Habari yako ndugu msomaji wa makala .Natumaini umeshaandika malengo yako ya mwaka na kama hujaandika wiki hii isiishe Kabla hujaandika malengo yako.Ninachoweza kukwambia ni kuwa kuweka malengo ni hatua ya kwanza ,kuweka mpango utekelezaji wa lengo ni hatua ya pili lakini kufanyia kazi mpango uliojiwekea ndiyo hatua itakayoleta matokeo makubwa katika maisha yako.
Mwezi huu tutakuwa
tukiangalia namna ya kumiliki biashara yako .Sielewi kwanini imeniingia akilini
hii lakini naamini kuwa watu wengi wameweka malengo ya kuanzisha biashara
lakini hawajui watafanyaje .Wameweka lengo la kuanzisha biashara lakini
akiangalia pesa aliyonayo anakata tamaa.Mwezi huu nitaenda na wewe na
kuhakikisha unaanza biashara hata kama watu wanaogopa na watu wengi
wanakuogopesha kutokana na hali hii ya uchumi.
Leo nataka nikwambia katika
hatua ya kwanza ya kumiliki biashara yako nataka nikueleze kwanini unapaswa
kuanzisha biashara yako (vitu
vyako ) kwa mwaka 2017 hata
kama hukuwahi kuwaza hivyo .Zifuatazo ni sababu ambazo rafiki yako JYB anaona
zinafanya wewe uanzishe biashara yako 2017.
1.Kuanzisha biashara ni
Mpango wa Mungu
Mpango wa Mungu ni kuwa
kila mtu amiliki na afanye vitu vyake.Mantiki ya kutawala ni pamoja na
kuanzisha vitu vyetu wenyewe na kutokuwa na Kuingiliwa na mtu yeyote .Hapa
haimanishi wewe uache kazi hapana inamanisha hata kama unaendelea kufanya kazi
kwa mtu utafute eneo lako la kutawala .Eneo la kujidai .Eneo ambalo hakuna mtu
yeyote atakayekuingilia katika eneo lako .Huo ndio mpango wa MUNGU ambao watu
wengi wameshindwa kuelewa kwa mapana yake na ndiyo sababu kubwa inayonisukuma
nikwambie kuwa lazima ufikiri kuanzisha biashara yako(vitu vyako) hata
kama hukuwaza kufanya hivyo tokea unazaliwa.
2.Hata watu wa Agano la
Kale na Jipya walifanya biashara
Najua wewe unaweza kuwa
huamini Biblia na pengine huwa hupendi kabisa kusikia lakini leo naomba iwe
siku ya kwanza kusikia mifano hii michache ya watu wa agano la kale na jipya
ambao nao walifanya biashara .Mistari hii ya Biblia wakati naisoma leo hii
imenisukuma nichukue Simu yangu nakuanza kukuandikia wewe ili ufahamu kuwa
biashara haijaanzishwa na akina Bilgate wala akina Mengi tu lakini kumbe
ilikuwepo toka zamani na watu walihimizwa kufanya biashara.Mistari hii ya
Biblia ikupe hamasa kubwa ya kuanza biashara .
A. Mwanzo 34:10 Nanyi mtakaa nasi, na nchi
hii itakuwa mbele yenu; kaeni, na kufanya biashara humo, mkapate mali humo.
B. Isaya 23:18 Na biashara yake na ujira wake utakuwa
wakfu kwa Bwana, hautawekwa hazinani wala hautawekwa akiba; bali mapato ya biashara yake yatakuwa
mali zao wakaao mbele za Bwana, wapate kula na kushiba, na kuvaa mavazi ya
fahari.
C.Ezekieli 28:5 kwa hekima yako nyingi, na kwa biashara yako, umeongeza
utajiri wako, na moyo wako
umeinuka kwa sababu ya utajiri wako
D. Mathayo 22:5 Lakini hawakujali, wakaenda zao, mmoja
shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake;
Naweza kuwa nimekuboa kwa
mistari hiyo lakini nimeona kabisa inatoa hamasa ya wewe kuanzisha biashara
hasa mwaka huu ambao JYB anataka kila mtu aanzishe biashara .
3.Biashara yako ndiyo
maisha yako .
Wakati tunasoma enzi zile
kabla hatujaanza kuzeeka kulikuwa na methali isimayo kuwa "Mtegemea cha nduguye hufa
maskini " .Methali hiyo
sikuwa naielewa kwa kipindi hicho na sasa baada ya kuwa mtu wa kufuatilia vitu
nimeanza kuielewa .Ukweli ni kwamba vitu vyako ndivyo vitakupa utajiri siyo vya
mwingine .Hata kama uko wapi na unafanya kazi wapi hili unapaswa kulielewa hili
kabisa ...Hakuna mwajiri chini ya jua labda azaliwe mwaka huu anayetaka
ufanikiwe kama unavyohitaji wewe...Kuna vitu anaweza kukufanyia ukadhani kuwa
anataka ufanikiwe kumbe ndiyo anafisha ndoto yako ...
Kwa leo Niishie hapa
,azimia kuanza vyako ,,,Usikose mwendelezo huu wa kujua kwanini unapaswa kuanza
biashara .
@Joas 0656110906