Ili uweze kufanya kitu chochote katika
maisha yako kinacholenga kubadili maisha yako lazima uwe na nguvu ya uwezekano
ndani yako ,Nguvu hii ndio itakusukuma kuona yale ambayo watu wanasema
hayawezekani kwako utaona kuwa yanawezekana .
Ukiona vitu vikubwa ambavyo vilitokea na
vinazidi kutokea ambavyo vimefanywa na wanasayansi wakubwa ,ujue ni kutokana na
nguvu ya uwezekano iliyoko ndani yao na kufanya vitu vikubwa ambavyo tunaviona
leo .
Pastor David Oyedepo wa makanisa ya
Winners Chapel na mmiliki wa Covenant University nchini Nigeria aliwahi kusema
akiwa anaongea na mamilioni ya watu kwenye Kanisa lake maneno haya "What
was impossible yesterday is possible today" akimanisha kuwa kile ambacho
jana hakikuwezekana jana leo kinawezekana .
Ili ufanikiwe katika maisha yako lazima
mtazamo wako uwe katika uwezekano na kuamini kuwa hakuna kisichowezekana kama
ukiamua kwa dhati kufanya jambo hilo unalofikiri kulifanya .Yawezekana Jana
halikuwezekana lakini leo likawezekana .
Wakati nasoma shule ya msingi mara
kadhaa nilikuwa nafanya mitihani kwenye kitabu cha hesabu kilichoitwa
"Mwandani mwa mwanafunzi" na kitabu kingine kilichoitwa " Jipime
katika Hisabati" .Kuna wakati nilikutana na majaribio magumu sana na
nikawa nawaza kuliacha jaribio hilo na kwenda jaribio lingine rahisi lakini
Niliamini kuwa labda akili ilikuwa imechoka na ndio maana niliona maswali kuwa
ni magumu na kesho yake nilivyojaribu kufanya jaribio lile lile nikakuta
maswali yanafanyika vizuri.
Maisha yetu ni vile tunavoamini ,Kama
tukiamini kuwa jambo linawezekana kila Jambo
litawezekana maana ubongo wetu hupokea kile tunachokiamini .Ukiamini kuwa jambo
fulani haliwezekani kweli alitawezekana na ukisema linawezekana litawezakana
maana msukumo wa kufanya jambo unaotoka kwenye ubongo hutokana na nini
umeingiza kwenye ubongo .Kile unachoingiza kwenye ubongo ni kichochezi
(impulse) na kisha ubongo hutoa mwitikio (reaction).
Nafahamu unaweza kuwa ulisikia wale watu
waliotaka kujenga mnara wa Baberi ili wafike mbinguni .Kwa akili ya kawaida
siyo rahisi kuamini kuwa Mnara ungeweza kujengwa kirahisi namna ile lakini
nguvu ya uwezekano ndiyo iliwafanya waamue na waingie katika utendaji .Ukweli
ni kwamba mnara ulianza kujengwa kwa
ushirikiano mkubwa na Mungu akastuka ikabidi awachanganye Lugha ili wasielewana
na hawakufanikiwa kujenga Mnara maana Mungu aliwazidi akili.
Kama ukiamini katika Uwezekano hakuna
kitu kitakachokuzuia na hivyo unaweza kuwa vyovyote unavyotaka kuwa bila
kuangalia haijalishi kuna vizuizi vingapi .
0753836463