“NGUVU YA MATENDO” ~ Joas Yunus




Jana usiku nilikuwa niko naperuzi kwenye mtandao wa youtube na nikakutana na somo ambalo ndugu yangu Lameck Hulilo alilowahi kufundisha na likanigusa sana .Somo hilo ni nguvu ya matendo  unaweza kulipata hapa : https://kijanajithamini1.blogspot.com/2016/07/nguvu-ya-matendo-by-lameck-amos.html

Muigizaji mmoja aliwahi kusema kuwa maneno huwa yanajenga ghorofa lakini vitendo ni swala lingine .Watu huwa ni wazuri sana katika kuongea na kuwa na mipango mikubwa lakini siyo watendaji wa yale wanayoyasema na kuyasikia .Na hii ndio sifa ya watu wa kawaida (average/poor people).Jack Ma Mwanzilishi wa Alibaba group aliwahi sema " Poor people think like university proffesor and do less than blind people "  akimanisha kuwa Maskini wengi wanawaza kama maprofesa lakini utekelezaji wao wanazidiwa na vipofu .

Unapopanga kitu chochote,ni muhimu kuweka mpango utekelezaji (Action plan) ili kile ulicholipanga kianze kuonekana .Najua mwaka huu ulikuwa na mipango mingi na uliiandika lakini je , kipi mpaka sasa umekifanya katika yale yote uliyoandika.

Vitendo huongea zaidi kuliko maneno(Action speak louder than words).Usiwe ni mtu wa kupanga mdomoni tu kwa maneno lakini ni vema sana ukaangia kwenye matendo .Kama umepanga kuanzisha biashara mwaka huu ni vizuri mara moja ukaweka mpango wa kibiashara (business plan ) na mpango wa kimasoko(marketing plan) tayari kuingia kwenye utendaji .

Baada ya yule mwanamke aliyekuwa anatokwa na damu kwa miaka mingi(Rejea Maandiko ya Biblia kwa wale tunaomini Biblia) alipoamua kwenda kugusa pindo la Yesu ndipo alipopata uponyaji .Hakuna jipya litakalotokea  juu ya maisha yako kama huchukui hatua utabaki kuwa na mipango mingi iliyoandikwa kwenye makaratasi ambayo hakuna chochote kitakachobadilika katika maisha yako na thamani yako itabaki kuwa ile ile .

Ukweli ni kwamba makaburini ndiko  kwenye utajiri mkubwa maana watu waliokuwa na mawazo ya kuanzisha makampuni na biashara kubwa walikufa bila kufanyia kazi  .Kwani ufe na kampuni yako kichwani ambayo ingeajiri vijana wengi wasio na ajira???

Ni kweli umekuwa ukihamasishwa sana lakini ni kwa namna ipi kuhamasika kwako kumebadilisha mtazamo wako??? .Ni kwa namna ipi umeanza kuweka yale unayosikia kwenye utekelezaji.

Ukianza mguu mmoja katika kutembea mguu mwingine hufuata.Mara tu unapoanza kuchukua hatua ya utekelezaji mambo mengi na mawazo mengi yatakuja lakini ukiendelea kusema nitafanya miaka si rafiki na unaweza usifanye .Acha tabia ya kuahirisha mambo na kusema nitaanza kesho .

Mbona kuna vitu visivyo na tija umevipa vipaumbele na huwa huchelewi kuvifanya kuliko kufanyia kazi ndoto zako kwa mustakabali wa familia yako na maisha yako kwa ujumla???

0753836463