Yakiwa yamebaki takribani
chini ya masaa 36 kufikia mwaka 2017 mwaka ambao JYB anaamini utakuwa mwaka wa
mabadiliko nimeona nikuandikie mambo muhimu ya kufanya siku hiyo ya
mwisho .
Hapa naomba ieleweke kuwa
sitaki kubadilisha mambo yako uliyoyapanga kufanya kesho Lahasha lakini nataka
nikueleze mambo ambayo ukiyafanya kesho yanaweza kufanya maisha yako yabadilike
kabisa mwaka 2017 .
Najua unaweza kuwa ulishawahi
kuyasikia mambo haya lakini kesho ukiyafanya kwa upya kabla ya sasa sita usiku
yanaweza yakaandika historia mpya na ukarudi kunisimulia mwakani 2017 .Mambo
haya ni ya msingi sana na nimelazimika kukufahamisha wewe ili uyafahamu .
1.Tafuta sehemu tulivu na anza
kutafakari
Kesho ni siku ya kutafuta
sehemu iliyotulia kabisa ,sehemu isiyo na kelele nyingi yaweza hata isiwe beach
lakini hata chumba chako kinatosha kabisa kuwa sehemu nzuri .Anza kutafakari
juu ya mwaka unaoisha ,mwaka 2016 .Tafakari ni wangapi wamekufa lakini wewe uko
hai na una sababu gani za kuwa hai leo ???.Kaa chini tafakari uzima ulio nao na
ulinzi ambao Mungu amekupa kisha mshukuru Mungu na Muahidi Mungu kulitafuta
kusudi la kuwa hai leo na kuliishi mwaka 2017.
2.Jipongeze kwa yale
uliyoyafanya .
Nikisema kujipongeza kuna
mwingine hapa anawaza kujistarehesha kwa mambo mbalimbali Lahasha !.Hapa ni
kuipongeza nafsi yako kwa maneno mazuri sana ..Jipongeze kwa yale uliyoyafanya
2016 hata kama ni madogo na hayajafikia lengo.Najua malengo yako mengi sana
hayajitimia lakini pata muda wa kujipongeza
kwa yale uliyoyafanya .Iambie nafsi yako kuwa ee nafsi yangu umefanya yote haya
kumbe hata haya mengine unaweza kuyafanya ukiamua .
3.Azimia kuachana na tabia
zinazokurudisha nyuma (Weka kiapo)
Ni lazima upate muda wa
kuangalia tabia ambazo zimesababisha kutokupiga hatua kwa mwaka 2016 na kuamua
kuziacha 2017 kwa udi na uvumba .Ndiyo kama ulikuwa na tabia za uvivu azimia
kuwa hutakuwa mvivu 2017.Kama ulikuwa na tabia za kutosoma vitabu azimia
kuachana na tabia hiyo .Katika hili ni lazima ujiwekee mkakati kambambe na
uiandike .Mifano hii inaweza kukuongoza .
-Mwaka 2017 nitahakikisha
nasoma vitabu 10
-Mwaka 2017 nitahakikisha
naamka saa kumi na moja alfajiri kila
siku .
4.Andaa taarifa yako ya mwaka
na iweke kwenye faili lako .
Hili pengine unaweza kuliona gumu lakini kumbe
ndilo lanaweza kufanya mwaka 2017 kuwa mwaka wa KUINUKA.Taarifa ya maendeleo
yako binafsi ni muhimu .Unaweza ukawaa hujawahi kufanya hili lakini anza kesho
kufanya hivyo .Taarifa yako iwe na mambo yafuatayo
- Malengo yako uliyokuwa umeweka 2016
- Malengo yaliyofikika 2016
- Malengo ambayo hayakufika 2016
- Changamoto ulizokutana nazo 2016
- .Malengo yako kwa mwaka 2017
- Mikakati ya kufikia malengo yako 2017
Joas Yunus 0656110906