"KUMBE UNAPASWA KUBADILI MFUMO WA MAISHA YAKO" ~Joas Yunus


Moja ya sababu ya msingi kwa timu yoyote kuweza kushinda ni mfumo wa uchezaji .Makocha huumiza sana vichwa sana kujua timu yake kwa kutumia mfumo gani .Utasikia kocha anasema kuwa yeye atachezesha timu yake kwa kutumia mfumo wa 4:4:2 na mwingine utasikia  anachezesha mfumo wa 4:3:3 n.k

Muda mwingine timu ikishindwa watu huanza kusema kuwa kocha alikosea kupanga mfumo wa kucheza na  utakuta kocha analazimika kubadili mfumo wa kucheza kwa mechi zijazo ili kupata matokeo makubwa .

Ukisikia wanafunzi wengi hawaajiriki na hawezi kujiajiri ni kutokana na mfumo wa Elimu butu ambao hautoi Elimu ambayo inamuandaa mwanafunzi kupambana na mazingira yake na sasa wanafunzi wengi wako mitaani huku wakiwa na vyeti utadhani na wameanza kuitwa wanafunzi hewa .Kinachopaswa kutafutwa hapa si mchawi wa Elimu yetu na kuingiza siasa bali ni kwenda moja kwa moja kubadili mfumo wa Elimu tulionao(Salaam Zimfikie waziri wa Elimu Dr Joyce Ndalichako ).

Kimsingi mfumo/aina ya maisha tunayoishi yana mchango mkubwa katika maisha yetu na huweza kusabababisha kufanikiwa kwetu au kutofanikiwa kwetu .Kuna mtu mfumo wa maisha yake ni Uvivu(uzembe) mtu huyu kamwe hawezi kufanikiwa .Kuna mtu mwingine mfumo wake wa maisha umejawa hofu na hawezi kufanya chochote ,mtu huyu hawezi kufanikiwa kama hatabadili mfumo wa maisha yake .

Unapaswa kukaa chini na kujiuliza ni mfumo gani wa maisha unaoishi kwa sasa .Andika chini na anza kubadili kile ambacho unaweza kukibadili na bahati nzuri ni kwamba vitu vingi tunao uwezo wa kuvibadili.

  • Kama mfumo wa maisha umejawa na hofu ya usichokijua amua leo kubadili mfumo huu ambao haulengi kupata matokeo chanya.
  • Kama mfumo wa maisha yako umejawa na Uvivu kuanzia leo amua kubadilika .
  • Kama mfumo wako wa maisha ni kuongelea watu siku nzima ,amua kubadilisha mfumo huu unaokutafuna .
  • Kama mfumo wako wa maisha ni kuambatana na watu ambao hawakusaidii chochote huku wakikutafuna amua kubadili mfumo huu mbaya usiokupeleka kwenye hatma yako
  • Kama mfumo wako ni kuamini vitu hasi amua kuwa na mfumo chanya


0753836463