NITAMILIKI BIASHARA YANGU SEHEMU YA TANO (5) ~ Jyb





Baada ya kuwa umepata wazo la biashara kuna mambo kadhaa unapaswa kufanya kuelekea kumiliki biashara yako.Mambo hayo watu wengi wamekuwa  hawafanyi kabisa na hii imesababisha kutoanza biashara au  biashara kutopiga hatua kubwa .Vitu vya kufanya baada ya kuwa umepata wazo ni pamoja na :
1.Andaa mchanganuo wa kibiashara (business plan)


Inashauriwa kuwa kabla ya kufanya biashara uandae mchanganuo wa biashara yako ili kujua unahitaji mtaji wa kuanzia kiasi gani ,wateja unaowalenga ni watu gani ,washindani wako ni watu gani n.k .Mchanganuo huu ndio hata taasisi na watu wanaoweza kukusaidia na kuwezesha wazo lako huwa wanahitaji .

Wito wangu ni  kuwa tuache kufanya mambo kienyeji ill tuboreshe na tupige hatua katika biashara zetu na watu washangae .Mtu mwingine naona anaanza kujiuliza kuwa " hivi hata biashara yangu ndogo nayowaza nitahitaji mchanganuo wa biashara???"  Jibu ni ndiyo .Kila kiashara inahitaji kuwa na mchanganuo wake ili iwe yenye tija.

Kwa bahati nzuri rafiki yangu Lendian  Bigoli 0788603066 ni mtaalamu wa kutengeneza mchanganuo wa biashara unaweza kumtafuta kwa njia ya simu akakusaidia ...Bei zake ni msaada kabisa tosha kwako wewe uliyeamua kuanzisha biashara .

Kupitia mtandao pia unaweza pia kupakua (download) mifano ya mchanganuo wa biashara ukaanza kuandaa mchanganuo wako lakini nakushauri uwasiliane na wataalam wakusaidie .

2. Andaa mpango wa kimasoko (Marketing plan)
Ni muhimu sana wakati hujaanza kuingia kwenye biashara hili nalo ukaanza kulifikiri .Biashara nyingi nimeshuhudia zikifa kwa kukosa wateja kwa sababu wakati zinaanza hakukuwepo na mchango wowote wa kimasoko.

Baada ya kuandaa mpango wa biashara kaa chini tengeneza mpango wa kimasoko ili ujue unaingia na mbinu gani katika soko hata kama washindani ni wengi .Ndiyo , acha kufanya mambo kimazoea amua kubadilika na kufanya mambo kwa utofauti na kwa waredi .

Kama hujui namna ya kuandika rafiki yangu Franklin 0766 133 413 ni mtaalamu mwenye shahada ya kwanza katika masoko na amefanya kazi nyingi .Pata muda umtafute na akuelekeze hata kwa njia ya mtandao namna ya kuandika mpango wa kimasoko.

3.Tafuta mtaji

Baada ya kuandika mpango wa biashara na masoko ni muda muafaka wa kutafuta mtaji wa kibiashara .Angalizo Hata kama utapata fedha za mtaji bila kuwa na mipango inayoeleweka hela yako haitaonekana na inaweza kupotea kabisa ukashangaa.Kupata mtaji sehemu yenye mipango ni jambo rahisi kabisa  kulio kupata mtaji sehemu ambayo unachotaka kufanya hakielewiki kimaandishi .



 Joas 0656110906 
Habari Njema kwako juu ya Uandishi wa Mpango wa biashara

Siku ya Jumamos tarehe 3/6/2017 pale Jengo la City Furniture lililoko Kariakoo darajani (Gerezani) Jirani na Mkuki House ghorofa ya tatu chumba namba 309 , JOINT PROFFESSIONALS CO. LTD  Kwa kushirikiana na JYB pamoja na VIPAWA LINK ASSOCIATIONS wamekuandalia mafunzo ya namna ya kuandika mchanganuo /mpango wa biashara kwako wewe .
Hii ni nafasi adhimu kwako wewe mjasiriamali na mafunzo haya siyo ya kupuuza kwani yamekuwa hayafundishwi kokote hata mwalimu wako wa biashara anaweza kuwa hakukueleza vizuri kuhusu hili .

Lazima ufahamu kuwa uandishi wa mchanganuo wa biashara ni gharama sana lakini siku hiyo utajifunza kwa gharama ya sh 10,000/= tu na mara baada ya hapo utakuwa na uwezo wa kuandika na utaweza pia kuanza kuwaandikia wengine na ikawa sehemu yako ya kujipatia kipatao .Hii siyo ya Kupuuza .

Tutakuwa na mtaalamu aliyebobea katika uandishi wa wa mpango wa biashara na miradi ndugu Lendian Bigoli Mkurungezi wa Sound Mind Consultants ambaye ameandika   miradi mingi sana na mpaka sasa .Njoo upate maarifa .

Nafasi zipo arobaini tu (40)  Hivyo tuma mchango wako kujiandikisha kupitia namba hizi  0657267074 /0744630713 /0656110906 .Nafasi hizi ni chache changamkia fursa hii adhimu bila kuchelea maana waswahili husema "mchelea mwana kulia hulia yeye"