“Ukimuona
kuku kwa mganga ujue kilichomponza rangi yake”. Kataa au kubali kuwa hapo ulipo
leo hii kunapelekewa na sababu fulani fulani ambazo unazifahamu au huzifahamu.
Vivyo hivyo kuwa katika kundi la maskini au katika kundi la matajiri
kunasababishwa na mambo kadhaa.
“Utajiri” ni
sawa na “Sumaku”, Sumaku huvivuta vitu
vyenye asili ya chuma, na kuvisukuma au kuvikataa vitu visivyo na asili ya
chuma kama vile plastiki, mbao, karatasi. Ili upate utajiri (Mafanikio ya kipesa) unahitaji kuwa na tabia
zinazovutwa au kuendana na utajiri. “Kuna watu fulani, kulingana na tabia zao
hawawezi kufanikiwa”-Eric Shigongo.
Watu walio
na mafanikio makubwa ya kipesa huwa maisha yao yana mambo kadhaa ambayo maskini
hawana. Katika makala haya tumekuandalia vitu 10 usivyovijua kuhusu maisha ya
matajiri wakubwa duniani.
1.Matajiri
Wote Wamejiajiri. “Kutegemea mshahara pekee kama chanzo cha utajiri au
mafanikio ya kipesa ni sawa na kipofu anayevuka barabara”. Hakuna mtu aliyepata
mafanikio makubwa ya kipesa kwa kutegemea mshahara. Watu wote wenye mafanikio
makubwa ya kipesa tunaowaita matajiri leo hii wanafanya biashara na shughuli
zao binafsi. Historia inaonesha kuwa, matajiri wengi waliachana na ajira kabla
ya kuwa hapo walipo leo.
2.Matajiri
Wote Wanajifunza Kila Siku. Wao huwa ni wanafunzi wa mafanikio kila muda.
Hutafuta maarifa mapya kila siku, hutafuta taarifa mpya, masikini yeye anahisi
anajua kila kitu swala ambalo sio kweli. Matajiri wengi wamekuwa ni wasomaji wa
vitabu vya maendeleo binafsi, “personal development books”, vitabu kama vile
Bible, Quran, Think & Grow Rich, Law of Success, Rich Dad Poor Dad, nk.
Wengi ambao hatujafanikiwa huwa hatujishughulishi hata kidogo katika kujifunza,
nadhani hicho ndo kinachopelekea uwepo wa maskini na tajiri.
3.Matajiri
Wote Wana Mitazamo Chanya. Chuki, Vinyongo, vipo akilini mwa watu masikini.
Tajiri hana muda na hizo habari. Ndio maana tajiri yupo karibu na tajiri,
maskini yuko pekee yake. Matajiri wote wamekuwa wakiwashauri watu wote kuwa
chanya na kuepuka mitazamo hasi kwani inapingana na mafanikio ya aina yoyote
hata ya kiimani.
4.Matajiri
Wote Wana Vyanzo Vya Pesa Zaidi ya Viwili. Hakuna tajiri yoyote aliyefanikwa
kwa kuwa na chanzo kimoja cha pesa. Wengi wao huwa ni wawekezaji katika Nyanja
mbali mbali za kiuchumi, matajiri wengi wanamiliki makampuni kuanzia mawili. Ni
masikini pekee anayetegemea chanzo kimoja tu cha pesa. Mtu ana duka moja,
ukimwambia apambane aongeze duka la pili anahisi unamdanganya.
5.Matajiri
Wote Hawalalamiki. Ni masikini peke yake anayeilalamikia serikali, mwalimu,
mchungaji, familia, ndugu, na marafiki. “Mtu anayehitajika kufanya kile
unachohitaji kifanyike katika maisha yako ni wewe”-Dr Ben Carson. Watu wenye
mafanikio makubwa ya kipesa, huamini kuwa, “wana nafasi kubwa ya kubadilisha
maisha yao wao wenyewe kuliko mtu yeyote mwingine”. Mafanikio uliyonayo ni
matokeo leo, yanatokana na wewe mwenyewe sio mtu mwingine.
6.Matajiri
Hawajutii Kuwa Pale Walipo. Tajiri hajutii kuwa tajiri, siku zote hujivunia
kuwa tajiri. Hata ukisema lolote baya juu yako, hatajuta hata siku moja. Kuwa
tajiri au maskini ni maamuzi ndo maana wao huwa hawajutii.
7.Kwao Kila
Kitu Kinawezekana. Neno haiwezekani kwao halina nguvu hata kidogo. Maskini ndo
anayeishi na neno haiwezekani. Neno Haiwezekani lipo kwenye Kamusi ya
Wapumbavu. Matajiri huwa wanaishi kwa Imani kubwa sana kumshinda hata Mchungaji
au Shehe. Wanaamini kuwa kila kitu kinawezekana hasa kwa kujiangalia wao
wenyewe walipotoka na walipo muda huu. Tajiri yeyoye sio mwoga, anachoogopa ni
woga wenyewe.
8.Matajiri
Wanalala Masaa Machache Sana. Watu huwa wanajiuliliza mbona ni kazi sana
kukutana na matajiri?, Jibu rahisi tu, huwa wako “busy”. Kama maskini anashinda
kitandani amelala eti kakosa kazi ya kufanya, tajiri yeyeye huwa hana hata muda
wa kulala. Matajiri wote huwa wanafanya “kazi sana” kwa masaa mengi. “Ukilala
sana unavuna ulichokiota”. Matajiri wote wanabidii na juhudi kubwa katika
kufanya kazi. “Uvivu hulipa leo, juhudi hulipa baadae” kwa hiyo inabidi kuchagua
kulipwa leo au baadae ingawa matajiri huchagua kulipwa baadae.
9.Matajiri
Wanaiona Baadae Yao Kabla Ya Kuifikia. Matajiri huishi na ndoto, maono na
matamanio. Huwa na malengo, hatua na
mikakati inayowapeleka kule wanakotaka kwenda. Hufanya kazi usiku na mchana
kufuata ndoto na maono yao. Huamini sana katika ndoto na maono. Huamini katika
malengo.
Pia ubunifu, umakini, matumizi mazuri ya pesa,
na nidhamu ya maisha huzingatiwa sana na matajiri kwa sehemu kubwa.
“Utajiri ni
matokeo ya tabia na vitendo vya mwanadamu katika maisha yake ya kila siku”
Thanks A lot
, Wish You Successful and Strong Future.