Ninakwenda kuzungumza kwa kifupi juu ya Watu 3 muhimu wa kua
nao katika maisha yako ili uweze kufikia mafanikio makubwa .
Tupo kwenye dunia ambayo tulikuta watu na tutawaacha watu.
Vyote tulivyovikuta vilianzishwa na binadamu wengine wenye mawazo mema na wenye
mawazo mabaya pia. Vitu vingi tunavyovifanya tunaendeleza tulivyovikuta ni mara
chache kukuta kitu kipya ambacho hakitegemei mazingira na asili ya
tulivyovikuta. Hivyo basi kwa vyovyote vile unahitaji mtu wa kukuongoza au kuku
Coach ili ufanikiwe katika pande zote za maisha.
Nitakwenda kuzungumzia sehemu kuu tatu za muhimu sana ambazo
unatakiwa uwe na watu wa kukuongoza ili uweze kukua na kupanda viwango kila
wakati. Ni vitu vya kawaida sana lakini leo nitakwenda kuzungumzia uone ilivyo
muhimu sana wewe kua na vitu hivi maana bila vitu hivi mafanikio yatakua magumu
sana kufikia. Safari yako itakua ngumu zaidi kama utakosea sehemu hizi tatu.
Tumekua tukizoea kuishi kwa mazoea sasa tunatakiwa tubadili
hali hii ili tuweze kua na mabadiliko.Nitaomba tuelewane kwamba hapa huendi
kuiga au kua hawa watu utakua wewe na utatimiza lile kusudi la Mungu ndani
yako. Kwanza kabisa uko hivyo ulivyo kwa
sababu ya mazingira uliyokulia na watu tulioishi nao tangu ukiwa mtoto hadi hapo ulipo. Kuna tabia nyingi sana unazo
kutokana na mazingira uliyokulia. (Hapa ndipo nakutana na kitu ambacho
nakipenda sana kujifunza kwa wengine napenda kujifunza kwenye mazingira mapya
na kwa watu wapya kwa kua wameishi maisha ambayo mimi siyajui na wanafahamu
vitu vingi ambavyo mimi sifahamu.
Watu wana utajiri mwingi sana ndani yao
ukiweza kukaa na mtu ambaye humjui kabisa unaweza kujifunza mambo mengi ya
ajabu kwake. )Dunia ya sasa inabadilika kwa haraka sana ni wachache sana
wanaofaidi mabadiliko haya. Wale wanaoona mbele wanaoona mabadiliko na
kuyatumia.Kwa sasa zipo njia nyingi sana za kuwafikia watu ukilinganisha na
miaka mitano iliyopita.Dunia inakimbia sana kwa kasi kubwa. Kila siku vinakuja
vitu vipya vinavyotuwezesha kufikia mafanikio kwa haraka.
Hawa ndio watu wa Muhimu sana kwenye safari yako usiwakose
ili uweze kusonga mbele. Sifa zao kabla hujawachagua ni za muhimu sana pia ili
wasije wakakupoteza badala ya kukufikisha kule unakotaka kwenda.
- Awe na mafanikio (Amefika Mbali) kwenye hiyo sehemu.
- Awe na Tabia njema zinazokubalika na jamii yake na dini yake. (mfano hapa ukikutana na mtu ambaye anakuelekeza kuhusu biashara na ni mlevi na mzinzi hizi tabia lazima atakuambukiza kwasababu atakua mtu wako wa karibu sana)
- Awe amekuzidi sana kwenye kile unachotaka akulelee (akuongoze).
Hizo ni sifa za muhimu tu za kuangalia zipo nyingine nyingi
sana utajifunza mwenyewe.
Hawa ni watu wa muhimu pia na ni muhimu sana kua nao kwenye
maisha leo nazungumzia watu wa karibu yako kabisa ambao watakua wanakufundisha
na kukuelekeza.
1. MLEZI WAKO WA
KIROHO
Huyu ni mtu wa muhimu sana na nimemweka wa kwanza.Bila roho
hakuna mwili
Bila roho mwili wako unakua umekufa.Unahitaji ukue kiroho na
upande viwango kila wakati. Ili uweze kuvutia mafanikio ya nje.Ukishindwa hapa
hata ukiwa bilionaire inaweza kua kazi bure. Hutaweza kuzifurahia.Tafuta mtu wa
kukulelea kiroho.
Mtu wa kukufundisha kumcha Mungu.Najua unakwenda kanisani
lakini kuna tofauti ya wanafunzi wale 3 waliokua karibu na Yesu 12 na wale 70.
Unapokua karibu na mtu mmoja ambaye anakulea kiroho lazima ukue kiroho.Hata Yuda Iskariote
alikua mwanafunzi wa Yesu lakini Hawakuenda wote kwenye Maombi
mlimani.Alikwenda na wale watatu.Mara ya mwisho kuwasiliana na Mlezi wako wa
Kiroho ni lini?Kama huna katafute mtu wa kukulea kiroho sifa nimezitaja hapo
juu.Mtu huyu anatakiwa akufahamu vizuri na wewe umfahamu vizuri.
Yaani muwe na
mahusiano ya karibu sana. Sio leo upo kwa huyu kesho uko huku. Mtu huyu awe
anafuatilia maendeleo yako ya kiroho kwa karibu sana.Haijalishi unasali wapi
kule ndio kunahusika na ukuaji wako wa kiroho. Ndio maana hatufundishwo
biashara kule.
Hapa ni kwa muhimu sana. Ukiwa vizuri kiroho mahusiano yakawa
na tatizo hutafika mbali.Ukiwa vizuri kiroho ndoa ikasumbua nayo ni tatizo.Tafuta
mtu wa kukulea kwa upande huu pia mtu aliefika mbele zaidi yako. Aliefanikiwa zaidi
yako.Kama unatafuta mchumba tafuta mtu alie kwenye ndoa na amefanikiwa.Ukimtafuta
single mwenzako atakupoteza.Mtu huyu
awe karibu yenu kabisa kulea mahusiano/ uchumba au ndoa yenu. Hakuna alie
zaliwa anajua kila kitu tunajifunza hapa duniani kwa waliotutangulia na waliopo
pia.
3. MLEZI WA MAONO
YAKO/NDOTO ZAKO/MALENGO YAKO/BIASHARA YAKO/PESA. (COACHER).
Mtu huyu ni wa muhimu pia katika maisha yako. Unataka
kumiliki utajiri wa dollar billion moja lazima utafute mtu wa kukulelea na
kukuwezesha ufikie huko. Huwezi kwenda mwenyewe.Unahitaji mtu wa kukuongoza kwenye
kila unachotaka kukifanya. Wengi wanakata tamaa kwa kua hawana watu hawa wa
kuwalelea.Mtu huyu anatakiwa awe anakufuatilia hatua kwa hatua kwenye kile
unachokifanya.Awe anapata taarifa za maendeleo yako kila wakati ikiwezekana
hata kila week.Ukipata mafanikio yeyote ajue pia ukipata changamoto ajue.
Mtu huyu anatakiwa awe amekupita kwenye kile unachokitaka na
hapa huendi kua Follower anakwenda kukutengeneza wewe uwe kiongozi. Uweze
kusimama mwenyewe na hatimae uongoze wengine.Kwa Tanzania wapo watu wanaofanya
kazi hizi kwa malipo pia. Lakini hapa unaweza kuanza na mtu.ambaye una mahusiano
nae ya karibu awe anakulelea.Siku hizi teknolojia imekua rahisi sana unaweza
kua na mawasiliano na mtu yeyote unaemtaka popote alipo duniani. Unaweza
kujifunza pia vitu vingi sana kupitia mitandao hii kama hapa kwenye group.Unaweza
kusoma vitabu na vitu vingi sana vile.unavyovitaka.
Unawezaje kumpata mtu huyu? Matajiri wako bize sana ni kweli na wakati mwingine
hawana muda wa kuwepo kwenye group kama hili.Kitu cha muhimu ni wewe
kujichanganya na watu jenga mahusiano mazuri na watu lazima utawafikia watu
hawa.Unaweza kwa kuanza kusoma vitabu. Fanyia kazia unayoyasoma.Sio lazima awe
mtu mkubwa kama Mengi ao Bakhresa. Unaweza kuanza na aliekuzidi kwa kiasi yeye
atakuwezesha uwafikie walioko juu yake zaidi na walioko juu yake watafanya
hivyo hivyo.
Naomba nimalizie kwa kusema kwamba.Kwa hiki ulichokipata leo
ukikifanyia kazi Utakua mshindi uliye zaliwa kuwa.Utafikia Hatma yako.Kwa
kufuata haya Wewe namaanisha wewe iliesoma leo.
SEE YOU AT THE TOP!