*NAMNA YA KUPATA MAWAZO MAZURI (GOOD IDEAS)

                                          


*Utajiri* wowote huanza na wazo .Wazo ni kama *mbegu *ya mahindi abayo baadae huzae mahindi mengi zaidi .Unapoosikia utajiri Mkubwa wa Bilgate alianza katika wazo .

Kuwa na wazo tu haitoshi ni lazima ufanyie kazi mawazo unayozalisha.Ni ngumu sana kufanyia kazi mawazo tunayopata kila siku kwa wakati lakini ni muhimu kuyaandika na kuyapa vipaumbele(uanze na lipi ).

Kumekuwa na shida kubwa kwa watu kupata mawazo mazuri na wengine kujiuliza kwa namna gani watu wengine wanapata mawazo mazuri .Ukweli ni kwamba kila mtu anaweza kuwa na mawazo mazuri kama akifuata kanuni za kupata mawazo mazuri .

Hizi ni baadhi ya njia ambazo unaweza kuzitumia kupata mawazo mazuri ,kinyume na hapo utabaki kusema huna bahati na kuwa watu wengine wanatumia uchawi kumbe mchawi wa kwanza ni wewe.

1.*Tafuta marafiki wapya* : Ni muhimu kuhakikisha kuwa unapata marafiki wapya kwa namna yoyote.Kuna watu kwa mwezi hawatafuti marafiki wapya na wamekuwa ni watu wa kukaa na watu wale wale ,wenye tabia na mawazo yale yale na wamewafanya wasifikirie zaidi ya wanavyofikiri.

Ndugu watu waliofanikiwa na wanaofanikiwa wana tabia ya kutafuta marafiki wapya ,wenye mawazo mapya ,mitazamo chanya na kiu ya mafanikio.Hakuna namna utapata mawazo mapya na mazuri kama unakuwa na marafiki wale wale .

2. *Soma vitabu kila siku*: Ukitaka kupata mawazo mapya hakuna namna utakwepa kusoma vitabu kila siku na kupata maarifa mapya .Kupitia vitabu unaweza kupata wazo zuri kupitia maarifa unayopata .Ukweli uko hivi kama hupendi kusoma vitabu hautaweza kupata mawazo yoyote.

3. *Kuwa mtu wa kuchunguza vitu* : Hii pia ni njia ambayo inasaidia kupata wazo zuri .unapopata ziara kwenda mahali fulani ni njia nzuri ya kujifunza na kupata mawazo mapya ,chunguza sana vitu utakavyovikuta huko .Unaweza kupata wazo kokote kule kama ni mtu unayechunguza vitu .Kuna watu wao wakisafiri njia nzima wanalala tu ,hawa hawapendi kujifunza na kupata mawazo kwao si kitu rahisi na chepesi .

4. *Peruzi Kwenye mitandao (web surfing) *; Dunia ya leo ya TEHAMA imeturahisishia vingi kwa makusudi yetu tumeshindwa kutumia mtandao vizuri .Tuna simu nzuri sana ambazo kupitia hizo tunaweza kujifunza mambo mengi lakini simu zetu zimekuwa za kuchat tu watsap na  kubadilisha profile zao facebook

5. *Penda kuandika (Keep Journal) * : Kimsingi huwa tunazalisha mawazo mengi sana kwa siku lakini hatuna utamaduni wa kuandika mawazo yanayokuja akilini mwetu .Kuna mawazo tuliyapoteza kwa kutokuandika na kuyapuzia na hayo watu wengine walivyoyapata wamekuwa matajiri .Mawazo yatakuja popote na muda wowote kwa hiyo ni muhimu kuwa na journal .Simu yako ya mkononi inaweza kukusaidia au Diary book .Katika mawazo mengi unayozalisha na kuyaandika utapata wazo zuri .

      *JYB (0753836463) *