Baada ya kueleza namna ya kupata mawazo hussusani
mawazo mazuri ya kuanzisha biashara leo nataka nikueleze mambo ya kufanya baada
ya kupata mawazo mazuri ya biashara .Mambo haya hayako kwenye mtaala wowote wa
darasani hata kama utaenda kusomea Havard .Unapopata mawazo mazuri ya biashara
anza kufanya yafuatayo mara moja bila kuchelea :
1.Chuja na Weka vipaumbele
vya mawazo yako
( Filter your ideas &Priotize them)
Kuna wakati unaweza kupata
mawazo mengi na ukashindwa ufanyie kazi wazo gani .Unapokuwa na wazo zaidi ya
moja ni ngumu sana kufanyia kazi mawazo yote kwa wakati mmoja hivyo unapaswa
kukaa chini na kuangalia wazo gani unapaswa kuanza nalo kwa kuzingatia uhitaji
,rasilimali ulizo nazo n.k
Watu wengi wameshindwa
kuanzisha vitu kwa sababu wanataka waanze na mawazo yote waliyonayo kwa wakati
mmoja jambo ambalo hupelekea kushindwa kufanyia kazi wazo lolote .Iko hivi
kwamba unapokuwa na wazo zaidi ya moja na unataka kufanyia kazi yote kwa wakati
mmoja kinachotokea kinaitwa "ideas conflict " . Hii ni kama vita
inayotokea akilini na kupelekea kushindwa kuamua kama hutakuwa makini .
Ni muhimu sana ukamaliza
jambo moja (focus on one thing) halafu ndipo jambo lingine lifanyike kinyume na hapa utakuwa kama fisi aliyetaka
yote kwa pupa mwisho akakosa yote .
2.Tafuta Taarifa juu ya
wazo lako
(Find information/Do Research)
Baada ya kupata wazo la
kuanza nalo ni muhimu ukaanza kutafuta taarifa sahihi kuhusiana na wazo
unalotaka kufanyia kazi .Taarifa hizo ni pamoja na taarifa za washindani wako
wanafanyeje ,taarifa za masoko ,taarifa juu ya changamoto na hatari zinazoweza
kutokea kama utaweza kufanyia kazii wazo
lako .
Taarifa hutoa picha (blue
print) ya namna wazo lako linavyoweza kufanikiwa au kushindwa .Hii ni muhimu
sana lakini kwa bahati mbaya watu wengi wameshindwa kuendelea au kuanzisha
biashara kwa sababu hawana taarifa au wana taarifa ambazo si sahihi kuhusiana
na kile wanachoweza kufanya .
Angalizo ni kuwa usimtume
mtu akutafutie taarifa ,tafuta mwenyewe taarifa
maana taarifa ya kuletewa huwa inadanganya .
3.Tafuta Maarifa ( Seek
Knowledge)
Ugonjwa mkubwa wa watu
wengi Hussusani watanzania ni kwamba hawataki kutafuta maarifa na kukuza
ufahamu wao .Ni watu wanafanya vitu kienyeji .Hawataji kujifunza lakini
wanataka matokeo makubwa wakati hawana maarifa.
Mwaka huu unapowaza kumiliki biashara yako waza kutafuta
maarifa .Maarifa ndiyo nguvu yako ,maarifa ndiyo yatakufanya ufanye tofauti na
wengine .Maarifa ndiyo yatakufanya uendelee hata kama mazingira ni magumu .
Azimia kuanza kusoma vitabu
na kufuatilia kwa upana kile unachowaza kufanya .Hudhuria semina mbalimbali
hata kama ni za kulipia .Jiunge na makundi ya watsap na Telegram mazuri
yanayoongeza vitu kila siku achana na makundi yanayongelea habari za michezo
,udaku ,umbeya na matukio ya watu .Anza kufuatilia vitu kwenye mtandao kupitia
simu yako na utaona badiliko na matokeo makubwa .
Joas 0656110906 (Jyb)