NITAMILIKI BIASHARA YANGU SEHEMU YA PILI ~Jyb




Jana nilikueleza baadhi ya sababu zinazokulazimu kuanzisha biashara yako mwenyewe kama hukusoma bonyeza hapa kusoma 

Leo tutaendelea kuangalia sababu zingine ambazo zitakufanya uanzishe biashara yako mwaka huu hata kama uko kazini .

Biashara yako ndiyo usalama wako

Moja ya hofu ilyotanda makazini (kwenye ajira) ni usalama wa kazi (Job security) .Ukiwa umeajiriwa ajira yako si salama yapo mengi ambayo yanaweza kutokea na hivyo unaishi kwa wasiwasi mwingi uwapao kazini na mara nyingi nidhamu ya woga  ndiyo hutawala eneo lako la kazi ili kumfurahisha mwajiri .Jambo hili siyo baya lakini ukweli linatafuna maisha yako ya baadaye maana maisha ni safari ndefu.

Mwaka huu  yamekwisha ni mwaka ambao hutaishi kwa wasiwasi maana utaanzisha vyako hata kama ni genge litakuwa lako si la mwingine ...hata kama ni kituo cha kutoa ushauri wa kitaalamu ni chako na si cha mwingine .Ndiyo chako ni chako tu ndivyo waswahili wanavyosema .

Ni ukweli usioweza kupingwa  kuwa mfumo wa ajira unawafanya watu wajengwe katika misingi ya hofu na kutojiamini na kama ndiyo hivyo hatma za maisha yetu yaliyojawa na hofu ni mbaya sana .


Biashara yako(vitu vyako) ndiyo urithi wa watoto wako na vizazi vyako

Mtoto wako hautamrithisha kazi yako maana ulipo si pako lakini kama utaanzisha vyako utakuwa unaandaa mazingira ya mtoto wako .Kuna dhana kuwa elimu ndiyo urithi wa mtoto lakini ukweli siku hizi elimu bila mwelekeo haileti tija .Ni muda wa kuangalia baada ya kupata elimu nini mtoto ameandaliwa ?.

Watanzania wengi wanadhani kazi zao nzuri ndizo za watoto wao hapana mtoto wako fahamu kabisa wakati akimaliza shule atakuja kukuuliza wewe umpe kazi.Wakati unaendelea na kazi yako anza kuwaza kuweka misingi na maandalizi ya watoto wako hata kama unawaona bado wadogo kesho watamaliza shule na kurudi kwako .Andaa mazingira ukiwa bado una nguvu na rasirimali za kutosha maana siku zilizo mbaya zinakuja ambazo uwezo wa kufikiri ,nguvu na rasirimali nyingine hautakuwa nazo au zitakuwa zimepungua .


Biashara yako (vitu vyako ) ndivyo vitakuza uelewa/ufahamu wako

Hapa kuna wengine wanaweza aidha wasinielewe au kunielewa vibaya .Ukiwa kwenye vitu vya mwingine  huna muda mwingi wa kujifunza vitu maana unafuata ratiba na utaratibu wa mwingine tofauti na ukiwa una mambo yako ambayo yanakufanya ufikiri kwa kina juu ya nini ufanye ..Unapata muda mwingi wa kutafakari vitu vyako kwa mapana zaidi  na kuongeza maarifa zaidi .

Siri ni hii kadri unavyoitumia akili yako ndivyo akili yako inavokuwa na kuongezeka na hii hufuata kanuni ya Baolojia ya law of use and disuse inayosema kuwa "kadri kitu kinavyotumika sana kinaongezeka na kama hakitumiki kinapotea"

Joas (Jyb) 0656110906

Kesho tutaangalia namna ya kupata wazo la biashara kwa mwaka huu usikose kabisa mfululizo huu utakaokufanya uanze biashara yako (vitu vyako ) mwaka huu.