhakikisha kuwa siku moja ndoto yako inakuwa
kweli .Umekuwa ukifanya vitu kwa mazoea kwa sababu huna ndoto yoyote
inayokufanya kuwaza kila siku namna gani utaifikia.
2.Unawasikiliza watu sana kuliko
kujisikiliza mwenyewe:Maisha yako ni yako na si ya kaka yako wala mjomba wako
au ndugu yeyote na rafiki yeyote uliye naye . Kila mtu atabeba mzigo wake
mwenyewe(Every body will carry his own burden).Kama unaamini katika
unachokifanya na unajua kitakufikisha mahali endelea kufanya kadri unavyoweza
.Watu wengi si wazuri na hawajui unakokwenda japo wanaweza kujua ulikotoa .
3.Hutafuti Maarifa : Bila maarifa
hutaenda kokote na maisha yako hayatabadilika .Utakuwa kama mtu anayepiga ngumi
ukutani ambapo mwisho wa siku huumiza mkono wake mwenyewe .Kama siyo msomaji wa
vitabu ,kuperuzi kwenye mtandao kutembelea blog kama www.kijanajithamini1.blogspot.com
na www.maishanamafanikio.blospot.com
hautaweza kupata maarifa ambayo yatakufanya ufanye mambo yako kwa uwaredi
mkubwa na kwa tofauti .Utakuwa ni mtu wa kufanya mambo kimazoea maana huna
maarifa na mwisho wa siku hutatoka pale ulipo.
4.Unajihurumia sana : Umekuwa mtu wa
kujihurumia sana na kutaka kukaa kwenye comfort zone ,sehemu ambayo unapata
vitu kwa urahisi .Hutaki kuumiza kichwa
na kuwaza juu ya maisha yako .Umekuwa mtu wa kutaka vitu ambavyo vimeshafanywa
na wenzio maana hutaki kuteseka na kukutana
na changamoto .
5.Unaishi kwa yaliyopita : Maisha siyo
jana maisha ni kesho .Kama ukiangalia ulivyoshindwa jana hutafikiria kuhusu
kesho .Ukiangalia biashara ya jana ilivyodhurumiwa na kuibiwa hutafanya
biashara kesho .Acha kabisa kuishi kwa ya jana hutasonga mbele .Angalia sana
kesho yako , Maisha ya watoto wako wa kesho ,mahusiano na familia yako ya kesho
na si vinginevyo .
6.Huchukui hatua : Umekuwa mtu wa kusema
nitafanya kesho na kesho ikifiika hufanyi .Umekuwa na mipango mingi isiyokuwa
na utekelezaji .Kama huchukui hatua utabaki hapo hapo ulipo hakuna jambo jipya litakalotokea .
7. Unasubiri Matokeo ambayo hujafanyia
kazi ; Usitegemee muujiza .Kile apandacho mtu ndicho atakachovuna .Unawezaje
kuvuna mahali ambapo hujapanda??? Hey ! Unawezaje kuvuna maharage kwenye shamba
la mahindi???? .Newton anasema ili kazi ifanyike lazima kani (force) itumike na
umbali(distance ) uwepo .Hakuna matokeo yasiyosababishwa.
8.Huzalishi mawazo : Umekuwa mtu ambaye
hutaki kuwaza kwa mtazamo mpya na kuzalisha mawazo mengi kadri iwezekanavyo
.Umeishi kwa wazo la mwaka 1999 mpaka leo na hujui kama dunia imebadilika .Hey!
Amka anza kuzalisha mawazo .
9.Umeishi kwa tahadhari nyingi :Kila
kitu kwako umechukua tahadhari ,unahisi ukianza biashara fedha zako zitapotea
,unahisi ukianzisha kitu hakitasonga mbele .Kwanini umekuwa hivo (too cautious)
????.Kama hutaachana na tabia hii hutatoka mahali ulipo na kamwe usitafute
mchawi .
10.Hujifanyii tathimini :Huna tabia ya
kupima yale uliyoyafanya kwa siku,wiki,mwezi na mwaka na hivyo unahisi kama
unaenda mbele kumbe unarudi nyuma .Ni muhimu ukawa na tathimini yako binafsi
katika mabo yako
JYB(0753836463)