Wakati mtu anavyoanza kufanya kitu
fulani au kufikiri kuanzisha kitu fulani hupitia changamoto kubwa na hasa
changamoto ya kukatishwa tamaaa kutoka kwa watu wanaomzunguka .
Unaweza kukuta mtu amegundua mwenyewe
kuwa ana uwezo mkubwa na kipaji cha kuimba lakini watu wanaomzunguka utasikia
wakimkatisha tamaa kwa maneno kama haya " hivi wa kuimba atakuwa
wewe???" "Wapi familia yenu na kuimba??". Hawa Kaa nao uwaambie
kuwa kwa sasa hawewezi kukuelewa maana hawajui unakoenda na wataamini siku
nyimbo zako zikirushwa redioni na hapo ndipo watakuja kwako kwa mara ya pili .
Huyu Diamond ambaye kizazi cha dot com
kinamshabikia sana alianza naye chini sana na hakueleweka mwanzoni na leo
wameanza kumuelewa .Binadamu huwa ana tabia ya kuelewa badae.Wewe ni shahidi
wengi darasani mwalimu akitoka ndo huwa wanaelewa .
Mark Zuckeberberg mgunduzi wa facebook
mwanzoni wakati anapata wazo la kutengeneza mtandao wa mawasiliano chuoni kwake
watu hawakuwa wanamuelewa vizuri na wengi walidhani asingeweza kufika kokote
hasa baada ya kufukuzwa chuo watu walijua ndo mwisho wa maisha yake na programu
yake ya facebook lakini sasa hao waliodhani hivo sasa wako facebook wanatumia
akili ya Zuckeberberg.
Ni kawaida kabisa kutokueleweka mwanzoni
na ndio maana hata wewe watu hawakuelewi na wanasema umepotoe njia kumbe wao
ndo wamepotea njia .Mtoto anapozaliwa ni ngumu kujua hasa anafanana na nani
mpaka akianza kukua na kuonesha sura
yake halisia .Kwanini watu wanakuogopesha wakati hata hawakujui wanabahatisha
??
Najua fika kabisa katika hilo
unalolifanya na unalowaza kulifanya kuna watu wengi wamekwambia hutafika kokote
na wakakupa mifano ya watu waliokuja na mawazo kama yako .Wamekuonesha
changamoto nyingi zilizo mbele yako badala ya kukuonesha fursa zilizopo mbele
yako ambazo ndizo zinakusukuma kufanya zaidi .Hawa waeleze wazi kuwa ni vema
wakakaa chini maana bado ni mapema kwa wao kuweza kukuelewa wataelewa baadae.
Kuna stori moja kwenye kitabu cha dini
kiitwacho BIBLIA ya Nuhu .Nuhu alivyokuwa analanda mbao kwa ajili ya
kutengeneza safina kwa gharika iliyokuwa mbele watu hawakumuelewa mpaka
yalipowakuta mafuriko na watu wengi wakaangamia.Hawa walielewa baadae mwanzo
iliikuwa vigumu kumuelewa Nuhu .
Kuna watu watakuelewa baada ya matokeo
au kukuta sehemu fulani .Unajua stori ya Yusufu ??? unakumbuka njinsi ambavyo
famikia yake haikumuelewa mwanzoni??? alipokuwa akiwasimulia ndoto ndugu zake
nahisi kama walidhani amechanganyikiwa lakini mwisho wa siku walimuelewa baada
ya yeye kuwasaidia walivyokutwa na njaa na yeye akiwa ni waziri mkuu wakati huo
.
Hey! kwanini unaangalia watu ambao
hawakuelewi ???? ,Wewe endelea mbele .Kama unauza genge uza sana na boresha
.Kama una mawazo makubwa fanya sana hao wanaokuzunguka wataelewa taratibu kama
mwanafunzi anayeelewa baada ya mwalimu kutoka.
0753836463