*MOYO SI MASHINE*~ Laban Nzelela



Neno la Mungu linasema linda sana moyo wako ...........moyo ni kiungo ambacho ili kiobekane kwa macho ni lazima kiwe nje ya mwili wataalamu wanasema unakaa upande wa kushoto,hivyo unalazimika kumpasua mtu ili uuone moyo wake.

Kwa kuwa hatuna uwezo wa kuuona moyo lakini tunao uwezo wa kuhisi mapigo yake,kila yanapopanda na kushuka hali ya mtu hubadilika ndo maana wataalamu wakaainisha shinikizo la damu la juu na la chini vyote hivi vinategemea utendaji kazi wa moyo.

Moyo wako ni wako mwenyewe ,*sasa tunaulindaje moyo ilihali hatuuoni*, je!biblia inaposema linda moyo wako inamaanisha moyo upi?
Sitazungumzia hayo ya biblia ina maana gani kutuagiza tulinde moyo bali nataka nizungumze juu ya moyo unapenda mtu,moyo ambao unasemekana kukabidhiwa kwa mwingine na mwenyenao.
Wengi kwa kushinda kulinda mioyo yao katika eneo la mahusiano na wenza wao wamejikuta wakiwa na mabadiliko kadhaa wa kadhaa kama vile;

Ngozi ya mwili kubadilika rangi;walioshindwa eneo hili hawakushindwa miguuni bali walishindwa kwenye moyo na waliposhindwa wakaangukia kwenye kubadili rangi za miili yao wakifikiri wataheshimika kumbe sivyo.

Tabia kubadilika.;wengine baada ya kushindwa kwenye moyo wakajikuta tabia zao zimebadilika wakawa watu wakujaribu pia mioyo ya watu kwa kuwadanganya kwa lengo la kuwaumiza kama kulipa kisasi.
Yawezekana hujanielewa ,hebu fikiria kiatu ambacho kimejaribiwa sana na watu na wewe ambaye unavaa size ileile na ulipojaribu ukagundua kinapwaya kidogo ilihali ndo size yako ya siku zote,kwanini kinaonekana kupwaya?

*Kinaonekana kupwaya kwa sababu ya kujaribiwa na watu wengi*
Vivyo hivyo kwa moyo wako ikiwa unajaribiwa na watu wengi hauwezi kubaki kama ulivyokuwa ni lazima utabadilika tu kama nilivyoainisha hapo juu,si hivyo hata usemi wako utabadilika,marafiki utabadilisha pia *maana moyo ukibadilika mtindo wa maisha hubadilika*

Usikubali kujaribu mahusiano na kutokatoka bila utaratibu kama ni mcheza basketball tunasema make sure yaani when you start ,start it perfect.Acha kabisa habari za kusema labda hakuwa wangu au najaribu kama tukifika mwisho basi Mungu ndo amepanga na msipofika Mungu amepanga.Mweeeeeeeh! Waulize wana wa Israel safari ilikuwa mpango wa Mungu na hawakufika wale walioanza kwani ulikuwa mpango wa Mungu wasifike.,? mtazame Adam alipewa na Mungu lakini kupitia huyohuyo akamwacha Mungu ,"loooh mwenzangu suala si hilo bali ni vile mnavyotembea ndiko kunakoamua mwisho wenu"

Laban Nzelela
0656574760