NITAMILIKI BIASHARA YANGU SEHEMU YA TATU ~Jyb


   




Habari ya leo ndugu yangu uliyeamua kufanya biashara mwaka Huu !

Nikupongeze kuwa umeamua vizuri sana na matunda yake utayaona mbeleni . Huwezi kuamini kuwa siku ndiyo zinakimbia hivyo .Ushauri wangu ni kuwa ile tabia uliyokuwa nayo ya kusema nitafanya kesho ,nitafanya mwezi ujao ,nitafanya....naomba uachane nayo kabisa mwaka huu na amua kufanya leo .Kwanini ufanye leo? ni kwasababu kesho hatuijui na hatujui kama tulivyonavyo na mawazo tuliyonayo yatafanya kazi kesho .

Siku moja rafiki yangu Hans Mkurugenzi wa HAYATE Organic Farms anayejihusisha na ulimaji wa STRAWBERRY na BLACKBERY aliniambia kuwa JYB sasa mwaka umeanza ni mwendo wa kukimbizana tofauti na ilivyokuwa mwaka jana.Nilimpongeza nikasema umeamua vema na matokeo utayaona badae kabla mwaka haujaisha .

Niachana na hayo nilikuwa tu najaribu kuamsha akili yako na kukuonesha jinsi gani muda siyo rafiki .Muda ni sasa anza sasa  wala si kesho kama unavyoweza kuwa unafikiri .

Leo  katika hatua ya tatu niliahidi kukueleza jinsi ya kupata mawazo ya kibiashara .Watu wengi wamekuwa wanalalamika kuwa hawana mitaji lakini kumbe ukifuatilia shida si mtaji shida ni kwamba hawana mawazo .Na ukweli ni kuwa msingi wa biashara na mambo makubwa unayoyaona duniani yakifanyika na yanayoeendelea kufanyika yanatokana na mawazo ya watu .

Mawazo yanafananishwa na mbegu(seeds) ambazo zikipandwa huzaa mbegu nyingi zaidi .Nilazima uwe na mbegu za mahindi zipandwe kwenye udongo sahihi ndipo unaweza kupata mahindi mengi zaidi .Mawazo yako ndiyo yatakufanya kuwa na biashara mwaka huu kwa hiyo usitafute kwanza mtaji ,tafuta kwanza wazo maana mawazo mengine ni mitaji tosha kabisa.

Zifuatazo ni njia zilizodhibitishwa kimataifa za namna ya kupata mawazo mazuri hussusani mawazo ya biashara .

1. Soma vitabu kila siku(read books)

Ukitaka kupata mawazo mapya hakuna namna utakwepa kusoma vitabu kila siku na kupata maarifa mapya .Kupitia vitabu unaweza kupata wazo zuri kupitia maarifa unayopata .Kwenye vitabu yapo mawazo mazuri ambayo unaweza kukutana nayo na ya kukusaidia .Jambo moja ambalo nataka niliweke wazi hapa ni kuwa wazo lako si lazima sana liwe jipya .Unaweza kupata wazo ambalo tayari lipo lakini wewe ukariboresha .

Kama  hukuwa mtu wa kusoma vitabu amua sasa kuanza kusoma vitabu ambavyo ndivyo vyenye mawazo mengi yanayoweza kukusaidia .Soma vitabu vya ujasiriamali na humu utakutana na mawazo  mazuri .


2.Kuwa mtu wa kuchunguza vitu (Observe things)

Hii pia ni njia ambayo inasaidia kupata wazo zuri .unapopata ziara kwenda mahali fulani ni njia nzuri ya kujifunza na kupata mawazo mapya ,chunguza sana vitu utakavyovikuta huko .Unaweza kupata wazo kokote kule kama ni mtu unayechunguza vitu .Kuna watu wao wakisafiri njia nzima wanalala tu ,hawa hawapendi kujifunza na kupata mawazo kwao si kitu rahisi na chepesi .

Wakati wa sikukuu ya Krismasi ya mwaka 2016 nilipata kwenda Mbeya ambako ndiko wanafamilia tulikuwa tunakutana .Nikiwa huko niligundua kuwa Mbeya bado haijaamka sana na yapo mengi ambayo bado hajafanyika na hata kama yanafanyika hayafanyiki kwa ubora na ustadi ...Ni sehemu ambayo ukikaa unaweza kufanya vitu vingi sana 

3. Peruzi Kwenye mitandao (web surfing) ;

Dunia ya leo ya Teknolojia ya Mawasiliano na Habari(TEHEMA) imeturahisishia vingi lakini kwa uzembe wetu tumeshindwa kutumia mtandao vizuri .Tuna simu nzuri sana ambazo kupitia hizo tunaweza kujifunza mambo mengi lakini simu zetu zimekuwa za kuchat tu watsap na  kubadilisha profile zetu facebook..

Siku moja nilikuwa naperuzi kwenye mtandao wa youtube ,nikakuta video moja ambayo imeonesha mawazo 40 ya biashara ambayo unaweza kuyafanyia kazi .Nilikaaa chini naa kuanza kuisikiliza ,ukweli ni video nzuri sana na mawazo yote ni mazuri

Acha kuchat tu mpendwa tumia simu yako kujifunza vitu ...sisemi uache kabisa kuchat lakini tumia  muda mwingi kujifunza .


5. Penda kuandika (Keep Journal)  

Kimsingi huwa tunazalisha mawazo mengi sana kwa siku lakini hatuna utamaduni wa kuandika mawazo yanayokuja akilini mwetu .Kuna mawazo tuliyapoteza kwa kutokuandika na kuyapuzia na hayo watu wengine walivyoyapata wamekuwa matajiri .Mawazo yatakuja popote na muda wowote kwa hiyo ni muhimu kuwa na journal .Simu yako ya mkononi inaweza kukusaidia au Diary book .Katika mawazo mengi unayozalisha na kuyaandika utapata wazo zuri .

6. Tafuta marafiki wapya na wazuri :

Ni muhimu kuhakikisha kuwa unapata marafiki wapya kwa namna yoyote  .Kuna watu kwa mwezi hawatafuti marafiki wapya na wamekuwa ni watu wa kukaa na watu wale wale ,wenye tabia na mawazo yale yale na wamewafanya wasifikirie zaidi ya wanavyofikiri na sasa wanasema hawana mawazo ya kibiashara .

Ndugu, watu waliofanikiwa na wanaofanikiwa wana tabia ya kutafuta marafiki wapya ,wenye mawazo mapya ,mitazamo chanya na kiu ya mafanikio.Hakuna namna utapata mawazo mapya na mazuri kama unakuwa na marafiki wale wale .


Kwa leo tuishie hapa kesho  nitakueleza vitu vya kufanya baada ya kupata wazo zuri la kibiashara ikiwa ni sehemu ya NNE  .Usikose kabisa kufuatilia mfululizo huu kama kweli una nia ya dhati ya kuanza biashara yako kwa mwaka huu.




Joas 0656110906