SABABU NNE (4) ZINAZOTUFANYA KUSHINDWA KUFIKA TUNAPOTAKA KUFIKIA ~ Seth Jacob




Kuanguka ni miongoni mwa mambo ambaayo watu wengi hatuyaelewi sana.  Tunaamini ni kitu cha kukiogopa na kukikwepa kwa nguvu zote na gharama zote. Na mbaya Zaidi kushindwa huko hakuna mtazamo mzuri mbele za jamii. Fikiria mtu umekopa pesa bank halafu ukafilisika vibaya na kuipoteza yote.. Umefanya mtihani na ukafeli vibaya au umeanzisha mradi Fulani umeshindwa kuendelea. Inaumiza sana. Kwa mtu ambaye hajajulia mchezo huu anaweza kuhisi ana laana. Tunaamini kuwa kushindwa  ndio kitu kibaya kuliko vyote.  Ni kweli kuwa sio kitu kizuri sana kwa mtazamo wa kawaida kama kitakukuta. Nakumbuka kuna wakati niliweka pesa nyingi kwenye biashara Fulani na ikapotea yote. Iliniuma sana lakini nikajua kuwa ili niimarike katika biashara lazima kuanguka kwanza.  Kuna msemo unasema kuwa tunashindwa kwa sababu hatujajifunza vya kutosha.  Kuna funzo zuri sana lipo katika kushindwa. 

Sababu zinazokufanya uanguke  au ushindwe ni kama zifuatazo:::::::;

1.UNAKATA TAMAA MAPEMA SANA.
Ni sababu kubwa sana hii. Watu wengi wanaanguka kwa sababu wakata tamaa mapema. Pale ambapo mambo hayaendi wao wanahisi ndio mwisho. Kumbuka kuwa tunaishi katika ulimwengu wwenye milima na mabonde. Misukosuko ndio mwendo wa ngalawa.  Labda hujaona faida au matokeo mazuri kwa muda wa miezi mitatu, sita au mwaka mzima unahisi sasa haiwezekani. Mafanikio huchukua muda mrefu sana. Kuanza kuona faida itakuchukua miaka mingi. Usikate tamaa. Tengeneza misingi mizuri na usikubali kupoteza zile jitihada zako ulizoziweka tangu awali.

2. UNAOGOPA MNO KUANGUKA.
Kumbuka kuwa hatua yoyote ya mafanikio huwa na maumivu makubwa sana. Tumia mfano rahisi wa mtoto anayejifunza kutembea huanguka mara nyingi sana. Lakini yule mtoto mwoga kuanguka huchelewa sana kutembea. Wapo wanashindwa mapema  kwa sababu ya woga wa kuanguka. Akishaona kuna dalili kama mambo hayaendi anakuwa ameshashindwa.  Kama una malengo mazuri hakikisha unapunguza kuogopa kushindwa. Angalia nini nini utakipata mwishoni.

3. HUJAWAHI KUANGUKA MARA NYINGI.
Jambo mojawapo la kukufanya ushindwe kwenye mipango yako ni  kuwa huna uzoefu na kuanguka.  Kuanguka kuna funzo kubbwa sana. Mtu aliyeanguka mara nyingi huwa imara sana. Anajua wapi huwa panasababisha akaanguka. Ana ujuzi,  maarifa na uzoefu wa  kutosha.  Huwa makini sana katika kila hatua. Ni mwepesi sana wa kulisoma anguko na kulizuia au kulikwepa.  Na kijiwekea tahadhari kubwa sana.

4. HAUPO TAYARI KUPATA MAFANIKIO.
Kila kitu kina maandalizi ya namna ya kukipokea. Mafanikio yanayokuja bila kupangiliwa hupotea  mapema sana. Lazima uwe na mipango sahihi ya kila hatua ya mafanikio.  Lakini pia lazima ujue namna gani utaweza kuyashikilia mafanikio hayo. Umefika kilele cha mafanikio yako. Unawezaje kubakia juu hapo. Unawezaje kumudu sifa unazozipata kutoka kwa watu? unawezaje kubakia na nidhamu ile uliyokuwa nayo wakati uanyatafuta? Watu haunguka mapema kwa sababu ushindi wa kwanza huwaondolea nidhamu, umakini na bidii ya kupata mafanikio Zaidi. Hapa ndipo uankuta mtu anaanza kurudi nyuma. Uanchotakiwa ni kuendelea kuhitaji Zaidi na Zaidi.


Unaweza kutupata Zaidi kwa kutembelea mtandao wetu uitwao www.mimimjasiriamali.com , pia kumbuka kulike page zetu mimi mjasiriamali.com  na Grow RICH TZ. Karibu sana.