VITU 10 UNAVYOVIOGOPA KATIKA MAISHA YAKO


Kama sio wewe basi ulishawahi kukutana na mtu ana wasi wasi, woga, hajiamini, hana furaha, hawezi hata kuomba msaada pale anapokuwa na shida ambayo inaweza kutatulika kwa haraka.

Mara zote katika maisha yetu ya kila siku binadamu huwa anaogopa vitu vifuatavyo;

1.#Kufa. 99% binadamu wote wanaogopa kufa, japokuwa wanajua kuwa kufa ni lazima. Kati ya watu 100, ni mtu mmoja ndio haogopi kufa.


2.Kupoteza #mapenzi(upendo) kutoka kwa mtu unayempenda au mtu mhimu katika maisha yako. Mfano, mzazi, ndugu, rafiki, mpenzi au mke na hata boss wako.



3.Kusikia neno #hapana. Tunaogopa sana kukataliwa pale tunapoomba kitu au kutoa mawazo kwa mtu fulani.



4.#Umaskini Leo hii mtu anaweza akafanya jambo lolote hata kuua ili mradi aondoe umaskini katika maisha yake. Mtu yuko radhi kufanya kazi yoyote angalau kupunguza umasikini.



5.#Kuzeeka. Kila mtu anajua kuwa ni lazima atazeeka lakini bado mtu anaogopa uzee. Kuna mtu unaweza ukamuamkia akakuambia eti unamzeesha au akaitikia kivingine. Kumbe anaogopa kuonekana umri mkubwa, anasahau kuwa ukikua busara ndio zinapoongezeka.



6.#Mtihani wa darasani. Hakuna kipindi ambacho binadamu anakuwa muoga kama kipindi cha mtihani. Dictator maarufu duniani kutoka Ujerumani, Bwana Adolf Lois Hitler, ambaye aliua Waisraeli zaidi ya million 6, alipoulizwa, kitu gani unakiogopa katika maisha yako? akasema; #mtihani



7.Kuongea mbele za watu #wengi(kuongea mbele ya hadhara). Kuna mtu ukimsimamisha mbele ya watu 500 au 1000 ukamuambia ongea lolote anaweza akaanza kulia. Mwingine anaweza akaanza kuongea kilugha cha kwao. Mwingine atatetemeka mwili mzima na mkimuacha dakika mbili kitakachotokea unajua mwenyewe.



8.#Magonjwa. Hata kama unapenda wanawake vipi, ukiambiwa yule msichana ana ngoma(ukimwi) hata salamu unaweza usimpe ukihisi atakuambiza. Huwa tunaogopa magonjwa sana.



9.#Kukosea. Tunajuwa kabisa kuwa hakuna binadamu ambaye hakosei lakini tunaogopa kukosea, tunashindwa kujaribu vitu vipya kwa sababu ya woga wa kukosea. "Kama hujawahi kukosea, basi wewe hujawahi kujaribu kitu kipya".



10.Kuzungumza na mtu kutoka tabaka la #juu. Mfano kiongozi, tajiri, boss wako. Ghafla boss wako anakuita ofisini kwake, huo woga, au rais anasimamisha gari mbele yako kisha anashuka anakuambia kijana vipi?, utashikwa na kigugumizi ambacho hakijawahi kutokea katika maisha yako.



NB; "Nothing to be feared, its to be understood".

Woga gani unaouna ni wa kijinga?, we ni kitu gani unakiogopa katika maisha yako?, unahisi mambo gani mengine ambayo binadamu huwa amayaogopa?